tangazo

Tuesday, February 26, 2013

DAU NONO LATANGAZWA ATAEMPATA ALIEMUUWA PADRI MUSHI.

 
 IGP Said Mwema

WAKATI kukiwa na taarifa kwamba maofisa wa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI) wametua nchini kwa ajili ya kufanya upelelezi wa mauaji ya Padri Evarist Mushi, Jeshi la Polisi limetangaza dau la Sh10 milioni kwa atakayefichua aliyemuua padri huyo.
Padri Mushi aliuawa kwa kupigwa risasi Jumapili iliyopita wakati akienda kuongoza ibada katika Kanisa la Mtakatifu Teresia lililopo Beit el Ras nje kidogo ya mji wa Zanzibar, ambapo inadaiwa kuwa waliomuua walikuwa wamepanda pikipiki aina ya Vespa na walimfyatulia padri huyo risasi tatu akiwa ndani la gari yake.
Wakati polisi wakitangaza dau hilo, Sheikh Ali Khamis Ali (65) mkazi wa Kitope Kaskazini Unguja, aliuawa jana kwa kukatwa mapanga mjini Zanzibar, baada ya wezi kuvamia shambani kwake.
Habari za kuaminika zilizopatikana juzi zinaeleza kuwa maofisa hao wa FBI, wako nchini na tayari na wamekutana na baadhi ya viongozi wa Serikali kwa ajili ya kuanza kazi hiyo.
Chanzo chetu cha habari kimeeleza kuwa maofisa hao walikutana na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi kwa ajili ya kuangalia ni namna gani watafanya shughuli zao katika upelelezi huo.
Pamoja na ushiriki FBI, taarifa zinaeleza kuwa maofisa wa Serikali ya Tanzania wamezungumza na taasisi za upelelezi za nchi tano, ili kuongeza nguvu katika upelelezi huo.
Taasisi nyingine inayotajwa kuwa huenda ikashiriki katika uchunguzi huo ni Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai ya Uingereza (Scotland Yard).
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Ame Silima alilithibitishia gazeti hili kwamba Serikali imeanza kufanya mazungumzo na mashirika mbalimbali ya upelelezi duniani kwa ajili ya kushirikiana nayo kuchunguza mauaji ya Padri Mushi, lakini akasema kuwa ni mapema mno kuyataja.
“Tumefuata maagizo aliyotoa Rais Kikwete kwamba tushirikishe mataifa mbalimbali kuchunguza mauaji yaliyotokea Zanzibar, siwezi kutaja kwa majina, ila tayari tumeanza kuzungumza na nchi mbalimbali,” alisema Silima.
Akizungumza mjini Zanzibar jana, Kamishna wa Polisi visiwani humo, Mussa Ali Mussa alisema kuwa hadi sasa hakuna mtu aliyefikishwa mahakamani kuhusiana na tukio hilo la mauaji.
“Hakuna aliyefikishwa mahakamani, lakini wapo watu ambao wamekamatwa wakihusishwa na tukio hili na tunaendelea kuwahoji, wengine tunawaachia,” alisema na kuongeza:
“Tumeahidi kutoa Sh10 milioni kwa mtu yeyote, atakayetoa taarifa za mauaji ya Padri Mushi, hii itakuwa kama zawadi tu.”

Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa maofisa wa FBI wamekutana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Said Mwema kuzungumzia suala hilo la mauaji ya Padri Mushi.
Tukio hili la kuuawa kwa Padri Mushi linahusishwa na matukio kadhaa ya vurugu zilizoambatana na uchomaji moto makanisa na mali mbalimbali hivi karibuni.
Moja ya matukio hayo ni lile la Jumatano ya Desemba 25 mwaka jana ambapo Padri wa Kanisa Katoliki lililopo Mpendae visiwani Zanzibar, Ambrose Mkenda, alijeruhiwa kwa risasi na watu wasiojulikana nje ya nyumba yake, saa 12 jioni wakati akitoka kanisani.
Padri huyo alipatiwa matibabu katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja na baadaye alihamishiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu zaidi.
Wakati huo huo, Sheikh Mussa Ali Mussa ambaye alikuwa kiongozi wa Misikiti ya Kitope na Mwakaje ameuawa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja, Ahmada Khamis alisema kuwa kiongozi huyo, aliuawa kutokana na kipigo alichokipata kutoka kwa wezi waliovamia shamba lake.
Kuuawa kwa Sheikh huyo kumezua hofu kwa wakazi wa Zanzibar wakidhani ni kitendo cha kulipiza kisasi, lakini Polisi imetuliza hali hiyo kwa kusema kwamba aliuawa na wezi waliokuwa wakiiba shambani kwake.
Alisema kwamba baada ya kuwafuma wezi hao wakiiba shambani kwake walimshambulia kwa mapanga na kupoteza uhai wake na kwamba hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo.

NGUVU ZATUMIKA KUZUIA MAITI ISISAFIRISHWE GEITA.


 
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Leonard Paulo

POLISI wa Mkoa wa Geita wametumia nguvu kuzuia msafara wa waombolezaji waliokuwa na mwili wa marehemu mfanyabiashara, Yemuga Fungungu (48), mwishoni mwa wiki iliyopita na kusababisha vurugu kubwa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Leonard Paulo alikuwapo wakati askari wake walipoingilia msafara huo na kusababisha vurumai kubwa.
Waombolezaji hao walikuwa wakiuhamisha mwili wa marehemu Fungungu kutoka Hospitali ya Runzewa kuupeleka katika Hospitali ya Geita.

Sakata hilo la ndugu na polisi lililotokea saa nane mchana juzi Jumamosi katika Pori la Samina, Geita na polisi wakiwa kwenye magari matatu wakiwa wamesheheni silaha mbalimbali walifika na kuzuia mwili wa marehemu kusafirishwa.

Baadhi ya ndugu wa marehemu akiwamo mkewe, wanadai kwamba Fungungu alifariki dunia baada ya kupigwa risasi na polisi wanaosemekana kwamba walimvamia nyumbani kwake usiku wa kuamkia Alhamisi iliyopita kisha kupora mamilioni ya fedha. Wanadai kwamba alipigwa risasi tumboni na kichwani katika Kijiji cha Runzewe, Wilaya ya Bukombe mkoani hapa.

Katika tukio hilo inadaiwa kuwa kiasi cha Sh360 milioni kiliporwa. Kati ya fedha hizo, Sh60 milioni zinadaiwa kwamba zilikuwa kwenye gari wakati Sh300 milioni zilikuwa kwenye masanduku mawili yaliyokuwa ndani ya nyumba.

Pia ndugu hao walidai kwamba Sh1.2 milioni zilichukuliwa na askari wawili wa kiume baada ya kumpekua mke wa marehemu kwenye nguo za ndani.

Pia askari hao wanadaiwa kupora mali mbalimbali za marehemu zikiwamo redio mbili, video kamera moja, nguo za marehemu ikiwamo kanzu, mashine ya printer, mashine ya inventor, karatasi za picha, deki mbili za kucheza CD, pamoja na nguo za mke wa marehemu.

Mapema Kamanda Paulo alikuwa ameeleza kuwa marehemu alijiua mwenyewe baada ya kumjeruhi Polisi, Fortunatus Beatus kwa risasi lakini taarifa hizo zimepingwa vikali na ndugu na jamaa wa marehemu ambao wanadai marehemu aliuawa na polisi akiwa nyumbani kwake.

Polisi kuzuia waombolezaji

Baada ya polisi kuyasimamisha magari manane yaliyokuwa katika msafara huo wa kupeleka mwili wa marehemu kwenda kuhifadhiwa katika chumba cha maiti Hospitali ya Geita, kulizuka mabishano makali kati ya Kamanda Paulo na ndugu wa marehemu.

Inadaiwa kwamba polisi walikuwa wakishinikiza mwili huo urejeshwe Runzewe, Bukombe kwa kuwa tayari ulikuwa umefanyiwa uchunguzi jambo ambalo liliwakera waombolezaji hao.

Kabla ya kamanda huyo kufika eneo hilo, msafara huo ulisimamishwa na Polisi wa Usalama Barabarani ambao walikuwa wamefuatana na wale wa Kutuliza Ghasia (FFU), wakiongozwa na Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Geita, Leonard Makona.
Baada ya kuusimamisha msafara huo, Makona aliwataka ndugu wa marehemu kumsubiri Kamanda Paulo ambaye alifika baada ya takriban dakika 10.

Mwandishi wa habari hii ambaye alikuwa katika eneo la tukio, alishuhudia ndugu wa marehemu na Kamanda Paulo wakirushiana maneno.

“Mnapeleka wapi mwili wa marehemu, ina maana hamkuridhika na uchunguzi wa daktari wa Bukombe?” alihoji kwa ukali na kujibiwa pia kwa ukali na kaka wa marehemu, Mariatabu Fungungu: “Kwa nini mnatusimamisha? Tunaomba tuite waandishi wa habari hapa ili waje washuhudie tukio hili. Kwa nini msikae ofisini?”

 Baadaye, kamanda huyo aliwaamuru askari wake kuwaingiza katika gari la polisi ndugu watano wa marehemu wakiwamo mke wa marehemu, Lucia Kilaza (23) na Mariatabu. Walifanya hivyo kwa kutumia nguvu na kisha kuondoka nao hadi katika Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Geita.

Ndugu wa marehemu walilalamikia kitendo hicho wakisema kilikuwa na lengo la kuficha ukweli wa tukio hilo.

Mke wa marehemu

Kilaza alidai kuwa kifo cha mumewe kilitokea baada ya zaidi askari 20 kuvamia nyumbani kwake yapata saa tisa usiku na kumwamuru Fungungu kutoka nje na alipogoma, ndipo walipoanza kupiga risasi na kuvunja vioo vya madirisha na milango na risasi kumpata marehemu. Pia alidai kuwa walipiga mabomu ya machozi.

Alisema baada ya tukio hilo, walivunja mlango na kuingia ndani kisha kumchukua mumewe ambaye tayari alikuwa amefariki na kumtupa nje... “Mimi pia walinichukua wakanitupa nje ya uzio baadaye wakaanza kunipekua nguo za ndani na kuchukua Sh1.2 milioni ambazo nilikuwa nimezificha baada ya kuona wameanza kufyatua risasi.”

Wakizungumzia tukio hilo, Mbunge wa Bukombe, Profesa Kalikoyela Kahigi na Diwani wa Runzewe, Yusufu Fungameza walisema Serikali inatakiwa kuingilia kati suala hilo ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua za kisheria waliohusika katika tukio.

Alipotakiwa kuzungumzia tukio hilo, Kamanda Paulo aliwaahidi waandishi wa habari kwamba angelitolea ufafanuzi jana Jumatatu. Hata hivyo, alishindwa kufanya hivyo kwa madai kwamba anapisha kwanza uchunguzi wa mwili wa marehemu kwenye Hospitali ya Geita.

Ndugu wa marehemu wamegoma kuuzika mwili wa marehemu wakitaka uchunguzi wa kina ufanyike kwa kutumia jopo maalumu la madaktari huku wakiitaka Serikali kuunda tume kuchunguza tukio hilo.

Mtandao wa ujambazi Mbeya

Katika hatua nyingine; Watu wanaodaiwa kujihusisha na matukio ya uhalifu katika mikoa ya Mbeya, Iringa, Morogoro na Dar es Salaam wamenaswa na polisi huko Mbeya.
Mtandao huo unadaiwa kuwahusisha askari mmoja wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) pamoja na wafanyabiashara maarufu wa Mbeya.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Diwani Athumani alisema jana kuwa watu 29 wanaodaiwa kujihusisha na mtandao huo wanashikiliwa na jeshi hilo.

“Askari hao mbali na kujihusisha na matukio ya ujambazi moja kwa moja, pia walikuwa na tabia ya kuwaazima majambazi sare za jeshi ambazo zilikuwa zikitumika kwenye matukio mbalimbali ya uhalifu,” alisema.

Alisema watuhumiwa wote hao wanakabiliwa na tuhuma za mauaji, ujambazi na kupokea mali za wizi na walikamatwa katika maeneo ya Mkwajuni, Chunya na Makambako na Mafinga, Iringa.

Kamanda Athumani alisema kuwa watuhumiwa 13 watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma za ujambazi, mauaji na kupokea mali za wizi, wengine saba watasafirishwa kwenda Iringa ambako ndiko watakakofikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Kamanda Athumani alisema uchunguzi wa watuhumiwa wengine 16 bado unaendelea na wataachiwa kwa dhamana na watatakiwa kuripoti vituo vya polisi watakavyopangiwa.

Saturday, February 23, 2013

KAHABA AJIFUNGUA NA KUTUPA MTOTO.

Stori:Dustani Shekidele, Morogoro
MTOTO mchanga hivi karibuni ametupwa katika Mto Kikundi mjini hapa akiwa amekufa, jirani kabisa na kambi ya makahaba wanaofanya biashara ya kuuza miili yao 

‘machangudoa’. Baadhi ya watu walioshuhudia mwili wa kichanga hicho walimwambia mwandishi wetu kuwa kichanga hicho kilitupwa na mmoja wa makahaba, hali iliyozua tafrani kwani wasichana wanaoaminika kuwa ni makahaba walikuwa wakiipinga kauli hiyo.

“We mpigapicha usiamini hayo wanayosema hao watu... tuna ujinga kiasi gani tuzae, tuue kisha tutupe mtoto sehemu yetu ya kazi?” alihoji msichana mmoja ambaye alikataa kujitambulisha.

Hata hivyo, wasichana waliojitambulisha kwa majina Pendo Komba, Rose Joseph na Amanda Athuman kwa nyakati tofauti walisema wanaofanya unyama huo ni makahaba japokuwa wenyewe wanakataa.

Walidai kuwa hii ni mara ya sita kwa watoto wachanga kutupwa kwenye eneo hilo.
Afisi mmoja wa polisi aliyekuwepo eneo hilo, (jina tunalihifadhi) wakati wanauchukua mwili wa kichanga hicho alisema wanamtafuta mwanamke aliyefanya ukatili huo ili afikishwe mahakamani.

PEMBE ZA NDOVU ZENYE THAMANI YA MAMILION ZAKAMATWA.

 
Gari la Kampuni ya GAME FRONTIERS OF TANZANIA likirejea katika Ofisi ya Kanda ya Kusini Magharibi ya Pori la Akiba la SELOU likitokea ndani ya Pori 
Hawa ni wafanyakazi wa Game frontiers of Tanzania wakiwa wamebeba pembe za ndovu


Pembe za ndovu, Risasi na Silaha zilizokamatwa
 ………………………………………………………………………………..
Na Hamza Mashole  wa  Songea- ( www.demashonews.blogspot.com)
Kampuni ya GAME FRONTIERS OF TANZANIA kwa kushirikiana askari wanyamapori wa Selou na Askari wa vijiji vinavyozunguka pori la Akiba la Selou wamefanikiwa kukamata meno ya tembo 15 yenye thamani ya milion miambili, Risasi 9, Bunduki moja aina ya RIFFLE 458 na Gobole moja ambavyo hutumika kuulia wanyama .
Doria hiyo imechukua takribani siku tatu katika pori la Akiba la Selou ikiwa ni sehemu ya kuwatafuta majangili wanaofanya mauaji ya wanyamapori katika pori hilo,
Akizungumza na mwandishi wetu Bw. Mohamed Mpapa ambaye ni mwakilishi wa kampuni hiyo ya GAME FRONTIERS OF TANZANIA, Amesema kuwa hiyo ni kujituma kutokana na motisha ya fedha anayoitoa mwezeshaji wa kampuni ya GAME FRONTIERS OF TANZANIA ndio chachu ya mafanikio ya kukamata meno,bunduki na risasi.
 Akiendelea kuzungumzia tukio hilo Bw. Mohamed Mpapa amesmea baada ya majangili kuwaona Game Frontiers Tanzania wakiwa katika doria ndani ya pori hilo huku wakiwa wamekamilika kimapigano majangili hao waliweza kukimbia na kuacha nyara hizo baada ya kuona nguvu yao ni ndogo katika kupambana na kundi la doria.
Ameongezea kwa kusema Kampuni yake imefurahishwa na mafanikio na ushirikiano uliopo kati yao, Serikali na wanavijiji kukabiliana na ujangili unaoendelea kuwamaliza tembo katika Pori la Akiba la Selou pia ametoa wito kwa jamii kuendelea kutoa ushirikiano katika kuwafichua majangili.
Nae Kaimu Mkuu wa Kanda ya Kusini Magharibi ya Pori la Akiba la Selou Bw. Bernald Lijaji amesema Pembe zilizokamatwa ni 15 pamoja na Bunduki aina ya RIFLE 458,Gobole moja na Risasi 9 aina ya 458 vimekamatwa katika Doria iliyofadhiriwa na Mwekezaji wa Kampuni ya GAME FRONTIERS OF TANZANIA

YALIYOJILI KATIKA MAGAZETI YA LEO JUMAAMOSI 23/02/2013 TZ

.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

Thursday, February 21, 2013

Simanzi yatawala, Waziri azomewa


Na: Elias Msuya, Zanzibar 
SIMANZI na vilio vilitawala mazishi ya Padri Evarist Mushi yaliyofanyika Kitope Zanzibar jana huku Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mohamed Aboud akipata wakati mgumu baada ya kuzomewa na waombolezaji kutokana na kukerwa na hotuba yake.Padri Mushi aliuawa kwa kupigwa risasi, Jumapili iliyopita wakati akijiandaa kwenda kuongoza misa katika Kanisa la Mt. Joseph Minara Miwili mjini hapa. Ibada ya mazishi iliyoongozwa na Askofu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo ilianza saa nne asubuhi katika Kanisa la Mt. Joseph Minara Miwili na kuhudhuriwa pia na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein. Baada ya misa hiyo iliyomalizika saa 6.30 mchana, msafara wa mazishi ulielekea Kitope yalipo makaburi ya viongozi wa Kanisa Katoliki. Baada ya kufika makaburini, ibada ya mazishi ilianza saa 7.30 mchana na mwili wa Padri uliwekwa kaburini saa moja baadaye. Viongozi wengine waliohudhuria mazishi hayo ni pamoja na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Nchimbi, Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbrod Slaa. Waziri Aboud alizomewa kutokana na kauli yake aliyotoa katika salamu za Serikali kuwa kifo cha Padri Mushi ni kazi ya Mungu, ambayo haina makosa. “Serikali imepokea msiba huu kwa
huzuni na masikitiko makubwa. Maumivu ya familia ya marehemu ni maumivu ya Serikali. Padri Mushi ametuachia pengo kubwa lakini kazi ya Mungu haina makosa,” alisema Waziri Aboud kauli ambayo ilipokewa kwa waomboleza kuguna wengine wakizomea hali iliyowafanya baadhi ya viongozi kuwatuliza.
Mmoja wa waombolezaji alisikika akisema: “Kazi ya Mungu ndiyo imewatuma hao wahalifu kuua kwa risasi?”

Mwakilishi wa familia, Francis Mushi alijibu kauli ya waziri huyo alipopewa nafasi ya kutoa salamu kwa kusema: “Tumeupokea msiba huu kwa masikitiko makubwa hasa kwa kuwa Padri hakuugua… Alikuwa kiungo kikubwa katika familia yetu.” Maneno ambayo yaliibua simanzi na vilio kutoka kwa waombolezaji wengi.

Hata Askofu wa Jimbo Katoliki Zanzibar, Augustino Shao aliyekuwa amekaa karibu na Rais Dk Shein alipopewa nafasi naye alisema waziwazi: “Naomba kusema kuwa, kauli hii ya mapenzi ya Mungu haipo… Hili ni suala la uovu na tusikubali kushindwa na uovu.” Kauli hiyo ilionekana kuungwa mkono na waumini.

Ibada hiyo ilihitimishwa kwa sala iliyoongozwa na Askofu wa Jimbo Katoliki Tanga, Antony Banzi.
Wanasiasa waomboleza
Akizungumza baada ya kumalizika kwa msiba huo, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbrod Slaa alisema wananchi wamechoshwa na kauli za Serikali za kuwatuliza huku watu wakiendelea kuuawa.

“Watanzania tusiendekeze kauli za Serikali za kila siku, eti Bwana ametoa Bwana ametwaa! Kifo cha Padri Mushi hakikutokana na ugonjwa wala Serikali, lakini haiwezekani kila siku Serikali iendelee na ahadi za maneno matupu.
“Haiwezekani Katibu wa Mufti, Fadhili Soraga ajeruhiwe kwa tindikali, Padri ajeruhiwe kwa risasi, kule Geita mchungaji ameuawa na mwaka jana mwandishi wa habari aliuawa na Jeshi la Polisi, tusidanganyane… tuseme ukweli,” alisema Slaa.

Akizungumzia kauli ya Rais Jakaya Kikwete ya kulitaka Jeshi la Polisi kushirikiana na vyombo vya nje katika upelelezi, alisema: “Suluhisho siyo kuleta ‘Scotland Yard’ hapa, tatizo letu tunashughulika na matawi wakati mzizi ukiwa bado haujakatwa. Tung’oe mzizi wa tatizo.”

Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia alivilaumu vyombo vya usalama kwa kushindwa kudhibiti mauaji hayo na kumtaka Rais Jakaya Kikwete kuwajibika kwa mauaji yanayoendelea nchini.

“Rais anapoingia madarakani anaapa kuwa mtiifu kwa Katiba na raia wake, lakini haya matukio ya umwagaji damu yamekuwa kawaida sasa. Damu ya mtu ni ya thamani huwezi kuinunua hata uwe tajiri.”

Wednesday, February 20, 2013

MWANAFUNZI APOTEZA MAISHA KWA KUJITEKETEZA KWA MOTO.

MSIBA WA MOTO 2 879d6

Na John Banda, Dodoma

Mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya Sekondari Nzuguni iliyopo manispaa ya Dodoma amekufa kwa kujichoma moto baada ya Mjomba wake kumchapa viboko kutokana na kosa la kutomsaidia Bibi yake kuosha vyombo.

Tukio la kifo cha mwanafunzi huyo lilitokea jana jumapili ambapo saa 11 jioni katika hospital Rufaa ya General Dodoma baada ya kulazwa kwa masaa kadhaa
.

Akisimulia kifo marehemu nyumbani kwa mwenyekiti wa mtaa wa maweni B. mjomba wa marehemu Paul Samwel 21 alisema kuwa siku hiyo ya tukio alitoka kazini kwake mapema akarudi nyumbani na kumkuta  mama yake akiingia jikoni baada ya kutoka kuosha vyombo ndipo alipotaka kujua alipo Catherine kwani siku hiyo ya ijumaa wanawahi kutoka shule.

Samwel alisema mama huyo alimjibu kuwa Katherine alipofika alitoka na hajui alipoelekea ndipo alipomsubili mpaka aliporudi akamuuliza kwamba kwanini alimuacha Bibi yake afanye kazi wakati anajua haoni vizuri ndipo akamua kukata fimbo na kuanza kumchapa alipotosheka akamuacha baada ya muda akiwa nyumba jirani alisikia kelele nyumbani.

''ndugu yangu nilikuta mjomba anaungua mwili mzima kuanzia kichwani tuliposaidia na kumpeleka hospital mwili wote haukuwa na kazi bali moyo tu ndiyo ulikuwa ukidunda pekee na jana jumapili saa 11 jioni alikata roho kwa weli ameniuma sana maana ni kama mdogo wangu maana mama yake alimuacha akiwa mdogo sana'', alisema Samwel

Kwa upande wa Wanafunzi wenzake waliofika kuomboleza nyumbani hapo walisema Marehemu alikuwa akilalamika mara kwa mara kuwa alikuwa akiteseka sana nyumbani kiasi cha kila siku kupewa adhabu za vipigo na mjomba wake huku akitaka fedha kwa Babu yake za kunulia vifaa vya shule na mahitaji mengine kama mtoto wa kike alikuwa anachapwa pia.

Wanafunzi hao Desleria Lupembe, Elika Zabron, Maria Paul na Anastadhia Boniface Wote wa kidato cha pili Nzuguni walisema kwa siku zilivyokuwa zinazidi kusogea karibu na kifo chake walikuwa wakimshangaa mwenzao huyo.

''Mara kwa mara alikuwa akituambia wakati wowote atakufa hivyo tumpe picha zetu ili awe anatuangalia na sisi hapa unayetuona tulishampa zetu, lakini alhamis akawa serios sana akasema mambo yamezidi hata jumatatu hatakuja shule na hatutaonana kwasababu siku hiyo alinyimwa hela na Babu yake mzee Samwel pamoja na kuchapwa sana huku akiambiwa amfuate mama yake'', alisema Maria paul [15]
Nae Bibi wa marehemu Juliana Samwel akizungumzia tukio hilo alisema baada ya kuchapwa na mjomba wake Kathe alichukua mafuta ya taa na kujimwagia mwili mzima na mengine akayanywa kisha akijiwasha na njiti ya kiberiti akawaka mwili mzima kiasi cha yeye kushindwa kumsaidia.

mwanangu mtoto aliungua karibu mwili mzima maana alikuwa amejiviringisha kanga toka chini mpaka juu nilipiga kelele majirani wakaja kuzima ule moto na kumbe alishaungua sana hata ngozi ilikuwa ikijichubua yenyewe, mzee Samwel angekueleza mengi lakini kaenda hospital kuuhifadhi mwili maana mama ya mrehema ndiyo leo anatoka Dar hivyo mazishi ni kesho mapema, kuhusu kifo sina cha kufanya imetokea imetokea nitafanyeje'', alisema. mama huyo wa umri kati ya 50/55 

Kwa upande wa majirani walisema tukio hilo lilikuwa la kutisha na si la kawaida kuwahi kutokea imeonyesha watoto wa sasa siyo wa kunyanyaswa hovyo, wakatoa ushauri kuwa kila mwenye mtoto akae na mwanae asimuamini mtu ndiyo sababu ya watoto wengi hasa wa kike kuharibikawa kutokana na kukosa uangalizi.

Monday, February 18, 2013

SILAHA ZATEKETEZWA KWA MOTO.

      
Askari wa Polisi akiangalia zoezi la uteketezaji wa  Silaha haramu uliozinduliwa na Makamu wa Rais Dk Mohammed Ghalib Bilal uliofanyika  Ukonga jijini Dar es Salaam jana.Picha na Venance Nestory  

ZAIDI ya silaha haramu 3,100 zimeteketezwa ili kukabiliana na uhalifu unaokumba nchi za Afrika Mashariki.

Akizungumza kwenye mkakati huo kuangamiza silaha hizo Dar es Salaam jana,  Makamu wa Rais, Dk Mohammed Gharib Bilal  alisema bado  kuna kazi kubwa  kukabiliana  na migogoro eneo hilo kutokana na wimbi la umiliki wa silaha haramu.

Silaha hizo ziliteketezwa kwenye viwanja vya Magereza Ukonga,  huku viongozi mbalimbali wa kitaifa na kimataifa wakihudhuria.

Dk Bilal alisema migogoro mbalimbali na usugu wa matukio ya uhalifu katika jamii,  yanachangiwa  na uwapo wa silaha ndogo na kubwa ambazo zinazomilikiwa kinyume cha sheria.

Alibainisha kuwa  takwimu zinaonyesha kuna sillaha 500,000  ukanda wa nchi za Afrika  Mashariki zinamilikiwa na watu wa aina mbalimbali kinyume cha sheria, jambo ambalo linasababisha kuongezeka kwa matukio tofauti hasa maeneo ya mipakani.

PADRI AUWAWA ZANZIBAR KWA KUPIGWA RISASI KICHWANI.

         
Akina mama wakilia baada ya kifo cha ghafla cha Padri Evarist Mushi kilichotokea jana asubuhi kwa kupigwa risasi muda mfupi kabla ya kuanza misa ya Jumapili kwenye Kanisa Katoliki la Kigango cha Mtoni,  



PADRI wa Kanisa Katoliki Parokia ya Minara Miwili lililoko Mji Mkongwe Zanzibar, Evaristus Mushi ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana jana asubuhi wakati akielekea kanisani kuendesha ibada.
Tukio hilo limetokea majira ya saa moja asubuhi wakati padri huyo akijitayarisha kwenda kuongoza ibada ya Jumapili katika Kanisa la Mtoni nje kidogo na Mji wa Zanzibar.
Hilo ni tukio la pili kutokea kwa padri kupigwa risasi Zanzibar baada ya Desemba 26, mwaka jana Padri Ambros Mkenda wa Kanisa Katoliki, Mjini Zanzibar kupigwa risasi na watu wasiojulikana nje ya nyumba yake saa 1:45 jioni wakati akitokea kanisani.
Akizungumzia tukio la jana, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Said Mwema pamoja na kuthibitisha, alisema ametuma timu ya wapelelezi kwenda Zanzibar kuchunguza kwa undani kuhusu tukio hilo.
“Watu wasiojulikana wamempiga risasi Padri Mushi, na baada ya tukio alipelekwa Hospitali ya Mnazi Mmoja na kufariki dunia. Polisi inaendelea na uchunguzi kuhusu tukio hilo,” alisema IGP Mwema.
Alisema hadi sasa watu watatu wameshakamatwa kuhusiana na tukio hilo na msako mkali unaendelea na kuchunguza tukio zima.
IGP Mwema alisema ametuma timu Zanzibar itakayoongozwa na Manaibu Kamishna wa Polisi wawili ambao ni Samson Kasalla na Peter Kivuyo wakiwa pamoja na Kamanda wa Operesheni wa jeshi hilo, Simon Sirro.
“Tumekuwa tukifuatilia nyendo hizi na hivi sasa tutapambana na wahalifu ipasavyo, vurugu zozote zile lazima tupambane nazo ipasavyo,” alisema Mwema na kuongeza: “Kama kwenye tukio hili kutakuwa na masuala ya kigaidi nayo tutachunguza.”
Alisema watawatafuta kwa udi na uvumba wale wote wanaochochea au kufadhili yanayotokea kwa kuwa wanachokifanya ni uhalifu.
Mwili wa padri huyo sasa umehifadhiwa katika mochwari ya Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja.
Katika Kanisa la Minara Miwili, Mji Mkongwe waumini walikusanyika wakionyesha hali ya kuchanganyikiwa baada ya kupata taarifa za kifo hicho cha ghafla.
 Wakizungumza kwa masikitiko waumini hao wamesema hawakuwa wakijua chochote kilichotokea hadi hapo walipofika katika kanisa kwa ajili ya kufanya ibada.
 “Tumetoka nyumbani tukiwa na matumaini makubwa ya kufanya ibada zetu kwa amani, lakini tulipofika hapa tumepokea taarifa kuwa padri wetu amepigwa risasi, jamani Mungu hiki ni nini, mbona Zanzibar imegeuka kuwa nchi isiyo na amani, vipi tutaishi katika hali kama hii ya kuhofu na wasiwasi...Mungu tusaidie waja wako sisi,” alisema mama mmoja huku akilia kwa majonzi.”
Mashuhuda

Walioshuhudia tukio hilo wanasema kawaida Padri Mushi huwa anakwenda kusalisha katika Kanisa la Mtoni na kwamba jana, baada ya kufika kanisani hapo wakati akitaka kuegesha gari lake walifika watu kwenye gari lake na kumfyatulia risasi na kisha kukimbia kusikojulikana.
Makamu Askofu wa kanisa hilo Zanzibar, John Mfoi alisema kuwa watu waliompiga risasi Padri Mushi walikuwa wapo kwenye pikipiki aina ya Vespa na walikuwa wakimfuatilia kwa nyuma wakati akieleke kanisani.
“Baada ya kufika karibu na kanisa alipigwa risasi na gari kupoteza mwelekeo kisha kwenda kuonga nyumba,”alisema na kuongeza: “Uchunguzi wa hospitali umegundua alipigwa risasi tatu mbili zimetolewa kichwani na nyingine haijulikani iliko.”
Matukio kama hayo ya kihalifu yamekuwa yakitokea mara kwa mara Zanzibar ambapo katika kipindi cha mwezi mmoja watu watatu walipigwa risasi maeneo ya Bububu na Mbweni, lakini hii ni mara ya pili kwa padri kupigwa risasi katika historia ya Zanzibar.

TEC wasikitika
Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC),Severin Niwemugizi alisema tukio hilo linatia mashaka kwa kuwa mauaji hayo yanaonyesha kuwa ni ya kupanga.
“Nimepata taarifa kwamba kuna mwenzetu ameuawa huko, lakini inaonekana ni mauaji ya kupangwa kwa kadiri ya hamasa ambazo zinatolewa na dini fulani, kwani waliwahi kusema hatutaifurahia Pasaka, nadhani ndiyo wanatekeleza hilo,” alisema Niwemugizi.
Alisema tukio hilo ni la kuogopesha na linaonyesha nchi inakoelekea si kuzuri kwa kuwa kikundi fulani kimeachiwa na kinafanya mauaji na kuwatendea maovu wengine lakini viongozi wamekaa kimya.
“Hii ni ishara mbaya kwani Serikali ipo hivyo tunahitaji kauli yao kuhusu haya mambo, kwa kweli nina mashaka na yanayotokea ili yasije yakatufikisha kwenye mauaji ya kimbari yaliyotokea Rwanda,”alisema Niwemugizi.

JK atuma rambirambi
Rais Jakaya Kikwete alisema amepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa ya kuuawa kwa Padri Mushi.
“Nimeligiza Jeshi la Polisi nchini kukusanya nguvu zake zote na maarifa yake yote kuhakikisha kuwa uchunguzi wa kina na wa haraka sana unafanyika ili kubaini mhusika ama wahusika na kuwakamata ili kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria.”


Alisema pia ameagiza polisi washirikiane na vyombo vingine vya usalama nchini na mashirika ya upepelezi ya nchi rafiki katika kufanya uchunguzi wa mauaji hayo.
Amesisitiza Rais Kikwete: “Nataka ukweli wake ujulikane ili kama kuna jambo lolote zaidi liweze kushughulikiwa na kukata mzizi wa fitina.”

Dk Nchimbi asema ni ugaidi
Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Nchimbi alisema kuwa mauaji hayo ni ya kigaidi  hivyo Serikali itachukua hatua kali kuhakikisha waliohusika wanakamatwa.
“Tutahakikisha kuwa Serikali inawakamata waliohusika na kuwatia mbaroni,”alisema Dk Nchimbi.

Mwinyi aonya
Rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi amewaonya viongozi wa dini kuhusiana na matukio ya vurugu yanayoendelea kujitokeza nchini akisema kuwa Tanzania ni sawa na gunia lililokusanya mchanyanyiko wa watu wenye kufuata mikondo ya dini inayotofautiana. Hivyo hakuna dini inayoweza kujigamba ni bora zaidi ya nyingine.
Aliwataka viongozi wa dini kuwakemea waumini wanaojihusisha na mienendo korofi kwa kuwa bila kufanya hivyo taifa linaweza kutumbukia kwenye mgogoro wa kidini na kusababisha upotevu wa hali ya amani na mshikamano.
Rais mstaafu Mwinyi ambaye alikuwa akizungumza kwenye sherehe za Maulidi iliyoadhimishwa jana na waumini wa Madhehebu ya Shia, alisema kuwa Tanzania iko kwenye wakati mgumu ikiandamwa na misukosuko ya aina mbalimbali ikiwemo ile yenye sura za kidini na kisiasa.
Alisema kuwa Tanzania iliyosifikia duniani kwa ustaarabu wake wa amani na mshikamano sasa inaanza kupoteza mwelekeo kwa raia wake kuingia kwenye maisha ya hofu na kushindwa kuaminiana.
“Ngoja niwapeni mfano mmoja hata kama mfano huu utakuwa mbaya kwenu, lakini nataka muelewe maana yangu… Tanzania ni sawa na gunia lililokusanya watu wa aina mbalimbali, wapo wale wenye dini, kuna wale hawana dini na wapo ambao wana dini inayotofautiana na dini nyingine...Hakuna upande unaoweza kujivuna kuwa ni bora kushinda mwenzake,” alisema na kuongeza;
“Ni wajibu wote tuliomo ndani ya gunia hili kushikamana na kuvumiliana kwani tukisema huyu ni bora zaidi ya mwingine, hatutafika mbali.”
Alisema kuwa Watanzania wanapawa kujenga tabia ya kuvumiliana na kutatua tofauti zao kwa njia ya majadiliano bila kujiingiza katika matukio yanayoweza kuharibu amani ya nchi.
“Waswahili walisema, maneno matamu humtoa nyoka pangoni. Hivyo nawatamanieni viongozi wa dini kazaneni kuwahimiza waumini wenu kutojihusisha na mienendo hatarishi kwa amani yetu,” alieleza Mwinyi, ambaye alioongoza Tanzania kuanzia mwaka 1985 hadi 1995.

Sheikh DSM aonya
Akizungumzia tukio la mauaji ya padri huyo, Sheikh Mkuu wa Dar es Salaam, Alhaji Mussa Salum pamoja na kulitaka Jeshi la Polisi kuharakisha uchunguzi wa tukio hilo.
Alisema kuwa hali ya hewa visiwani humo imechafuka na kuonyesha wasiwasi wake kuhusiana na kujitokeza kwa matukio hayo.
Alisema kuna haja kwa mamlaka kutafakari kwa makini na kujiuliza kwa nini matukio hayo yanajitokeza wakati huu ambapo baadhi ya viongozi wa dini wameendelea kushikiliwa kizuizini.
“Kwangu mimi haya ya Zanzibar yanajadilika, pia lazima tujiulize kwa nini matukio haya ya mashambulizi yanajitokeza zaidi wakati huu,” alisema.

Lowassa: Waislamu, Wakristo waungane
Waziri Mkuu aliyejiuzulu,  Edward Lowassa  amewataka Waislamu na Wakristo wote nchini kuungana kwa pamoja kuitetea na kuilinda amani iliyopo kwa vitendo.
Akizungumza katika Harambee ya Kanisa la Moravian Kanda ya Magharibi iliyofanyika katika Wilaya ya Nzega, mkoani Tabora, Lowassa alisema kuwa waumini hao kwa pamoja wanapaswa kuungana na kuwa kitu kimoja katika kuitetea amani iliyopo kwa vitendo.
Aliendelea kusisitiza kwamba kwa sasa kuna baadhi ya Watanzania wanaichezea amani iliyopo kwa sasa hapa nchini na kufanya mauaji ya watumishi wa Mungu.

“Hii ni Tanzania tunayoitaka kwa Waislamu na Wakristo kushirikiana katika ibada kama hii leo hapa kanisani,” alisema Lowassa.
Lowassa aliendelea kusisitiza kwamba Watanzania wanapaswa kuhakikisha kila siku wanamuomba Mungu, ili kuendeleza amani hapa nchini inadumishwa kwa hali na mali.
Alisema kwamba watu wanaomsema vibaya kila kukicha waendelea kufanya hivyo, kwani kwa kufanya hivyo wanaendelea kumuimarisha kiimani na nguvu kubwa ya ushawishi kwa watu wa Mungu ambao ndiyo wamekuwa wakimuunga mkono kila siku katika kazi ya Mungu.
Alirudia kauli yake aliyoitoa mkoani Mbeya hivi karibuni, “Mimi ni tajiri wa watu na siyo tajiri wa fedha kama wanavyosema huko mitaani  na watu wasiokuwa na mapenzi mema na Mungu,”alisema Lowassa.
Katika harambee walikuwapo baadhi ya Waislamu kutoka Mikoa ya Mwanza, Shinyanga na Tabora pamoja na viongozi mbalimbali wa siasa kutoka sehemu mbalimbli hapa nchini.
Askofu Mkuu wa Kanisa la Moravian Kanda ya Magharibi, Issack Nicodemo alisema kuwa Waislamu na Wakristo hapa nchini ni ndugu kutokana na uhusiano uliopo tangu zamani.
Alisema kuwa vitendo vinavyoendelea kufanyika hapa nchini vya mauaji kwa viongozi wa dini ni vya kulaaniwa.

Thursday, February 7, 2013

Zambia: Many dead in bus and lorry crash north of Lusaka

Spectators gather at the scene of a crash some 100km (60 miles) north of Lusaka, the capital of Zambia, on Thursday 

At least 53 people have been killed in a crash involving a bus and lorry in Zambia, police say.
The death toll could rise as rescuers were still trying to get into the bus wreckage hours after the crash, police reportedly said.
The accident occurred about 100km (60 miles) north of the capital Lusaka on a two-lane highway known for heavy traffic.
Poorly maintained and overloaded vehicles are commonplace in Zambia.
Nonetheless, this is said to be one of the worst traffic accidents in the country's history.
According to reports, the bus was operated by the Zambia Postal Service, which provides passenger services on buses which carry post, and was full of people.
'Bus swerved'
Deputy minister for Works and Supply Colonel Panji Kaunda with a Provincial Army representative inspects the scene of the crash on Thursday 
The extent of the damage to the bus was visible as a deputy minister visited the crash site.

It crashed into a lorry - and according to Zambia's information minister Kennedy Sakeni a sports utility vehicle was also involved in the crash, the Associated Press news agency reported.
The wreckage of the bus was so mangled that hours later emergency workers were still trying to get into it to check for victims, police spokeswoman Elizabeth Kanjela was quoted as saying.
There was serious speeding by all the vehicles involved, Harry Kalaba - an official in the vice-president's office - told AFP news agency from the crash site.
A survivor was quoted as saying the bus had been swerving to avoid an oncoming vehicle.
Some 22 dazed or unconscious survivors were being treated in a nearby missionary hospital, AFP said, while more seriously injured casualties had been taken to hospital in Lusaka.
President Michael Sata conveyed his government's "deepest condolences" to families of the victims.
Police are investigating the cause of the crash.
In 2005, 44 schoolchildren were killed when the vehicle they were travelling in crashed in northern Zambia.

BAADHI YA MAGAZETI YA LEO ALKHAMISI TZ 07/02/2013

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
11757 4891428196311 375914601 n 21b72

Translate