tangazo

Wednesday, January 30, 2013

JACK PATRICK NUSURA AUE MTU..

Na Musa Mateja
STAA wa Bongo anayetesa kwenye mitindo, Jacqueline Patrick anakabiliwa na msala wa kumtwanga na chupa nusu kumuua mrembo anayejulikana kwa jina la Hafsa Sasya, Risasi Mchanganyiko linanashuka nayo.
Hafsa Sasya baada ya kujeruhiwa na Jacqueline Patrick.
Habari zilizopenyezwa na chanzo chetu kutoka eneo la tukio zinasema kwamba, ishu ilitokea usiku wa kuamkia Jumamosi ya Januari 26, mwaka huu ndani ya Ukumbi  wa Elements Lounge uliopo Masaki, Dar.
CHANZO KINATIRIRIKA
Huku sharti la kutotajwa jina lake gazetini likisisitizwa na chanzo hicho, kilisema: “Unajua yule dada (Hafsa) anasoma Kurasini na anaishi Kijitonyama, namfahamu vizuri sana. Walipokutana na Jack pale ukumbini palitokea kutokuelewana kidogo.
“Baada ya muda hali ikawa sawa, watu wakajua yamekwisa. Jack akaenda zake chooni, aliporudi alikuwa na chupa na kwenda kumpiga nayo Hafsa. Mabaunsa wakamwondoa Jack ukumbini na kumwingiza Hafsa kwenye gari lake kwa lengo la kumpeleka hospitalini. Kilichoendelea hapo sijui.”
Jacqueline Patrick.
PEKUPEKU ZA RISASI
Mwandishi wetu aliingia mzigoni rasmi na kuanza kuichimba kwa kina habari hiyo ambapo alipata uhakika wa kutokea kwa tukio hilo na Jack kufikishwa katika Kituo cha Polisi Oysterbay ambapo alifunguliwa kesi yenye jalada namba  OB/RB/1678/13  KUJERUHI.
Baada ya kujiridhisha kwa hilo, zoezi lililofuata lilikuwa ni kuwatafuta wawili hao ili waeleze wanachokijua kuhusu tukio hilo. Wa kwanza kupatikana alikuwa ni Jack.
BOFYA HAPA KUMSIKILIZA JACK
“Ni kweli kulitokea ugomvi siku ile...na ni kweli nilihojiwa na Polisi wa Kituo cha Oysterbay, lakini nimetoka kwa dhamana na kesi imekwenda mahakamani.”

Hafsa baada ya kushonwa nyuzi tatu usoni.
HUYU HAPA HAFSA
“Mimi na Jack tulikuwa marafiki lakini nashangaa amenipiga na chupa bila sababu. Nimeshonwa nyuzi tatu. Siku ile alinikuta nimesimama na rafiki yangu mara akanipiga kikumbo kisha akaenda chooni, aliporudi akanikumba tena, nilipomuuliza ikawa kosa; akanipiga na chupa.
“Imeniuma sana maana amenipa jeraha usoni mwangu bila sababu ya msingi, maana sina ugomvi naye. Kwa sababu hili suala lipo mikononi mwa sheria, naamini itachukua mkondo wake.”

Tuesday, January 29, 2013

KUACHIWA KWA LULU: MAMA KANUMBA ALIA ZAIDI YA MASAA MAWILI.

Na Hamida Hassan
HABARI za staa wa sanaa za maigizo nchini, Elizabeth Michael ‘Lulu’, kuachiwa kwa dhamana, zimemkumbusha mbali mama mzazi wa marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa, hivyo kumfanya aangue kilio kwa saa mbili.
Elizabeth Michael ‘Lulu’ akiwa mahakamani jana.
Mama Kanumba, yupo mkoani Kagera kwa sasa, mara alipozipata taarifa za Lulu kuachiwa huru, alichukua picha yamarehemu Kanumba kisha akajikunyata, akakaa sebuleni peke yake na kuanza kuangua kilio.
Takriban saa moja tangu Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, ilipotangaza kumwachia Lulu kwa dhamana, chanzo chetu mkoani Kagera kilituhabarisha: “Mama Kanumba leo amekuwa mnyonge tofauti na siku zote, aliposikia tu Lulu kaachiwa huru, amejiinamia tu, analia sana.”
Baada ya kupata taarifa hizo, mwandishi wetu alimpigia simu Mama Kanumba ambaye alipopokea tu, kilio kilisikika.
Wakati analia, Mama Kanumba alisema: “Siumii Lulu kuachiwa, najua ni mapenzi ya Mungu ila naumia sana kwa sababu mwanangu mpenzi nilishamzika.”

Mama mzazi wa marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa.
Hata hivyo, mazungumzo hayo yalikoma baada ya Mama Kanumba kushindwa kunyamaza, licha ya mwandishi wetu kutumia muda mwingi kumbembeleza aache kulia.
Saa moja na nusu baadaye, Mama Kanumba akiwa amenyamaza, alimpigia simu mwandishi wetu, akieleza kwamba pale alipo ameshikilia picha ya Kanumba ambayo inamkumbusha machungu aliyokua ameanza kuyasahau.
AKAZUNGUMZA MAZITO
Kuhusu kile kinachomuuma zaidi, Mama Kanumba alisema: “Anayeniumiza ni Mama Lulu, sisi wote ni wazazi lakini hata siku moja hajaja kuniona, kunipa pole, japo najua kilichotokea siyo mapenzi ya Lulu.”
KUNA WAMBEA WALICHAFUA HALI YA HEWA
Mama Kanumba alisema: “Kuna watu wamenipigia simu huko Dar es Salaam kwamba leo kutakuwa na sherehe ya nguvu ya kumpongeza Lulu kupata dhamana.”
Je, hilo lina ukweli? Staa wa Filamu, Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’ ambaye amekuwa bega kwa bega kuhakikisha Lulu anapata dhamana, alisema: “Hakuna sherehe, hatuwezi kufanya hivyo, jamii haitatuelewa.”
Mama Lulu naye: “Jamani namshukuru Mungu kwa Lulu kupata dhamana, hakuna sherehe. Mazingira ya kesi yalivyo, haitakuwa vizuri kufanya sherehe, haitakuwa ubinadamu.”
MASHITAKA YA LULU
Lulu anakabiliwa na kesi ya kumuua bila kukusudia, aliyekuwa mcheza filamu maarufu Afrika, Steven Kanumba.

MAITI YA MTOTO MCHANGA YAGEUKA NA KUWA JOGOO.

Stori: Makongoro Oging’
BADO tupo mwanzoni mwa mwaka lakini tukio la maiti ya kichanga kugeuka jogoo ndani ya chumba cha kuhifadhia maiti kwenye Hospitali ya Mwananyamala, jijini Dar es Salaam linaweza kuongoza mengine yote ya ajabu yanayoweza kujiri ndani ya 2013.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, ACP Charles Kenyela.
Mwananyama ni hospitali yenye hadhi ya mkoa kitabibu, ina rekodi za kuwa na matukio ya ajabu, ila hili siyo tu kwamba linaingia miongoni mwa hayo bali pia linaweza kutia fora.
Asubuhi ya Jumatano iliyopita, ilikuwa kizaazaa pale jokofu lililotumika kuhifadhi maiti ya kichanga cha mtoto, kukutwa kuna jogoo.
Mshangao zaidi ni kwamba ndani ya lile jokofu, pembeni ya yule jogoo, kulikuwa na hirizi pamoja na tunguri.
TUKIO LILIKUWA HIVI
Habari kutoka vyanzo vyetu, zimewekwa wazi kuwa Jumanne iliyopita, saa 7 mchana, polisi walipigiwa simu, wakataarifiwa kuhusu maiti ya mtoto iliyokuwa imetelekezwa eneo la Kigogo, Mbuyuni, Dar es Salaam.
Vyanzo vyetu vimebainisha kuwa polisi baada ya kupata taarifa hizo walifika eneo la tukio na kukuta maiti hiyo ya kichanga ikiwa imefunikwa kwa kuzungushiwa sanda.
ETI, KILIKUWA KICHANGA CHA KIKE
Kwa mujibu wa Moses Madilu, mkazi wa Kigogo, aliyedai kushuhudia tukio hilo, polisi walipofika eneo la tukio waliikagua maiti hiyo na kubaini kwamba ni ya kike.
Chanzo chetu kikaeleza kuwa baadhi ya mashuhuda, hususan wanawake, walitokwa na machozi kwa masikitiko kwamba itakuwa mtu alijifungua halafu akakinyonga kichanga hicho kabla ya kukitelekeza eneo hilo.
“Baada ya kujiridhisha kwa kazi yao, polisi waliichukua maiti hiyo ya kichanga, wakaipakia kwenye ‘difenda’, wakaipeleka Hospitali ya Mwananyamala,” kilieleza chanzo chetu.
HOSPITALI YA MWANANYAMALA
Ndani ya hospitali hiyo, mwandishi wetu alielezwa kuwa polisi walipofika, walishusha maiti hiyo na kumkabidhi mganga wa zamu aliyejulikana kwa jina moja la Dk. Liwa.
Muuguzi mmoja wa hospitali hiyo (jina tunalo) alisema: “Dk. Liwa aliwaambia wale polisi wapeleke maiti hiyo mochwari.
“Polisi walifanya hivyo lakini kule mochwari walimkuta msimamizi mkuu, Omar Buyoya aliyekataa kuipokea kwa vile daktari hakuthibitisha kama kile kichanga kilikufa au kilikuwa hai.
“Polisi na Buyoya walivutana kwa muda mrefu, alitokea mhudumu mwingine wa mochwari aliyekuwa akijuana na polisi mmoja aliyebeba ile maiti, alikubali kuupokea mwili huo na kuingiza ndani kwenye jokofu la kuhifadhia maiti.”
Muuguzi huyo aliendelea kusema kuwa siku iliyofuata, Dk. Liwa alifika mochwari na alipofungua jokofu na kufunua sanda, badala ya kukuta maiti ya kichanga, alikuta jogoo, tunguri na hirizi.
“Dk.Liwa alipatwa  na mshangao mkubwa huku jasho likimtoka kutokana na uoga, aliwaita wafanyakazi ambao walijazana hapo  mochwari kushuhudia.
“Baadhi ya wafanyakazi walipigwa na butwaa huku wengine wakicheka hadi kudondoka chini na wakawa wanajiuliza kama kweli polisi wanaweza kupeleka jogoo hospitali au ni mambo ya kishirikina,” alisema muuguzi huyo.
Dk. Liwa na wafanyakazi wenzake waliondoka mochwari na kuacha hilo jogoo katika chumba cha maiti huku wakishindwa la kufanya.
MGANGA MKUU ANENA
Gazeti hili lilimtafuta Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mwananyamala, Dk. Sophinias Ngonyani ambaye alikiri  kuonekana kwa jogoo badala ya maiti ya kichanga.
“Polisi walituletea kifurushi wakiamini kuwa ni maiti ya kitoto kichanga ambapo tulikipokea lakini ilipotazamwa na daktari, tulikuta jogoo, hirizi na tunguri, tuliamua kumchoma moto kwa sababu kile ni chumba cha kuhifadhi maiti siyo cha kuhifadhia mizoga ya kuku, ng’ombe au mbwa,” alisema Dk. Ngonyani.
POLISI WANENA
Naye Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, ACP Charles Kenyela alipoulizwa juu ya sakata hilo alisema kwamba wao kama jeshi la polisi walipigiwa simu na raia mwema kuwa  kuna maiti ya kichanga ambapo askari waliondoka hadi eneo la tukio na kuichukua mpaka Hospitali ya Mwananyamala.
“Polisi waliichukua hadi Hospitali ya Mwananyamala kwa wataalamu na baada ya kuikabidhi waliondoka na kuendelea na shughuli nyingine, nami nashangaa kusikia kwamba madaktari walikuta bonge la jogoo,” alisema Kenyela.
MASWALI MATANO
Je, ni kweli polisi waliikagua maiti na kugundua ni kichanga cha kike?
Kama ndiyo, ilikuwaje kikageuka jogoo?
Kwa nini daktari hakuipima ile maiti, badala yake akaelekeza ipelekwe mochwari?
Je, au polisi walibeba mzoga wa jogoo, wakampakia kwenye difenda wakidhani ni maiti ya kichanga?
Mkweli nani, polisi wanaodai kupeleka maiti ya kichanga, au hospitali wanaosema walipelekewa mzoga wa kuku, tunguri na hirizi?

LULU AREJEA URAIANI KWA DHAMANA.


NA FURAHA OMARY WA GAZETI LA UHURU
“WATU waendelee kuniombea, hii ni dhamana tu, lakini kesi bado, safari ni ndefu. Namshukuru Mungu, yeye ndiye kila kitu.”

Hiyo ni kauli ilitolewa na msanii wa maigizo nchini, Elizabeth Michael ‘Lulu’, baada ya kuachiwa kwa dhamana na Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, katika kesi inayomkabili ya kuua bila kukusudia.

Lulu, ambaye alikuwa anasota rumande kwa takriban miezi minane katika gereza la Segerea, kuanzia Aprili mwaka jana, anashitakiwa kwa kumuua bila kukusudia msanii mwenzake, Steven Kanumba.

Msanii huyo aliachiwa huru kwa dhamana jana na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu wa Kanda hiyo, Francis Kabwe baada ya kutimiza masharti ya dhamana yaliyotolewa juzi na Jaji Zainabu Mruke wa mahakama hiyo.

Akizunguzumza na waandishi wa habari baada ya kutoka nje ya jengo la Mahakama Kuu, Lulu alisema anawashukuru watu wote na kuwaomba waendelee kumuombea kwa kuwa hiyo ni dhamana tu,kesi bado inaendelea na safari ni ndefu.

Sunday, January 27, 2013

WAKAZI WA KIGAMBONI WAVAMIA AFISI YA WIZARA YA ARDHI


WAKAZI wa Kigamboni Dar es salaam, wamelalamikia usiri wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi katika mchakato wa kupata Mamlaka ya Kuendeleza Mji wa Kigamboni (KDA) pamoja na ujenzi wa mji huo.

Malalamiko hayo yamekuja siku moja baada ya Waziri, Profesa Anna Tibaijuka kuanzisha KDA itakayoshughulikia usimamizi wa maendeleo ya ujenzi wa Mji mpya wa Kigamboni na kuufanya ujitegemee kutoka kwenye Manispaa ya Temeke.

KDA imeanzishwa chini ya Sheria ya Wakala wa Serikali ya 1997, ili iweze kuhakikisha mji huo unajengwa na unakuwa bora.

Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti Dar es salaam jana, wananchi hao walisema wana hofu na hatma ya masilahi yao kutokana na mchakato wa ujenzi wa mji huo kufanywa kwa siri bila kushirikishwa katika hatua za awali.

Walisema hawaupingi uamuzi wa Serikali kujenga mji huo, lakini wanapinga kitendo cha serikali kutokufuata taratibu za ushirikishwaji wananchi hao ambao ndiyo wadau muhimu.

Mwenyekiti wa Mtaa wa, Feri Juma Mihambo alisema ujenzi wa mradi huo umekua ukisuasua tangu mwaka 2008,lakini walishtushwa na taarifa za kuanzishwa kwa KDA kutoka kwenye vyombo vya habari kuwa ndiyo chombo kitakachowasimamia.

“Serikali ishuke chini kwa wahusika halafu iwaeleze kwa kina kwa nini mradi umechelewa kwa takriban miaka minne na pia kwa nini imefanya usiri kuanzisha wakala ambaye atashirikiana nao bila wao kujua” alisisitiza Mihambo.

Naye Nassoro Chano alisema KDA isimamie mpango mji pekee na kuwaachia wananchi uhuru wa kukubaliana na wawekezaji katika masuala ya viwanja na mali nyingine.

“KDA ituachie jukumu la kuingia ubia na mwekezaji ili tupate masilahi stahiki na mwekezaji huyo atatakiwa kujenga kwa kufuata mipango na ramani iliyotolewa na wakala,” alisema Chano.

Ngoroka Ngoroka alisema serikali iwafuate wananchi hao na izungumze nao upya kwa kuyasikiliza mawazo yao juu ya kuendeleza mradi huo, lakini sio kwa utaratibu wa kuwafanya wapokeaji wa uamuzi kutoka ngazi za juu.

Titus Lugoe alisema serikali iache tabia ya kukurupuka na kuwalazimisha wananchi kuwa wapokeaji wa taarifa na maamuzi wakati nao ni wadau muhimu wa kufanikisha mipango ya serikali.

“Mwaka 2008 tulitangaziwa tusiendelee na ujenzi wa miradi yetu, lakini baada ya hapo hakuna kilichoendelea mpaka jana(juzi) tulivyosikia kwenye vyombo vya habari kuwa mradi unaendelea”

Mkuu wa kaya ilipo gesi anusurika kutekwa, wananchi wachoma moto gari

MKUU wa Kaya ya Msimbati ambako gesi asilia inachimbwa mkoani Mtwara, Bibi Somoe Mtiti (106) amenusurika ‘kutekwa’ na mtu anayeaminika na wakazi wa eneo hilo kuwa ni mfanyakazi wa Idara ya Usalama wa Taifa baada ya wananchi kuvamia gari lake na kuliteketeza kwa moto jana usiku.
Hivi karibuni Bibi Mtiti aliionya Serikali juu ya mpango wake wa kusafirisha gesi ghafi kwenda Dar es Salaam kwa madai iwapo itapuuza onyo hilo bomba hilo litasafirisha maji badala ya gesi iliyokusudiwa.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mtwara, Maria Nzuki alisema hana taarifa zozote kuhusiana na tukio hilo kwa kuwa mhusika hajakwenda polisi kulalamika.

Kwa mujibu wa wanakijiji hao, mtu huyo ambaye ana asili ya kijiji hicho waliyemtambua (jina linahifadhiwa) aliwasili kijijini hapo jana saa 10 jioni akiwa na gari dogo aina ya Mark II na kwenda nyumbani kwa shangazi yake.

Habari zinadai kuwa saa 2 usiku mshukiwa huyo alidaiwa kwenda nyumbani kwa Bibi Mtiti akiwa na gari pamoja na shangazi yake.
“Unajua yule bibi tunamlinda, sasa ilipoonekana ile gari usiku pale, watu wakaanza kujiuliza linafanya nini…wakaanza kusogea, kadiri muda ulivyokuwa unakwenda ndivyo watu walivyozidi kuongezeka,”alisema Juma Ayoub mkazi wa kijiji hicho.

Asha Hamisi ni mtoto wa pili wa Bibi Mtiti, akihadithia juu ya tukio hilo, alisema yapata saa 2 usiku wakiwa wanakula chakula walipokea wageni wawili ambao baada ya kumaliza kula waliomba kuongea na mkuu huyo wa kaya.

“Alikuja kijana na mama wakaniomba kuongea na bibi…alimuuliza bibi kama ana uwezo wa kwenda Mtwara, bibi akajibu hawezi…wakaniuliza mimi kama naweza kwenda badala yake nikawaambia siwezi…akasema ametumwa na Rais Jakaya Kikwete na Hawa Ghasia...wamjie bibi wakazungumze naye mambo ya gesi,” alisema Hamis.

Aliongeza kuwa “Kama bibi yupo tayari Jumanne ijayo watamfuata kwa gari…mimi nikasema sitaki…nilipochungulia nje nikaona watu wengi wamezunguka.”

Kwa upande wa mtoto mwingine wa bibi huyo alisema,” Kwa kuwa tunamfahamu tulimwambia aondoke mpango aliojia haufai, akawa anabisha, tukaendelea kumsihi..wakati huo watu wanazidi kuongezeka…alipotoka akakosea njia, alipopita hakukuwa na njia…watu walimfuata wakaanza kumrushia mawe…aliacha gari akakimbia…ndipo wananchi walipoliteketeza gari kwa moto,” alisema Manzi Mohamedi Faki mtoto wa tano wa Bibi Mtiti.

Shangazi wa mtuhumiwa amethibitisha kumpokea mwanaye huyo na kumsindikiza kwa Bibi Mtiti na ambako alimwomba mkuu huyo wa kaya akubali kuondoka naye kwenda Dar es Salaam kwa maelezo kuwa ametumwa na viongozi wake wa juu.

“Ni mwanangu mtoto wa kaka yangu, alikuja akaniomba nimepeleke kwa bibi akamsalimie tuliondoka saa 2 usiku…watu walituzingira na hali ilipokuwa mbaya niliondoka na kumwacha mwanangu pale, naye alikimbia na ndipo walipochoma moto gari,” alisema shangazi huyo.
Alifafanua kuwa “Huyu mwanangu anaishi Dar es Salaam, anafanya kazi Usalama wa Taifa…nadhani alirudi jana hiyohiyo Mtwara.”

Mwenyekiti wa Kijiji cha Msimbati, Salum Tostao alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa ofisi yake haikupokea mgeni yeyote kutoka serikalini kwa siku hiyo.
“Ni kweli gari limechomwa lenye namba za usajili T 609 BXG mali ya Mussa Babu…taarifa hii ni kwa mujibu wa nyaraka tulizookota kutoka ndani ya gari hilo,” alisema Tostao.

Selemani Babu alikanusha madai ya yeye kwenda kijijini hapo jana na alisema, “Hapana, hapana labda

MBUNGE WA CUF AWATETEA WANANCHI WA MTWARA KUHUSU GESI.

MBUNGE wa Mkanyageni (CUF) Zanzibar, Habib Mnyaa amesema, atawasilisha maombi ya wakazi wa Mkoa wa Mtwara katika kikao cha kumi cha Bunge kupinga gesi iliyogundulika mkoani humo kusafirishwa kwenda Jijini Dar es Salaam.

Mnyaa akizungumza na wandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam alisema kwa muda sasa kumekuwapo na mjadala kutoka makundi mbalimbali kuhusu sakata hilo huku yakiwa hayajaonyesha ufumbuzi wa mgogoro huo.

Mnyaa ambaye pia ni Kiongozi wa Chama cha Wananchi (Cuf), alisema atatumia ibara ya 34 ya kanuni za Bunge kuwasilisha maombi hayo bungeni ili kupatiwa suluhisho.

Alisema Katibu wa Bunge amemtaka kuandaa maombi hayo kwa maandishi na lugha fasaha kisha aiwasilishe kwa Spika wa Bunge, Anne Makinda.

Mbunge huyo alisema amekwisha mwandikia barua Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah kuhusu adhima hiyo ya kutaka wananchi wa Mtwara kupatiwa majibu kwa ufasaha.

“Madai ya wananchi wa Mtwara yana msingi kwani wanatakiwa kujua fidia kwa athari za kijamii, kiuchumi na kimazingira zinazoweza kujitokeza hasa kwa wananchi wanaoishi katika rasilimali hizo zinazovunwa,” alisema Mnyaa na kuongeza:

“Kitendo cha wananchi hao kuhoji na kutaka kuhakikishiwa ni kwa namna gani watafaidikia na fursa ya rasilimali ya gesi ni cha msingi ikizingatia kuwa mkoa huo ni moja ya mikoa ya pembezoni iliyosahaulika kimaendeleo kwa muda mrefu,” alisema.

Mbunge huyo alisema madai ya wananchi wa Mtwara yasitafsiriwe kwa mtazamo hasi na kinachotakiwa ni kuwaelimisha na kujua watakavyonufaika na rasiliamali hiyo.

Mapema wiki hii Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, alitoa tamko kutaka suluhu ya mgogoro wa gesi unaoendelea baina ya Serikali na wakazi wa mikoa ya Mtwara na Lindi kwa kuzitaka pande hizo kuacha kulumbana na badala yake wajiandae kukaa meza moja na kutafuta mwafaka kwa njia ya amani.

Rais Mkapa alisema anafedheheshwa na mgogoro huo huku akiwataka wananchi na wadau wa maendeleo Mkoa wa Mtwara, kusitisha harakati za maandamano na mihadhara.

“Fujo, vitisho, kupimana nguvu na malumbano siyo masharti ya maendeleo,” alisema Mkapa na kuongeza;

“Nikiwa kama mwana-Mtwara na Raia mwema mpenda nchi, nimefedheheshwa sana na matukio haya ya siku za karibuni Mtwara. Kwa sababu hiyo natoa wito kwa wadau wote wa maendeleo ya Mtwara, kusitisha harakati hizi na maandamano na mihadhara.”
 
Mkapa aliendelea kueleza katika tamko hilo kuwa “Badala yake wajipange kukaa pamoja katika meza moja, kupitia historia,kutathimini mipango, kuchambua kwa kina mikakati ya utekelezaji wake,hatimaye kufikia mwafaka wa ujia wa maendeleo. Liwezekanalo leo lisingoje kesho.”

Chanzo na mwananchi

Friday, January 18, 2013

36 WACHUKUWA FOMU TFF,WAREJESHA 18



Wakati kesho ndiyo mwisho wa kuchukua na kurejesha fomu za kuwania uongozi kwenye uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPL Board) waombaji 36 wameshachukua na 18 tayari wamesharejesha.
Idadi hiyo ni kufikia leo mchana (Januari 17 mwaka huu). Pia Kamati ya Uchaguzi ya TFF inasisitiza kuwa wanaorejesha fomu hizo kwa email wanatakiwa kuzituma kwa Katibu Mkuu wa TFF kwa email ya tfftz@yahoo.comna si kwa email binafsi za wajumbe wa Kamati ya Uchaguzi au maofisa wa TFF.
Waombaji wanne walioongezeka katika orodha ni Blassy Kiondo kwa Kanda ya Katavi na Rukwa, Eliud Mvella (Mbeya na Iringa), Geofrey Nyange (Morogoro na Pwani), na Omari Abdulkadir kwa Kanda ya Dar es Salaam.
Orodha kamili ya waombaji ni Athuman Nyamlani, Jamal Malinzi na Omari Mussa Nkwarulo (urais) wakati waombaji wa umakamu wa rais mpaka sasa ni Michael Wambura, Ramadhan Nassib na Wallace Karia.
Kwa upande wa wajumbe wa Kamati ya Utendaji na kanda zao kwenye mabano ni Salum Chama (Kagera na Geita), Mugisha Galibona, Samuel Nyalla, Titus Osoro na Vedastus Lufano (Mara na Mwanza).
Epaphra Swai na Mbasha Matutu (Shinyanga na Simiyu), Charles Mugondo na Elly Mbise (Arusha na Manyara), Yusuph Kitumbo (Kigoma na Tabora), Ayubu Nyaulingo, Blassy Kiondo, Nazarius Kilungeja na Selemani Kameya (Katavi na Rukwa) na James Mhagama (Njombe na Ruvuma).
Athuman Kambi na Zafarani Damoder (Lindi na Mtwara), Hussein Mwamba na Stewart Masima (Dodoma na Singida), Farid Nahdi, Geofrey Nyange na Twahili Njoki (Morogoro na Pwani), Elias Mwanjala na Eliud Mvella (Iringa na Mbeya), Khalid Mohamed (Kilimanjaro na Tanga) na Muhsin Balhabou, Omari Abdulkadir na Shaffih Dauda (Dar es Salaam).
Kwa upande wa Bodi ya Ligi Kuu (TPL Board) waliochukua fomu mpaka sasa ni wawili tu. Yusuf Manji amechukua fomu ya uenyekiti wakati Said Mohamed amechukua fomu ya kuwania umakamu mwenyekiti.
SUPER WEEK TENA NDANI YA LIGI KUU YA VODACOM
Mzunguko wa pili ya Ligi Kuu ya Vodacom utaanza Januari 26 mwaka huu huku kukiwa na maombi ya televisheni ya SuperSport kuonesha mechi za Super Week kama ilivyokuwa katika mzunguko wa kwanza.
Raundi tano za awali katika ratiba ya mzunguko wa pili zinabaki kama zilivyo wakati nyingine zilizobaki zitatolewa baada ya kuingiza mechi za Super Week.
Wakati huo huo, mzunguko wa pili wa Ligi Daraja la Kwanza unatarajia kuanza Januari 26 mwaka huu. Ratiba ya ligi hiyo na tarehe rasmi ya kuanza itatangazwa baada ya kupitiwa na Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) inayotarajiwa kukutana mwishoni mwa wiki.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

BAADHI YA VICHWA VYA HABARI MAGAZETI YA LEO 18/01/2013 TZ

IMG-20130118-00358 3c85b

IMG-20130118-00360 6853c

IMG-20130118-00362 c1e74
IMG-20130118-00363 64950
IMG-20130118-00364 91725
IMG-20130118-00365 11a3a
IMG-20130118-00366 de3fa

wasanii bongo movies kupelekwa nigeria


 Mkurugenzi wa Mad Mad Entertainment, Yasmin Razak (katikati) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuhusu kampuni yake kuingia mikataba na wasanii wa filamu wa Tanzania watakaokwenda Nigeria na Jmahuri  ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kwa ajili ya kutengeza filamu. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Superior, Issack Kasanga na Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Simon Mwakifamba. 


Msanii wa filamu, Steve Nyerere (kulia) akifafanua jambo wakati wa mkutano hupo.Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Superior, Issack Kasanga na Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Simon Mwakifamba.  

DAR ES SALAAM, Tanzania

KAMPUNI ya Mad Mad Entertainment iliyopo jijini London nchini Uingereza, imeanzisha program maalum ya kupeleka wasanii wa filamu za bongo nje ya nchi kwa lengo la kukuza sanaa hiyo hapa nchini.
 Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Yasmin Razak alisema ameamua kufanya kazi na wasanii  hao ili kuleta mabadiliko na kuwakwamua kiuchumi wasanii wa filamu hapa nchini.


 “Kwa muda mrefu niliokaa London sioni kama sanaa hii ina maendeleo, nikafikiria kitu gani nifanye ili  kukuza tasnia hii, katika mkataba na kampuni msanii atakayetengeneza filamu na wasanii wa nje atalipwa kiasi cha sh 50 milioni pamoja na malipo mengine yatakayokuwepo kwenye mkataba, ikiwa ni pamoja na asilimia fulani kwa kila kazi itakayouzwa hapa nchini.

“Nimekuwa nikifanya kazi hiyo na wasanii wengi kutoka Nigeria wakiwemo kina Omotola, Two Face na wengineo na pia Ghana, Congo na hata Uingereza, hivyo nimeonelea kuwa itakuwa vema Tanzania nao kuingia katika mchakato huo,”alisema Razak.

Razak ambaye amewahi kufanya kazi ya filamu na Fally Ipupa,  alitaja vigezo vya msanii atakayechaguliwa ikiwa ni pamoja na umaarufu,  kuijua lugha ya kiingereza, uwezo wa kuigiza na kuuvaa uhusika wowote pamoja na mavazi.

Naye rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Simon Mwakifamba aliwataka wasanii hao kujipanga katika kuhakikisha wanaingia kwenye ushindani huo na kuwataka wale watakaochaguliwa kujituma na kuonyesha nidhamu ya uhakika.

“Hapa kuna kuinua vipaji, soko la kimataifa na mengineyo, hivyo ni vema kufanya kazi kikamilifu kwa wale watakaochaguliwa na si kujisahau, wanatakiwa wasanii watatu na tupo katika hatua za awali za mchujo,” alisema
Mwakifamba.
Naye muigizaji Issa Musa maarufu kama Cloud, alisema kuwa lugha itakuwa ni tatizo kubwa kwa wasanii walio wengi, hivyo kuitaka kampuni hiyo iangalienamna ya kuweza kuwasaidia wasanii hao.

Thursday, January 17, 2013

RATIBA YA MICHUANO YA MATAIFA AFRICA(AFCON) 2013


Madaraka ya Rais yawagawa vigogo

Waziri Mkuu Mstaafu John Malecela akizungumza na Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba aliokutana nao jana, ili kutoa maoni yake kuhusu Katiba Mpya. Kulia ni Makamu Mwenyekiti Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani na Mjumbe wa Tume Prof. Mwesiga Baregu.Picha ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba 

VIONGOZI waandamizi wastaafu wa Serikali, John Malecela, Frederick Sumaye na Barnabas Samatta wametofautiana kuhusu madaraka ya Rais yanavyostahili kuwa katika Katiba Mpya.
Katika maoni waliyotoa jana mbele ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Mawaziri Wakuu wastaafu, Malecela na Sumaye walitoa misimamo hiyo inayopingana kwa nyakati tofauti jana.

Wakati Malecela akitaka Katiba Mpya isiguse madaraka ya Rais kwa namna yoyote ile, Sumaye amependekeza viongozi anaowateua mkuu huyo wa nchi, wathibitishwe na vyombo vingine.

Msimamo wa Sumaye haukutofautiana sana na ule wa Jaji Mkuu mstaafu, Samatta ambaye amependekeza madaraka ya Rais yaangaliwe upya katika kipengele cha uteuzi wa viongozi wa umma na utaratibu wa kuwapata majaji.

“Napendekeza kwamba Katiba Mpya iangalie upya madaraka ya Rais katika uteuzi wa viongozi wa umma, lakini masuala mengine yanayomhusu Rais katika utendaji kazi wake yabaki kama yalivyo kuwa sasa,” alisema Jaji Samatta.

Akizungumza muda mfupi baada ya kuwasilisha maoni yake kwa Tume ya Katiba, Jaji Samatta alisema anataka Katiba Mpya itazame upya madaraka ya Rais katika uteuzi wa viongozi wa umma ili kuwe na mgawanyo mzuri katika nafasi hizo.

Jaji Samatta alipendekeza pia utaratibu wa kuwapata majaji utazamwe upya na Katiba Mpya iseme kwamba mawaziri hawapaswi kuwa wabunge.

“Kama tunataka maendeleo katika Mhimili wa Mahakama ni vyema Katiba Mpya ikaweka utaratibu mpya wa kuwapata majaji. Napendekeza Katiba Mpya iweke utaratibu wa kuwapata majaji ili kuhakikisha tunaboresha upande wa Mahakama zetu.”
“Utaratibu huo utasaidia kwa kiwango kikubwa kuboresha Mahakama zetu jambo ambalo litakuwa jema kwani zitafanya kazi kwa kiwango cha juu.”

Viongozi wabanwe
Jaji Samatta alisema Katiba Mpya ni vyema ikaunda chombo maalumu kitakachokuwa kinawabana viongozi wa umma ambao hawafanyi kazi zao ipasavyo.
Alisema chombo hicho kama kitatambulika kikatiba, kitasaidia kuondoa matatizo mbalimbali ya utendaji wa viongozi wa umma katika masuala ya maendeleo.

“Kumekuwa na malalamiko mengi ambayo yanawahusisha viongozi wa umma hasa kwa kutowajibika kwa wananchi, sasa ni vyema Katiba Mpya ikaunda chombo kitakachokuwa kinawabana viongozi wasiofanya kazi zao ipasavyo,” alisema.
Pia Jaji Samatta alipendekeza Katiba Mpya ikataze mawaziri kuwa wabunge ili kila mmoja afanye kazi zake ipasavyo.

Sumaye
Sumaye alitaka viongozi wanaoteuliwa na Rais wathibitishwe na vyombo vingine akitolea mfano uteuzi wa majaji na watumishi mbalimbali wa juu katika Serikali... “Rais anaweza kuwateua, lakini Bunge linaweza kushiriki kuwapitisha watu hao.”

Pia alipendekeza nafasi za wakuu wa wilaya ziendelee kuwepo lakini zisiwe za kisiasa.

Malecela
Akizungumzia madaraka ya Rais, Malecela alisema anawashangaa watu wanaotaka Rais apunguziwe madaraka na akapendekeza Katiba Mpya kumpa nguvu ili aendelee na madaraka aliyonayo sasa.

Alisema haoni kama kuna haja ya kumpunguzia Rais madaraka kwani tayari kuna mihimili mingine ya dola.

“Nawashangaa watu wanaotaka Rais apunguziwe madaraka. Mimi naona hakuna haja ya kufanya hivyo kwani tayari kuna mihimili mingine ya dola ambayo inafanya kazi zake kwa kujitegemea,” alisema Malecela na kuongeza:
“Wanaotaka Rais apunguziwe madaraka ni vyema wangetuambia ni madaraka gani hayo wanayotaka apunguziwe.” Alisema Rais ndiye anayewaunganisha wananchi.
Malecela pia amependekeza Katiba Mpya iweke mfumo mzuri wa kuwapata wabunge wanawake kupitia viti maalumu hadi kufikia asilimia 50 pamoja na kuwapo kwa mabunge mawili ili kuboresha utendaji kazi wa Serikali.

Kama alivyopendekeza Spika wa Bunge, Anne Makinda hivi karibuni, Malecela naye alisema ili kuhakikisha Serikali inafanya kazi yake vizuri, ni vyema Katiba Mpya ikaweka mfumo wa kuwa na mabunge mawili.

CUF sasa wamiliki migodi minane ya madini Tanga

Mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF,Professa Ibraim Lipumba 

CHAMA cha Wananchi (CUF) Wilaya ya Handeni, mkoani Tanga kimewatahadharisha wananchi kuepuka kuwaunga mkono watu au viongozi wanaohamahama na kuanzisha vyama vya siasa, kikidai wanataka kujinufaisha binafsi.

“Acheni kuwaunga mkono watu wanaoanzisha vyama vipya, haiwezekani kwa mfano mtu umekaa CUF karibu miaka 20, leo unaanzisha chama kipya eti unahimiza watu wakufuate, haiwezekani,” alisema Katibu wa CUF Wilaya ya Handeni, Masoud Mjaila na kuongeza:
“Kwani hao watu umewachukua ‘msukule’ wakufuate kila unakotaka kwenda… Hapana, wakataeni.”

Mjaila alikuwa akihutubia mkutano wa hadhara wilayani hapa juzi, uliokuwa ukilenga kuweka mambo sawa, baada ya wiki iliyopita Chama cha ADC kukishambulia kwa kukituhumu kuanzisha migodi ya madini wilayani humo isiyokuwa na kibali.

Katika mkutano huo, Mjaila alikiri wana kampuni inayomiliki migodi minane ya madini mbalimbali Kijiji cha Sezakofi, Kata ya Ndolwa.

Alisema wanaimiliki kihalali huku akionyesha vibali, hatua iliyolenga kujaribu kujisafisha, kufuatia kurushiwa tuhuma na Mlezi wa ADC Kanda ya Kaskazini, Hassan Doyo, aliyejiunga na chama hicho baada ya kutimuliwa CUF.

“Wananchi msikubali kuburuzwa, hiki chama chenu cha CUF kina miaka 20 tangu kuanzishwa, hapa Handeni kina miaka 15, lakini mnaona hali ilivyo, ndiyo hivi karibuni sasa na sisi tupo ndani ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa,” alisema Mjaila na kuongeza:
“Sasa hawa ADC wameanza jana, leo wanataka waungwe mkono, hapana! Hawa wanatafuta masilahi yao maana huku CUF walifukuzwa.

“Eti wanasema migodi ile ya madini haina vibali, siyo kweli kwani serikali iko wapi, tumechangia zaidi ya Sh3.5 milioni, kusaidia miradi mbalimbali ya Serikali ya Kijiji cha Sezakofi.”

Alisema wanatambua vijembe hivyo vinatokana na fitina zilizojaa viongozi wa ADC, hawataki CUF wapate maendeleo.
Aliwashauri nao kutumia fursa zilizopo kwa ajili ya kujipatia maendeleo badala ya malumbano majukwaani.

Katika mkutano huo, CUF kilitangaza kutoa msaada wa shuka 20 zenye thamani ya Sh180,000 hospitali ya wilaya hiyo.

Pia, walitoa sabuni zenye thamani ya Sh150,000.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa chama hicho wilayani hapa, Jumaa Magogo, alisema wagonjwa waliolazwa hospitalini hapo wanauziwa uji.

Magogo alisema kitendo hicho siyo cha kiungwana na kwamba, kinafanywa na mawakala waliopewa kazi ya kutoa huduma hiyo na halmashauri ya wilaya.

Mradi wa gesi Kilwa ‘kuzaa’ hospitali ya kisasa ya kimataifa

Ramani ya hospitali hiyo  

WASWAHILI husema, ‘mgeni njooo , mwenyeji apone’.
Usemi huu una maana nyingi, lakini mojawapo ni ile ya kuona kwamba mara nyingi mgeni afikapo, ujio wake huwa zawadi hata kwa wenyeji.
Kwa Watanzania ,wengi wao wanaposafiri kwenda kutembelea jamaa zao ni kawaida yao kubeba zawadi.

Utaratibu huu unaweza kushabihiana na utakaotokea katika Wilaya ya Kilwa Mkoani Lindi ambako imegundulika gesi.
Kampuni ya Statoil kutoka Norway ikishirikiana na Exxon Mobil iligundua gesi katika Visiwa vya Zafaran na Lavan vilivyopo Kitalu 2, Ukanda wa Pwani ya Tanzania, hususan Pwani ya Kilwa.

Mradi huo una gharama kubwa pia utafanywa na wageni ambao wana utalaamu wa miaka mingi katika biashara ya gesi duniani.

Kutokana na ujio wa wageni hao, Watanzania hususan wakiwamo wakazi wa Kilwa, Lindi na Mtwara kwa jumla hawana budi kupata faida za moja kwa moja na zingine zisizo za moja kwa moja. Miongoni mwa faida zisizo za moja kwa moja ni gesi hiyo kutumika kutengeneza umeme utakaopatikana kwa uhakika na kuuzwa kwa wananchi wote.

Hata hivyo, ujio wa mradi huo kwa upande mwingine una faida kwao kutokana na kutoa ajira ambayo itazingatia uwezo.
Je wakazi wa Halmashauri ya Kilwa watapata faida gani ya kudumu kutokana na gesi hiyo?
Hili ndilo swali ambalo Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, Adoh Mapunda anasema walijiuliza baada ya kufika kwa wageni hao.

Mapunda anasema madiwani, watendaji na mkuu wa wilaya walikaa na kutafakari kwa kina juu ya faida ya kudumu itakayoonekana wilayani mwao kutokana na ujio wa mradi wa gesi.
“Sisi tulikataa kauli za kusaidiwa madawati kwenye shule zetu, ama kupewa dawa kwenye hospitali na zahanati zetu

Hii ni kwa sababu tuna uwezo nazo, badala yake tukabuni mradi mkubwa wa kimataifa ambao utakuwa na faida ya kudumu kwa Kilwa na taifa kwa ujumla”, anasema.
Anafafanua kwamba mradi huo ni ujenzi wa hospitali ya kimataifa itakayolingana na ile ya Apollo nchini India ambayo viongozi mbalimbali duniani hukimbilia kwenda kutibiwa.
Hospitali ya aina hiyo itajengwa na mwekezaji na itaendeshwa na taasisi nyingine ya kimataifa huku halmashauri ikiwa na hisa za kupata gawio la kila mwaka kutokana na faida.

‘’Tulizungumza na wawekezaji, Statoil , kwamba watujengee hospitali ya aina hiyo ambayo itakuwa na uwezo wa kutoa tiba kwa viongozi wakiwamo marais wa Afrika na wakuu wa kampuni mbalimbali Afrika zikiwamo kampuni za uwekezaji katika gesi , madini na hata usafirishaji na wafanyabiashara wa nchi mbalimbali,’’ anafafanua.

Mapunda anasema mpango huo unatekelezwa kupitia utaratibu uliopo kwenye mikataba kwa wawekezaji kuhusu uwajibikaji na ushiriki katika masuala ya kijamii, Social Co-operation Responsibility (SCR).

Anasema tayari Statoil imetenga Sh18 bilioni kuanza ujenzi wa hospitali hiyo mjini Kilwa wakati wowote kuanzia mwaka huu. Anafafanua kuwa michoro ya hospitali hiyo ipo tayari na imechorwa kama lilivyokuwa jengo la kifalme yaani Kasri lililojengwa eneo la Kilwa Kisiwani enzi za Sultan wa Kiarabu aliyekuwa akimiliki kisiwa hicho.

‘’Tunatarajia kwamba taasisi ya kimataifa ya Aga Khan Foundation ndiyo itakayoendesha hospitali hii kwa kiwango cha kimataifa . Tulikaa na kuzungumza pande zote tatu, yaani Kilwa, Statoil na Aga Khan Foundation na kukubaliana kuanzisha hospitali hiyo, hivyo tuna imani itaendeshwa kama ile ya Apollo,’’ anasisitiza Mapunda.

Anasema hospitali hiyo itaajiri madaktari mabingwa kutoka ndani na nje ya nchi, itakuwa na wafanyakazi wataalamu , pamoja na wahudumu ambao wengi watatoka Halmashauri ya Kilwa.

Kutokana na hali hiyo, Halmashauri ya Kilwa inatoa wito kwa wakazi wa wilaya hiyo kutoa ushirikiano kwa wawekezaji ili malengo hayo yatimie.

“Hospitali hiyo itaongeza majengo mengi ya kisasa yakiwamo makazi ya wafanyakazi, hivyo ni jukumu la wakazi wa Kilwa kujiandaa kwa kulima mazao mengi na kujenga nyumba za kisasa,’’ anahamasisha

Hadi sasa, Kilwa ina hospitali mbili, vituo vya afya vitano na zahanati 43, anaeleza mkurugenzi huyo.

Unyama wa polisi kwa wanafunzi IFM ulaaniwe


TUNASHINDWA kupata maneno sahihi kuelezea unyama na ukatili wa kutisha uliofanywa na Jeshi la Polisi juzi kwa wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) walipoandamana jijini Dar es Salaam kulishinikiza jeshi hilo kuwapa ulinzi, kutokana na makundi ya wahuni kuhatarisha usalama wa wenzao wanaoishi Kigamboni, wilayani Temeke kwa kuwapora, kuwabaka na hata kuwalawiti.

Picha za magazeti ya jana na juzi ziliwaonyesha polisi waliosheheni silaha za kivita wakifanya unyama huo kwa kuwapiga na kuwajeruhi vibaya wanafunzi waliokwenda katika Kituo cha Polisi cha Kigamboni kulalamikia kitendo cha polisi kutochukua hatua dhidi ya makundi ya wahuni wanaowatesa na kuwadhalilisha wanafunzi hao.

Picha hizo za kuhuzunisha na kughadhabisha zilionyesha pasipo kuacha shaka kwamba Jeshi la Polisi siyo chombo cha kulinda raia na mali zao kama inavyodhaniwa, bali ni mabaki ya jeshi la kikoloni lililorithi utamaduni wa kutesa na kupora haki za wananchi. Katika picha hizo, polisi walionekana wakifanya vitendo vya kikatili kwa wanafunzi hao waliokuwa wakiandamana kwa amani. Baadhi ya picha zilionyesha polisi wakiwatesa wanafunzi wa kike kwa kuwapiga virungu vichwani, huku wanafunzi hao wakilia na kusaga meno.

Picha hizo zilikuwa kumbukumbu tosha ya polisi wa Kikaburu walivyokuwa wakitesa wazalendo huko Afrika ya Kusini kabla nchi hiyo haijapata uhuru. Kosa la wazalendo hao, kama lilivyokuwa kosa la wanafunzi hao wa IFM juzi ni kudai haki zao za kiraia za kukataa maisha ya mateso na udhalilishwaji ili waishi maisha ya utu, heshima na amani. Badala ya polisi kusikiliza hoja zao na kuahidi kuzifanyia kazi mara moja, walitunisha misuli na kuwapa kipigo kama wafanyavyo kwa majambazi na wahalifu sugu.

Inasikitisha kuona kwamba kila mara polisi wanapozima maandamano wanakuwa kama wanyama wasiokuwa na akili timamu. Hawaonyeshi kuchukua tahadhari yoyote au kuonyesha ubinadamu kwa watu hao wanaodai haki zao kwa amani. Hawaonyeshi weledi wa kazi zao, bali wanatumia nguvu na mitulinga na kuvunja haki za binadamu kwa kusababisha mateso na maumivu kwa watu hao.

Madai ya wanafunzi wa IFM yalikuwa sahihi kwa vigezo vyovyote vile. Maandamano yao yalikuwa na lengo la kuwapa moyo na kuwafariji wenzao waliokuwa wakiporwa fedha na mali zao kila kukicha, mbali na kudhalilishwa kwa kubakwa na kulawitiwa, huku polisi wakishindwa kuchukua hatua dhidi ya makundi ya wahuni yaliyokuwa yakifanya vitendo hivyo, hata baada ya kupewa taarifa kuhusu wahalifu hao. Tungetegemea Polisi hao wawafariji wanafunzi waliodhalilishwa badala ya kuwapa kipigo.

Sisi tunalaani kwa nguvu zote unyama huo uliofanywa na polisi.Tunapendekeza hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya jeshi hilo, kwani matukio ya mauaji, mateso na unyanyasaji wa raia wasiokuwa na raia ambayo yamekuwa yakifanywa na polisi katika miezi ya hivi karibuni ni ushahidi tosha kwamba jeshi hilo limekosa mwelekeo na linapaswa lidhibitiwe ili liheshimu sheria na haki za binadamu na kuzingatia dhana ya utawala bora.

Tunawataka viongozi na wanafunzi wa IFM waache woga, wasimame kidete na kupigania haki za wenzao waliotiwa aibu na hofu na magenge hayo ya wahuni huko Kigamboni. Ni matumaini yetu kwamba polisi watatimiza wajibu wao kwa kuyadhibiti magenge hayo na kuyafikisha mbele ya sheria haraka iwezekanavyo.

KAMPUNI YA TIGO YAGOMA KUPUNGUZA GHARAMA ZA SIMU

 


WAKATI Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ikiwasilisha rai ya kupunguza gharama za mwingiliano wa simu , Kampuni ya Tigo imekataa kufanya hivyo kwa madai kuwa itahatarisha uwekezaji wake kwa punguzo la asilimia 69.

Msimamo huo wa Tigo, umekuja baada ya TCRA kukutana na wadau wa mawasiliano jana jijini Dar es salaam, ili kukusanya maoni kuhusu mapendekezo ya kupunguza gharama ya mtandao mmoja kwenda mwingine. Hatua hiyo inalenga katika kuwasaidia wananchi kumudu gharama za mawasiliano ya simu.

Naibu Mkurugenzi wa Utekelezaji wa Kanda wa TCRA, Victor Nkya, alisema punguzo hilo ni la kutoka asilimia 35 hadi asilimia 69 na kwamba litaanza kutumika Machi mosi mwaka huu na kukoma Desemba 31 mwaka 2017 .

Nkya alisema punguzo la gharama ya kupiga mtandao mmoja kwenda mwingine kwa mwaka 2013 litakuwa asilimia 34.92, mwaka 2014 asilimia 32.40, mwaka 2015 asilimia 30.18, mwaka 2016 asilimia 28.57 na mwaka 2017 ni asilimia 26.96.

“Lengo letu ni kupunguza gharama za mwingiliano wa simu, mfano mwananchi ambaye yupo Tigo anapiga kwenye mtandao wa Vodacom hizi gharama atazilipa mwenye kampuni ya Vodacom kuilipa kampuni ya Tigo badala ya kulipa mwananchi kama ilivyo sasa,” alisema.
Alisema maoni yanayotolewa na wadau yatachukuliwa na Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Mawasiliano na kuyafanyia kazi.

Ofisa Mdhibiti wa Kampuni ya Tigo, Levocatus Nkata, alisema punguzo hilo ni kubwa hivyo wawekezaji watashindwa kuendesha kampuni zao.
Alisema Kampuni ya Tigo inatoa huduma zake hadi vijijini na kwamba hatua hiyo itaifanya ishindwe kupeleka na kutoa huduma kwenye maeneo hayo.

Nkata alisema itachukua muda mrefu kurudisha gharama walizotumia kuendeshea kampuni yao kutokana bei ya kuendesha mitambo.

“Sisi hatukubaliani na hayo mapendekezo yaliyoletwa na TCRA, punguzo hilo kwa sisi wawekezaji ni kubwa sana, tunachoomba wasipunguze ibaki kama ilivyo na kwa mwaka 2017 tunaomba ipunguze kufikia asilimia 45 tu, “alisema Nkata.

Kampuni za Airtel, Vodacom , Benson na Dovetel zimekubali punguzo hilo lakini zimeiomba TCRA ipunguze asilimia chache.

Wednesday, January 16, 2013

WANANCHI WAYAKIMBIA MAKAZI YAO MBEYA


IDADI kubwa ya wakazi wa Kijiji cha Karungu, mkoani Mbeya wameyakimbia makazi yao wakihofia kukamatwa na polisi kutokana na tukio la watu wawili kuzikwa wakiwa hai pamoja na maiti ya marehemu Nongwa Hussein katika tukio linalohusishwa na imani za kishirikina.

Ofisa Mtendaji wa Kijiji hicho kilichopo Kata ya Ivuna, Wilaya ya Momba, Credo Martin alisema jana kwamba wananchi wa kijiji hicho walianza kuyakimbia makazi yao Jumapili jioni baada ya polisi kufika kijijini hapo kuwasaka waliohusika na tukio la kuwazika wenzao wakiwa hai.

Waliozikwa hai ni Ernest Molela anayekadiriwa kuwa na umri wa zaidi ya miaka 60 na Bibi Mizinala Nachela ambaye umri wake unakadiriwa kuwa zaidi ya miaka 50, ambao walifanyiwa unyama huo kwa tuhuma kwamba walihusika na kifo cha marehemu Hussein.

Polisi waliofika kijijini Karungu walifukua kaburi hilo na kuwatoa Molela na Nachela wakiwa wamekwishafariki dunia na baada ya miili yao kufanyiwa uchunguzi ilikabidhiwa kwa ndugu na jamaa zao kwa ajili ya maziko yaliyofanyika juzi mchana.

Martin alisema licha ya kwamba hivi sasa hali ni tulivu, idadi kubwa ya wakazi wa kijiji hicho, hasa wanaume, hawapo kwani wamekimbia kukwepa msako wa polisi waliokuwa wakiwawinda watuhumiwa wa tukio la kuwafukia wenzao.

“Ukijaribu kuzunguka ni kama watu hawapo, wengi wao, hasa wanaume wamekimbia na ukienda kwenye nyumba zao unakuta watoto na kinamama tu, kuna habari kwamba wengine wameondoka kabisa na baadhi yao wanarejea usiku sana na kuondoka alfajiri kwenda mafichoni,” alisema Martin na kuongeza:

“Cha kushangaza ni kwamba hata pale kwenye msiba wa Nongwa, hakuna watu wengi wapo kinabibi tu, jambo ambalo siyo kawaida kwa sababu huku kwetu msiba huwa ni kama siku tatu na baada ya matanga watu wa mbali huondoka halafu wale wa karibu huondoka mmoja baada ya mwingine.”

Ofisa Mtendaj huyo wa Kijiji alisema baadhi ya watu walioyakimbia makazi yao walitajwa kushiriki katika uhalifu huo lakini wengine hawakutajwa na kwamba wamekuwa na hofu na taharuki kutokana na tukio hilo kutokuwa la kawaida.

Martin alisema siku ya tukio hilo, kundi la vijana waliokuwa na marungu, fimbo na mawe lilikuwa likizunguka kijijini hapo kuwasaka watu waliowatuhumu kuwa wachawi na kwamba ndiyo waliosababisha kifo cha Hussein.

Alisema kutokana na hali hiyo, baadhi ya watu waliondoka kwenye msiba na wale waliokuwa wametoka vijiji vya jirani waliondoka wakihofia kudhuriwa na vijana hao, hivyo mazishi yalifanywa na ndugu na jamaa wa karibu na kundi hilo pekee.

“Kwa ufupi ni kwamba hata walioshiriki mazishi ni ndugu tu wa karibu maana watu walikimbia kutokana na tafrani hiyo, hakuna ambaye aliweza kuwazuia kufanya kile walichokiamua maana mtu yeyote aliyejaribu kuonyesha kutokukubaliana nao walitishia kumdhuru,” alisema Martin.

Kaimu Ofisa Mtendaji wa Kata ya Ivuna, Joseph Silwimba alisema jana kwa simu kwamba idadi kubwa ya wanaume katika Kijiji cha Karungu wameyakimbia makazi yao wakihofia kukamatwa na polisi.

Vitendo hivyo viliambatana na tukio la kukamatwa na kuwekwa chini ya ulinzi, Mwenyekiti wa Kitongoji, Alfred Kukwe ambaye alifungwa kamba miguuni na mikononi, kulazwa kifudifudi, kisha kumnyang’anya simu yake ya kiganjani ili asiweze kutoa taarifa kokote.

Jana, Silwimba alisema Kukwe alifikwa na mkasa huo alipofika katika eneo la msiba ambako alikwenda kupeleka jeneza la kumzikia Hussein ambalo alikwenda kulitengeneza kwa mafundi waliopo kijiji jirani cha Ivuna.

Kabla ya Molela na Nachela kuzikwa katika kaburi moja na marehemu, Silwimba alikaririwa juzi akisema kwamba kwa nyakati tofauti, walipigwa hadi kuzirai na vijana walioshiriki kuchimba kaburi hilo maalumu kwa ajili ya kumzika Hussein.

Silwimba alisema Hussein alifariki Dunia Jumamosi saa 10 jioni baada ya kuugua kwa muda mrefu, lakini ilionekana kuwa baadhi ya wakazi wa kijiji hicho walihusisha ugonjwa wake wa muda mrefu ambao ulisababisha kifo chake na ushirikina.

Jumapili kati ya saa 5.30 na saa 6 mchana, vijana hao walifanya uharibifu kwa kuchoma moto nyumba ya George Hussein ambaye ni kaka wa marehemu baada ya kumkosa nyumbani hapo, kwani naye alikuwa akituhumiwa kuhusika na kifo cha ndugu yake.

Alisema baada ya kufanya uharibifu huo, walikwenda nyumbani kwa Mzee Molela ambaye alipigwa hadi kuwa katika hali mbaya na waliporejea msibani walimkuta Nachela ambaye pia walimpiga hadi akazirai.

Silwimba alisema Molela na Nachela baada ya kupigwa, walivutwa hadi kwenye eneo la maziko ambako baada ya jeneza la marehemu Hussein kushushwa kaburini nao walitumbukizwa humo kisha kufukiwa wakiwa hai.

Monday, January 14, 2013

BAADHI YA VICHWA VYA HABARI MAGAZETI YA LEO JUMAATATU 14/01/2013 TZ

 2013-01-14 09.21.57 03c9c

2013-01-14 09.21.30 c7268
2013-01-14 09.20.54 2068a
2013-01-14 09.20.32 00ad4
2013-01-14 09.22.43 a8bd6
2013-01-14 09.22.25 64347
2013-01-14 09.25.41 8f245
2013-01-14 09.23.04 e4bcc
000 0002 09f33

000 0001 a3c81

Sakata la gesi Mtwara, Mbatia na wabunge wake hatiani

 
   James Mbatia 

MWENYEKITI wa NCCR Mageuzi, James Mbatia jana alijikuta katika wakati mgumu baada ya kulazimika kufungiwa katika ofisi ya NCCR-Mageuzi wilaya ya Mtwara Mjini kutokana na baadhi wa wananchi walioudhuria mkutano wake wa hadhara uliofanyika uwanja wa Mashujaa, kutaka kumdhuru kwa madai kwamba hawakuridhishwa na hotuba yake.

Mbatia alianza kurushiwa chupa tupu za maji alipokuwa akitoka uwanjani hapo baada ya kukatisha hotuba yake kutokana na baadhi ya wananchi kupinga kauli zake kwa madai hawamuelewi.

Kauli inayodaiwa kumgharimu Mbatia ni ile ya ‘Iwapo gesi itatoka Mtwara’ ndipo wananchi hao walipoanza kupaza sauti wakisema “Hatukuelewi…hatukuelewi” hata hivyo Mbatia aliendelea kuhutubia hali iliyosababisha wananchi hao wapaze sauti zao kwa kuimba nyimbo.

“Haitoki… Hatoki…Haitoki…” sauti za wananchi zilisikika na hata Mbatia alipojaribu kuwatuliza wananchi hao kwa kusema ‘gesi kwanza…. Gesi kwanza” baadhi waliitikia na wengine waliendelea kusema hawamuelewi.

Hali hiyo ilimlazimisha Mbatia kukatisha hotuba yake saa 11.25 jioni na aliondoka uwanjani hapo kwa kutembea kwa miguu hali iliyotoa mwanya kwa wananchi kumrushia chupa tupu za maji. Mwenyekiti huyo akiwa ameambatana na wabunge wa chama hicho, Moses Machali (Kasulu Mjini) na Agripina Buyogela (Kasulu Vijijini) mkoani Kigoma, walielekea kituo cha polisi kilichopi karibu na uwanja huo na baadaye alielekea ofisi za NCCR Mageuzi wilaya.

Alipotafutwa jana kuzungumzia suala hilo, Mbatia hakupatikana kupitia simu zake zote za mkononi hata wabunge Buyogela na Machali pia simu zao zilikuwa zimefungwa.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mtwara, Mary Nzuki alisema hakuwa na taarifa za Mbatia kunusurika kupigwa ila aliahidi kufuatilia suala hilo. “Ninachojua Mbatia yuko hapa kweli na amefanya mkutano wake, baada ya mkutano ule akiwa anatoka eneo la mkutano alikuwa anasindikizwa na wafuasi wake ambao walikuwa wanamshangilia. Sasa kama walipofika huko mbele walimgeuka hilo sijui”, alisema Nzuki.
Pinda afunguka

Wakati huohuo, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amewasihi wakazi wa mikoa ya Kusini kuwa wavumilivu na kuruhusu mradi wa kusafirisha gesi kutoka mikoa hiyo kwenda Dar es Salaam ufanikiwe kwa kuwa una faida kubwa kwao.

Pinda alitaja manufaa hayo kuwa ni pamoja na ajira kwa vijana watakaoshiriki katika ujenzi huo, ujenzi wa viwanda na miundombinu na upanuzi wa Bandari ya Mtwara.

“Nilishangaa kuona wananchi wa Mtwara wanaandamana kupinga ujenzi wa bomba la gesi asilia kutoka huko kwenda Dar es Salaam. Mradi huo ndiyo utakuwa suluhisho la tatizo la umeme nchini, ”alisema Pinda na kuongeza:

“Wananchi wa Mtwara wawe wavumilivu, watanufaika sana na mradi huo. Mradi utajumuisha upanuzi wa Bandari ya Mtwara pamoja na ujenzi wa Viwanda mbalimbali vitakavyosaidia kukuza uchumi wa maeneo yao kwa kutoa ajira na kukuza biashara zao.”

Waziri Mkuu Pinda alitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita, alipokuwa akijibu maswali ya waandishi waliotaka kufahamu hatima ya mgogoro huo.

Alijibu maswali hayo baada ya kuzindua Makao Makuu ya Biashara ya Kampuni ya Vifaa vya Umeme ya Beko Grundig kutoka Uturuki inayofanya kazi zake nchini kwa kushirikiana na mwekezaji mzawa, Modern Holdings East Africa Ltd.
Pinda alisema pamoja na kwamba gesi asilia inayopatikana Mtwara ni mali ya Watanzania wote, wakazi wa mkoa huo hawapaswi kuwa na wasiwasi na mradi huo, kwani utawanufaisha kwa kiasi kikubwa kinyume na wanadhani.

Kauli hiyo ya Waziri Pinda inaungana na ile aliyotolewa na Rais Jakaya Kikwete wakati wa salamu za mwisho wa mwaka jana ambapo alisisitiza kuwa mradi huo utawapa faida nyingi wakazi wa Mtwara na Watanzania wote.

Kauli za viongozi hao zilikuja baada ya wakazi wa Mtwara kuandamana wakipinga gesi asilia kusafirishwa kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam kwa maelezo kwamba kitendo hicho kitawafanya wasifaidike.

Waziri Pinda alisema kukamilika kwa mradi huo wa gesi kutasaidia kutatua tatizo la umeme nchini na kwamba ifikapo 2015 tatizo hilo litageuka historia, hali itakayochochea kasi ya uwekezaji nchini.

Aliongeza kuwa mbali na mradi huo wa gesi asilia, Serikali inaendelea kuboresha miradi mingine ya kuzalisha umeme ukiwamo ule wa makaa ya mawe uliopo Kiwira mkoani Mbeya.

Aliwataka wafanyabiashara wazawa kupanua wigo wa biashara zao kwa kuwekeza nje ya nchi zikiwemo nchi za bara la Ulaya kama Uturuki ili kuongeza ushindani wa biashara za kimataifa.

Naye Balozi wa Uturuki nchini Ali Davutogh alisema ongezeko la wawekezaji kutoka nchini kwake litakuza uhusiano wa kiuchumi baina ya nchi hizo mbili pamoja na kuongeza ajira, teknolojia na kukuza sekta ya viwanda nchini.

AMUUNGUZA SEHEMU ZA SIRI MKE WAKE.

 
MWANAMKE mkazi wa Kijiji cha Matui, wilayani Kiteto, mkoani Manyara ameponea chupuchupu kuuawa baada ya mume wake kumchoma na chuma cha moto sehemu za siri kutokana na wivu wa mapenzi.

Mwanamke huyo alifanyiwa kitendo hicho juzi usiku kwenye kijiji hicho, baada ya mume wake  kumtuhumu kuwa ana uhusiano wa mapenzi na msaidizi wao wa nyumbani.
 

Akizungumza kwenye Hospitali ya Wilaya ya Kiteto juzi, wakati akipatiwa matibabu mwanamke huyo alisema hivi sasa anasikia maumivu makali.

Alisema alipofanyiwa kitendo hicho alipoteza fahamu kwa muda mrefu, kwani alitokwa na damu nyingi na alizinduka baada ya kufikishwa hospitalini hapo iliyopo umbali wa kilomita 32 kutoka nyumbani kwake.  

Aliongeza kuwa kabla ya kufanyiwa kitendo hicho, kila mara mume wake alikuwa anamweleza kuwa amesikia tetesi kuwa ana uhusiano wa mapenzi na msaidizi wa kazi, hivyo atamfanyia kitu ambacho hatakisahau.

“Siku ya tukio hilo alikoka moto akachukua nondo ya kuweka alama kwenye ng’ombe,  akaniambia ingia ndani mke mwenzako anakuita, nilipoingia ndani naye akaingia na kufunga mlango akaniingiza hiyo nondo ya moto,” alisema.

Daktari wa hospitali hiyo, Godfray Mbise alisema mwanamke huyo amepata kilema cha maisha baada ya kufanyiwa kitendo hicho cha kikatili, kwani ameachiwa majeraha sehemu za siri, mapajani na mgongoni.

Hata hivyo, Diwani wa Kata ya Matui, Kidawa Athuman alisikitishwa na kitendo cha Polisi wa Kituo cha Matui kutochukua jambo hilo kwa uzito.

Athuman alisema askari hao wanashindwa kumchukulia hatua mwanaume aliyefanya kitendo hicho, kutokana na nguvu kubwa ya uchumi aliyonayo.

Pia, alisema kijana huyo msaidizi wa kazi ambaye anahisiwa kuwa alikuwa na uhusiano na mwanamke huyo, naye alichomwa moto sehemu ya taya na alitoroshwa katika maboma ya Kimasai akitibiwe ili kuficha jambo hilo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Akili Mpwapwa alisema hajapata taarifa za tukio hilo na kwamba, atazifuatilia ikufahamu hatua zilizochukuliwa baada ya kutokea jambo hilo.
 

“Ndiyo kwanza wewe unanipa habari hizi, ngoja nizifuatilie kisha nitakujulisha kinachoendelea lakini hadi hivi sasa (jana) bado sijapewa taarifa yoyote kuhusiana na kitendo hicho,” alisema KMpwapwa.

Translate