tangazo

Saturday, March 30, 2013

WACHEZAJI 3 WA DC MOTEMA PEMBE WAFARIKI KWA AJALI YA GARI.



Gari ambayo imepata ajali na kuua wachezaji watatu wa klabu ya DC Motema Pembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo jana Ijumaa, likiwa nyang'anyang'a baada ya kugongana na lori.

KINSHASA, DR Congo
Mlinda mlango Guelor Dibulana na washambuliaji Hugues Muyenge na Mozart Mwanza walikuwa wakirejea nyumbani baada ya ibada ya Ijumaa Kuu kwenye Kanisa la Saint-Dominique jijini hapa, kisha gari walilokuwamo kugongana na lori
WACHEZAJI watatu wa klabu ya soka ya DC Motema Pembe (DCMP) ya hapa wamefariki dunia kwa ajali ya gari iliyotokea jana Ijumaa jijini hapa, mamlaka za kipolisi zimeeleza.
Mlinda mlango wa kimataifa Guelor Dibulana, washambuliaji Hugues Muyenge na Mozart Mwanza walikuwa wakirejea nyumbani baada ya ibada ya Ijumaa Kuu kwenye kanisa la Saint-Dominique jijini hapa, kisha gari walilokuwamo kugongana na lori.
Mchezaji mwenzao aliyetambulika kwa jina moja la Mbindi, ambaye alikuwa dereva wa gari hiyo yu mahututi, pamoja na abiria mwingine mmoja ambaye hakutambulika, lakini wote wana majeraha makubwa na hali zao ni mbaya.
DCMP ilikuwa inajiandaa na pambano la leo Jumapili ya Pasaka dhidi ya AS Vita Club  katika mechi ya tatu ya Linafoot – ligi ya daraja la juu zaidi DR Congo na ilitarajiwa jana Jumamosi mamlaka husika zingebadili ratiba hiyo.
Uongozi wa juu wa klabu hiyo ulikataa kujibu maswali kutoka SuperSports.com, ukidai ilikuwa ni mapema mno kwa wao kutoa maelezo kuhusiana na ajali hiyo pamoja na vifo vya wanandinga wake. Mungu aziweke roho za marehemu mahala pema peponi. Ameen.
SuperSport.com

No comments:

Translate