tangazo

Tuesday, July 9, 2013

BAADHI YA MAGAZETI YA LEO 09/07/2013 TZ.

DSC 0093 2f26f
DSC 0094 41f6e
DSC 0095 18c25
DSC 0096 ff9d6
DSC 0097 ce2d6

DSC 0098 44b89
DSC 0099 492cb
DSC 0100 fa6a6
DSC 0101 15811
DSC 0102 75dee
DSC 0103 002ef
DSC 0104 cb495
DSC 0105 c51ea
DSC 0106 7d8e2
DSC 0107 77aa8
DSC 0108 62ae5
DSC 0109 7a8c5

MWANAFUNZI AJILIPUA KWA MOTO KISA MAPENZI.



MWANAFUNZI wa Chuo cha Ufundi (VETA), mkoani Dodoma, Taliki Juma (22), amedaiwa kujiua kwa kujilipua kwa petroli kisa mapenzi.
Taarifa zinasema, kufuatia moto mkali uliotokana na petroli hiyo, mbali na mwanafunzi huyo aliyejitia mhanaga kwa mapenzi, watu wengine wanane waliokuwa karibu na moto huo nao walijeruhiwa vibaya.
Akithibitisha, leo Kamanda wa Polisi wa mkoa, David Misime, amesema tukio hilo lilitokea jana mida ya saa 12.30 jioni katika Kitongoji cha Machaka, Kata ya Nzughuni.
Kamanda alifafanua kwamba mapema mwanafunzi huyo alinunua lita tano za mafuta ya petroli katika kituo cha mafuta cha Nanenane na kisha kujilipua na kisha kwenda kujilipua akiwa katika saluni ya Irene Mapunda ambaye inasadikiwa alikuwa mpenzi wake.
Alisema, mwanzoni watu waliokuwa karibu naye walijaribu kumsihi asijilipue lakini hawakufanikiwa, kwani aliwasha kibiriti ndani ya saluni hiyo na kusababisha moto mkubwa kulipuka ambao uliwaunguza wengine waliokuwa karibu naye pamoja na mali zote zilizokuwa ndani ya Saluni hiyo kuteketea.
"Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa chanzo cha tukio hilo ni wivu wa kimapenzi, hata hivyo Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma linaendelea na uchunguzi wa kina juu ya tukio hili," ilieleza taarifa ya Kamanda wa Polisi.
Taarifa iliwataja waliojerihiwa kuwa ni Mugina Hessein (32), Benson Mushi (11) Japhet Japhet (18), Meshack John (18), Swaibu Kassim (20),Ester Silau (30), Shaban Pili (20) na Fedrick Gabriel (21) ambao wote wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma na tathimini ya hasara iliyosababishwa na moto huo bado haijafahamika.

CHADEMA WASUSIA KONGAMANO LA TCD.

MAPIGANOARUSHA CHADEMA11 a80f6

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema hakitashiriki kongamano la amani lililoandaliwa na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), chini ya ufadhili wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Oganaizesheni na Mafunzo wa chama hicho, Benson Kigaila, alisema chama chake kinazo sababu nyingi za kususia kongamano hilo.

Katika taarifa hiyo, Kigaila alimtuhumu Mwenyekiti wa TCD, James Mbatia, kwamba amekiuka maazimio ya kikao cha kuteua mwezeshaji wa mkutano huo na badala yake amefungamana na Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uteuzi.Alisema Chadema haitashiriki kwa sababu amani ya nchi haijadiliwi na watu 70, bali amani inatengenezwa kwa kuzingatia uwepo wa mazingira ya haki na usawa.


Kigaila alisema Serikali, ambayo inatuhumiwa kwa uvunjifu wa haki za binadamu, haiwezi kujisuluhisha yenyewe na kuongeza kwamba amani si mali ya vyama vya siasa, bali ni tunu inayohusisha wadau mbalimbali.Alisema Pinda, ambaye amekuwa mstari wa mbele kutoa lugha za uchochezi, chuki, uhasama, ubabe, ukiukwaji na za vitisho, hawezi kuwa na fursa ya kuwa mwenyekiti wa kongamano la amani.Kigaila alisema chama chake hakitashiriki kwa sababu Serikali ya CCM imejaa unafiki, kwani imekuwa ikihubiri amani mchana wakati usiku inachochea udini na kuwagawa Watanzania kwa misingi ya imani za kidini na vyama.“Tumepokea barua saa saba leo (jana) kutoka TCD ikitualika kushiriki kongamano la amani, tumekutana kwa dharura kujadili mwaliko huo wa ghafla.“Tunataka umma utuelewe kwamba tuna dhamira ya dhati ya kuona Tanzania inakuwa kisiwa cha amani, lakini hatukubali kushiriki katika vikao ambavyo viongozi hawana dhamira nzuri, hatutaki kutumia gharama ya Sh milioni 400 ambazo ni kodi za Watanzania wanyonge bila mafanikio,” alisema.Mbatia atoa ufafanuzi Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TCD, James Mbatia, aliishangaa Chadema kwa uwamuzi huo na kusema kuwa tuhuma zilizoelekezwa kwake ni za uwongo.Mbatia, ambaye pia ni Mbunge wa Kuteuliwa na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, alisema Pinda hawezi kuendesha kongamano hilo kwa kuwa yupo katika safari ya kikazi mkoani Njombe.“Ni vema wenzetu wasusia wafanye hivyo kwa jambo la msingi, lakini si katika hili. Kwanza nawashangaa wanasusiaje wakati wao walishiriki kikao cha kupanga kongamano hili Februari 7, mwaka huu Dodoma,” alisema.Kwa mujibu wa Mbatia, mada zilizopangwa kujadiliwa ni amani na demokrasia itakayowasilishwa na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Ole Gabriel na vyombo vya habari na usalama itakayowasilishwa na mwandishi wa habari mkongwe, Ayoub Rioba.

WANASWA NA JNIA KWA DAWA ZA KULEVYA,YASEMEKANA NI MTU NA MPENZI WAKE.

 

Dar es Salaam . Jeshi la Polisi Kitengo cha Kudhibiti Dawa za Kulevya, linawashikiliwa watu wawili, wanaodaiwa kuwa ni mtu na mpenzi wake kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya aina ya Heroin kilo mbili  zinazokadiriwa kuwa  na thamani  ya  zaidi Sh90 milioni.

Mkuu wa kitengo hicho, Godfrey Nzowa aliliambia gazeti hili jana kuwa watuhumiwa hao ambao mmoja ni mwanamke walikamatwa  juzi  saa 8 mchana kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA).

Alisema watuhumiwa walikuwa wakisafiri kwenda Mji wa Bangkok Thailand kupitia Addis Ababa, Ethiopia ambapo walikata tiketi ya ndege la shirika hilo.

“Walipoanza kufanya ukaguzi watuhumiwa hawa walijichomeka katikati ya wenzao ndipo tulipowanasa na dawa hizo ambazo walizificha kwenye mabegi yao katikati ya nguo,” alisema Nzowa.

 Alisema  kuwa watuhumiwa hao waligawana dawa hizo kwani walipofanyiwa upekuzi na polisi walikutwa  kila mtu akiwa na  kilo moja.

MJUKUU WA MANDELA AZUA TAFRANI JENGINE...ATAKA KUMSHTAKI WAKILI.

Mjukuu wa Mandela 

Johannesburg. Wakili wa mjukuu wa Mandela, Gary Jansen anatarajia kumfungulia mashtaka wakili wa familia ya Mandela kwa kuidanganya mahakama kuhusu afya ya Mandela.
Jansen alisema angefungua kesi hiyo jana ingawa hadi muda wa mahakama unakwisha alikuwa hajafungua shtaka lolote dhidi ya wanafamilia ya Mandela na wakili wao.
“Mteja wangu amejisikia vibaya, alipenda na anaheshimu matakwa ya babu yake na wala hakutaka haya mambo yawe hadharani hadi kwenye vyombo vya habari,” alisema Smith Wakili wa familia ya Mandela, David Smith ambaye anawasimamia binti mkubwa wa Mandela, Makaziwe, mke wa sasa Graca Machel na mke wa zamani, Winnie Madikizela Mandela aliiambia mahakama Juni 26, kupitia haki ya kiapo kuwa shujaa huyo wa Afrika, yu mahututi kiasi cha madakatri kushauri mashine ya kupumulia iondolewe.
Tuhuma za kuwa Mandela yupo mahututi na huenda akafariki wakati wowote, ilimsababisha hakimu kufanya uamuzi wa haraka ya kusikilizwa kwa kesi hiyo na hatimaye miili ya watoto watatu wa Mandela kufukuliwa kisha kuzikwa upya huko Qunu.
Hatua hiyo ya mahakama ilifanyika baada ya kuonekana kuwa Mandela aliwahi kutamka kuwa angependa kuzikwa katika eneo ambalo watoto wake wengine wamezikwa.
Gerald Bloem, Mwenyekiti wa Baraza la Mahakama ya Eastern Cape Bar alisema wachunguzi wanaweza kuwaita wanafamilia ya Mandela kutoa ushahidi kama mashauri ya kinidhamu dhidi ya wakili wa familia yataendelea.
Hata hivyo, Bloem alieleza kuwa wakili Smith huenda akakumbana na mkondo wa sheria iwapo itabainika kuwa aliidanganya mahakama kuhusu afya ya Mandela na atatakiwa kutoa ushahidi ambao madaktari watakosa pa kuupata.
Wanafamilia hao, walikataa kuzungumza lolote juu ya hatua za Jansen na mteja wake, Mandla zinazotarajiwa kuchukuliwa ingawa Denis Goldberg, rafiki wa karibu wa Mandela, alipomtembelea wiki iliyompita alithibitisha kuwa hakuwa mahututi na aliweza kunyanyua viungo vyake, sambamba na kutambua sauti.
Goldberg alizungumza na waandishi wa habari na kuthibitisha kuwa madaktari wamekataa Mandela asiondolewe mashine ya kupumulia kwani afya si mbaya hadi pale moja ya ogani zake itakaposhindwa kufanya kazi kabisa.
Wakati huo huo, Mandla amemcheka Mfalme wa Wazulu, AbaThembu, Buyelekhaya Dalindyebo ambaye alitangaza kumng’oa Uchifu, kuwa hana sifa za kufanya hivyo.
Dalindyebo alitangaza kumvua Uchifu Mandla kwa madai kuwa amepoteza heshima yake baada ya kuwa na mgogoro na wanafamilia wenzake kuhusu mabaki ya miili ya watoto watatu wa Mandela.
Mfalme huyo alisema Mandla hafai kuongoza watu wa Mvezo kwa kuwa ameipoteza heshima yake ambayo aliipata awali na kutawazwa kuwa chifu baada ya kulichafua jina la familia inayoheshimika ya Mandela.

Hata hivyo, Mandla aliikebehi kauli ya mfalme Dalindyebo akisema kuwa mfalme huyo hana msimamo na hekima.
Msemaji wa Mandla, Freddy Pilusa alisema kumfukuza Chifu kunahitaji mchakato mrefu na ushahidi wa makosa aliyoyafanya na si kuamka na kuamua kuwa unamfukuza Chifu.
“Huwezi tu kuamka siku moja na kuitisha mkutano na kufanya uamuzi kama huo,” alisema Pilusa.
Hata hivyo, msemaji wa nyumba ya kifalme, ya kabila la Abathembu, Nkos Daludumo Mtirara alisema: “Sisi tunaona kauli ya Dalindyebo kama utani tu, kwa sababu alikwishaondolewa kwenye cheo hicho miezi tisa iliyopita.
“Tunamtambua Mandla kuwa bado ni chifu kwa sababu, bado Serikali haijamuondoa Mandla katika cheo chake na anaendelea kupata haki na heshima yake kama kawaida.”
Mtirara alisema kauli ya Zwelibanzi ni ya kuharibu mila na tamaduni, kuchonganisha na kukuza jambo hili kwa sababu hata yeye hana mamlaka.
“Tunajua kuwa Zwelibanzi anavuta sana ‘Dagga’ na tunafahamu kuwa Zwelibanzi yupo katika operesheni ya kuivuruga familia ya Mandela” alisema Mtirara.

Thursday, June 13, 2013

MUUAJI WA DADA ALIYECHINJWA KAMA KUKU MIKOCHENI B APATIKANA.


MFANYAKAZI wa Jaji Kileo, Philemon Laiza (27) anadaiwa kumchinja mtumishi wa ndani wa jaji huyo, ambaye ni raia wa Kenya, Perpetua Mainab (30). 


Mtuhumiwa huyo, ambaye alikuwa ni mtunza bustani katika nyumba ya Jaji Kileo, alifanya unyama huo wiki iliyopita.

 Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Kamishna wa Polisi Kanda Maalum, Suleiman Kova, alisema mwili wa mtumishi huyo wa ndani ulikutwa kwenye dampo la kutupia takataka maeneo ya Mikocheni B.

“Tukio hilo lilitokea karibu na dampo la kutupia taka Mikocheni ‘B’, katika eneo linalomilikiwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA).

“Mfanyakazi huyo wa ndani alikutwa ameshakufa baada ya mwili wake kuchinjwa sehemu ya shingo, jeraha sehemu ya mkono wa kushoto karibu na kiganja, jeraha kwenye paji la uso na mwili wake ukiwa umetapakaa damu sehemu za kichwani,” alisema Kova.

Alieleza kuwa mtuhumiwa huyo ambaye alikuwa akifanya kazi pamoja na marehemu, alikiri kuwa na marehemu siku hiyo ya Ijumaa ya Juni 8 mwaka huu.

Alisema baada ya polisi kufanya upelelezi mtuhumiwa alikutwa na kiatu kimoja cha marehemu na nguo alizovaa siku ya tukio, ambazo zilikuwa zimetapakaa damu.

“Nguo hizo za marehemu zilikuwa zimetapakaa damu na baada ya mahojiano ya muda mrefu, mtuhumiwa alikiri kuhusika na tukio hilo.

Kamishna Kova alisema kuwa mtuhumiwa alipohojiwa alidai kuwa marehemu alitoweka nyumbani tangu siku ya Ijumaa na baada ya kubanwa na polisi mtuhumiwa alikiri kuhusika na tukio hilo.

Kova alisema mtuhumiwa bado anahojiwa na upepelezi ukikamilika atafikishwa mahakamani.

NEW TRACK: LADY JAY DEE--YAHAYA.

Tuesday, June 11, 2013

BAADHI YA MAGAZETI YA LEO JUMAANNE TZ.



3 ded5d
4 d7f0c
5 5e857

6 5d1b0
7 47585


10 bd70c

12 592b4
13 843a3
14 703f7






15 ec293

MBUNGE ASOTA RUMANDE KWA KUSHINDWA KUTIMIZA MASHARTI YA DHAMANA.

murji 39ae7
Mbunge wa Mtwara Mjini (CCM), Hasnein Murji jana alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani hapa akituhumiwa na kosa la uchochezi. Baada ya kusomewa shtaka hilo, mbunge huyo alirudishwa rumande kutokana na kushindwa masharti. Sharti hilo lilikuwa ni kuwa na pasi ya kusafiria, ambayo alikuwa ameiacha Dar es Salaam alikokamatwa.

Murji amepandishwa kizimbani ikiwa ni moja ya mkakati wa vyombo vya dola kuwasaka na kuwafungulia mashtaka watu inaowatuhumu kuhusika kuchochea vurugu ambazo chanzo chake ni kupinga ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam.

Mwendesha Mashtaka ambaye ni Wakili wa Serikali, Zuberi Mkakatu aliieleza Mahakama kuwa mnamo Januari 19, mwaka huu, maeneo ya Ligula mkoani hapa mtuhumiwa alichochea watu kutenda makosa.

Hakimu Mkazi Mfawidhi Mkoa wa Mtwara, Dynes Lyimo alisema dhamana iko wazi kwa mshtakiwa kwa masharti matatu. Kuwasilisha hati ya kusafiria mahakamani na kuwa na mdhamini mmoja mkazi wa Mtwara ambaye atasaini mali isiyohamishika isiyopungua Sh20 milioni. Sharti la tatu lilikuwa mshtakiwa kutoruhusiwa kufanya mikutano ya hadhara pasipo kibali cha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara.

Mbunge huyo anayewakilishwa na Wakili Chaula Msechu alifikishwa mahakamani hapo jana saa 3.15 asubuhi akiwa katika gari la polisi huku ulinzi ukiwa umeimarishwa. Polisi waliokuwa na silaha na wengine wakiwa na mbwa walikuwa wametanda mahakamani.

Mbali ya mahakamani, polisi walikuwa wakipita katika barabara mbalimbali za Mtwara sambamba na askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Licha ya matangazo mbalimbali ya polisi kwamba hakutakuwa na tishio la uvunjifu wa amani, baadhi ya wananchi waliogopa kufungua biashara zao na wengine wakikimbia mji.
Washtakiwa 91 chanzo mwananchi.

Translate