tangazo

Sunday, March 31, 2013

MUHUSIKA WA MAUWAJI YA PADRI MUSHI AKAMATWA ZANZIBAR.

Kamishna wa jeshi la polisi Zanzibar Mussa Ali Mussa
Kamishna wa jeshi la polisi Zanzibar Mussa Ali Mussa

Jeshi la polisi Zanzibar limefanikiwa kumkamata mtu anaedaiwa kuhusika na mauwaji ya Padri wa kanisa Katoliki Evarest Mushi yaliotokea mapema mwaka huu.
Akizungumza na wandishi wa habari kamishna wa jeshi la polisi Zanzibar Mussa Ali Mussa amesema mtuhumiwa huyo Omar Mussa Makame mkaazi wa Mwanakwerekwe ametambuliwa na watu walioshudia tukio hilo lilitokea katika maeneo ya Bububu.
Amesema baada ya kuchora michoro ya sura ya mtu aliehusika na tukio hilo kwa kutumia watu walioshuhudia na kuitoa kwenye vyombo vya ulinzi, wananchi na mitandao ya kijamii mhalifu huyo ametambuliwa.
Kamishna Mussa amesema mwananchi aliesaidia kutambuliwa kwa mtu huyo atazawadiwa shilingi milioni 10 kufuatia jeshi la polisi kuahidi kutowa zawadi ya kiwango hicho cha fedha.
Hata hivyo amesema kwa usalama wa mtu aliesaidia kukamatwa kwa mhalifu huyo na sababu za kiupelelezi tukio la kuimkabidhi fedha hizo litafanyika kwa njia za siri
        Aidha Kamishna Mussa amewataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano wa hali ya juu ili kufanikisha upelelezi wa matukio mengine yaliopita ikiwemo kujeruhiwa kwa viongozi wa kidini.
Amesema jeshi la polisi litaendelea kutunza siri zap watu watakaotoa taarifa hizo.

Saturday, March 30, 2013

RAIS MSTAAFU WA AFRICA KUSINI AFIKISHA SIKU YA TATU HOSPITALI.

Wananchi wamekumbwa na wasiwasi kwani Mandela amekuwa akitibiwa ugonjwa wa mapafu
Rais mstaafu wa Afrika Kusini Nelson Mandela, yuko hospitalini kwa siku ya tatu kwa matibabu ya ugonjwa. Hadi sasa hakuna taarifa zozote kuhusu muda ataokuwa hospitalini.
Siku ya Ijumaa Mandela aliripotiwa kuendelea vyema na matibabu yake lakini hakuna taarifa mpya kuhusu hali yake.

Hapo jana maafisa wa utawala nchini Afrika Kusini walisema kuwa Mandela alikuwa anaendelea vyema na matibabu baada ya kulazwa hospitalini kwa siku ya pili akiwa na maradhi ya kifua.
Taarifa kutoka rais wa nchi hiyo Jacob Zuma zilisema kuwa hali ya Mandela inaendelea kuimarika na kwamba hata aliweza kula vyema kiamsha kinywa chake.
Mapema leo Jacob Zuma, aliwahakikishia wananchi wa Afrika Kusini kuwa rais mstaafu Nelson Mandela anatibiwa ugonjwa wa mapafu ambao umekuwa ukitokea mara kwa mara.
Katika mahojiano na BBC , bwana Zuma alisema kuwa watu hawapaswi kuwa na wasiwasi kwani Mandela anaendelea kupokea matibabu.
Mandela mwenye umri wa miaka 94 alilazwa hospitalini kabla ya Jumatano usiku.
Alikuwa hospitalini kwa siku 18 mnamo mwezi Disemba, akipokea matibabu ya mapafu na kibofu.
Katika taarifa yake iliyotolewa mapema, Zuma alisema kuwa Mandela anaendelea kupokea matibabu.
Rais Zuma hata hivyo hajaelezea alikolazwa Mandela.
Miaka muhimu katika maisha ya Mandela
  • 1918 Alizaliwa mkoa wa Eastern Cape
  • 1943 Ndipo alijiunga na chama cha African National Congress
  • 1956 Alishtakiwa kwa kosa la uhaini , ingawa mahakama ilitupilia mbali mashtaka hayo
  • 1962 Alikamatwa na kushtakiwa kwa kosa la hujuma na kufungwa jela kwa miaka mitano.
  • 1964 Alishtakiwa tena na kufungwa maisha jela
  • 1990 Aliachiliwa huru kutoka jela
  • 1993 Ashinda tuzo ya amani ya Nobel
  • 1994 Alichaguliwa rais wa kwanza mwafrika mweusi nchini Afrika Kusini
  • 1999 Aling'atuka mamlakani kama kiongozi kwa hiari
  • 2004 Astaafu
  • 2005 Atangaza kuwa mwanawe alifariki kutokana na maradhi ya ukimwi
Akiongea na mwandishi wa BBC Lerato Mbele, bwana Zuma alisema kuwa watu wanapaswa kuwa watulivu.
"ndio, nimekuwa nikiwambia watu kukubali kuwa Mandela sio kijana tena na ikiwa atakwenda hospitalini mwara kwa mara kwa ukaguzi wa kiafya, sidhani hilo linapaswa kuwaweka watu wasiwasi. Ningependa kusema kuwa watu hawapaswi kuwa na wasiwasi hata kidogo,'' alisema Zuma
Mandela anasifika na kujulikana kama Madiba jina la utani.
Alipohojiwa kuhusu ikiwa watu wa Afrika Kusini wajiandae kwa lolote , Zuma alijibu kusema kuwa ''ikiwa mzee anafariki, watu husema kuwa ameenda nyumbani.Nadhani hayo ndio baadhi ya mambo ambayo tunapaswa kutafakari.''
Lakini alisisitiza kuwa bwana Mandela ameweza kupokea matibabu vyema.
Bwana Mandela anatazamiwa na wengi kama baba wa taifa kwa kupambana dhidi ya enzi ya ubaguzi wa rangi.
Mandela alifungwa jela miaka 27 lakini aliachiliwa baada ya kuhudumu miaka 18
Ni mara ya nne kwa Mandela kulazwa hospitalini katika muda wa miaka miwili.
Aliugua kifua kikuu mapema miaka ya themanini, alipofungwa jela katika kisiwa cha Robben Island, kwa miaka 18.
Mapafu yake inaarifiwa yaliathirika pakubwa kwa sababu ya kufanya kazi katika machimbo ya mawe alipokuwa anahudumia kifungo chake.
Licha ya kufungwa kwa miaka mingi ,Mandela aliwasamehe maadui wake wa zamani alipokuwa rais na kuwataka wanachi wote wa Afrika kusini licha ya rangi yao, kusameheana.

WACHEZAJI 3 WA DC MOTEMA PEMBE WAFARIKI KWA AJALI YA GARI.



Gari ambayo imepata ajali na kuua wachezaji watatu wa klabu ya DC Motema Pembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo jana Ijumaa, likiwa nyang'anyang'a baada ya kugongana na lori.

KINSHASA, DR Congo
Mlinda mlango Guelor Dibulana na washambuliaji Hugues Muyenge na Mozart Mwanza walikuwa wakirejea nyumbani baada ya ibada ya Ijumaa Kuu kwenye Kanisa la Saint-Dominique jijini hapa, kisha gari walilokuwamo kugongana na lori
WACHEZAJI watatu wa klabu ya soka ya DC Motema Pembe (DCMP) ya hapa wamefariki dunia kwa ajali ya gari iliyotokea jana Ijumaa jijini hapa, mamlaka za kipolisi zimeeleza.
Mlinda mlango wa kimataifa Guelor Dibulana, washambuliaji Hugues Muyenge na Mozart Mwanza walikuwa wakirejea nyumbani baada ya ibada ya Ijumaa Kuu kwenye kanisa la Saint-Dominique jijini hapa, kisha gari walilokuwamo kugongana na lori.
Mchezaji mwenzao aliyetambulika kwa jina moja la Mbindi, ambaye alikuwa dereva wa gari hiyo yu mahututi, pamoja na abiria mwingine mmoja ambaye hakutambulika, lakini wote wana majeraha makubwa na hali zao ni mbaya.
DCMP ilikuwa inajiandaa na pambano la leo Jumapili ya Pasaka dhidi ya AS Vita Club  katika mechi ya tatu ya Linafoot – ligi ya daraja la juu zaidi DR Congo na ilitarajiwa jana Jumamosi mamlaka husika zingebadili ratiba hiyo.
Uongozi wa juu wa klabu hiyo ulikataa kujibu maswali kutoka SuperSports.com, ukidai ilikuwa ni mapema mno kwa wao kutoa maelezo kuhusiana na ajali hiyo pamoja na vifo vya wanandinga wake. Mungu aziweke roho za marehemu mahala pema peponi. Ameen.
SuperSport.com

Translate