tangazo

Friday, November 30, 2012

MIKOPO KWA WANAFUNZI AMBAO NI WATOTO WA VIGOGO YAPIGWA MARUFUKU



             Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Seif Sharif Hamad

BODI ya Mikopo ya Elimu ya Juu Zanzibar, imeagizwa kuacha mara moja upendeleo wa kutoa mikopo kwa watoto wa vigogo kwani kufanya hivyo ni kwenda kinyume na malengo ya kuanzishwa kwa taasisi hiyo.

Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Seif Sharif Hamad alitoa agizo hilo jana alipozungumza na uongozi na watendaji wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Zanzibar Mnazi Mmoja mjini hapa.

Seif alisema yapo malalamiko mengi kutoka kwa wananchi na wazazi, kwamba Bodi hiyo inatoa mikopo kwa watu ambao hawana sifa, wakiwamo watoto wa vigogo.

“Yapo malalamiko mengi ya wananchi na wazazi kuhusu Bodi hii, ikiwamo kutoa mikopo kwa njia ya upendeleo kwa watu ambao hawana sifa na watoto wa wakubwa,” alisema.

Alikumbusha watendaji wa Bodi hiyo, kwamba taasisi hiyo imeanzishwa kusaidia maendeleo ya watoto masikini wasiokuwa na uwezo wa kumudu gharama za masomo.

“Hayo ndiyo malengo ya kuanzishwa kwa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu, kutoa mikopo kwa watoto wa masikini wasiokuwa na uwezo wa kugharimia masomo,” alisisitiza.

Alisema wakifanikiwa kutekeleza malengo hayo kwa kiasi kikubwa, Bodi itatoa mikopo kwa wanafunzi wengi na kuepusha urasimu na kutiwa shinikizo kutoka kwa wakubwa.

Awali Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi hiyo, Iddi Khamis alisema Bodi imezidiwa na maombi na mahitaji ya wanafunzi wa elimu ya juu wanaohitaji mikopo hiyo wakiwamo wenye sifa.

Akifafanua, Iddi alisema kwa sasa vipo vyuo vya elimu ya juu vinne vikiwa na wanafunzi wenye mahitaji ya mikopo kwa ajili ya kujiendeleza zaidi, lakini Bodi haina uwezo huo.

“Tumezidiwa na idadi ya wanafunzi wanaohitaji mikopo ya elimu ya juu sasa…vipo vyuo vikuu vinne vyenye wanafunzi wanaohitaji mikopo,” alisema.

Hata hivyo, Khamis alisema kwa bajeti ya mwaka 2012/13, Bodi imeongezwa bajeti ya fedha kutoka Sh bilioni 4 hadi Sh bilioni 8 ingawa bado hazitoshi.

Alifafanua, kuwa maombi ya mikopo kwa wanafunzi yameongezeka kutoka 800 hadi 1,800 na Bodi imeshindwa kuwapa mikopo wanafunzi hao wa ziada hivi sasa.

Hata hivyo, wanafunzi wanaokosa mikopo kutoka Bodi hiyo bado wana nafasi ya kuomba kupitia Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

POLISI AFUKUZWA KAZI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MTUHUMIWA HUKO MBEYA.






JESHI la Polisi mkoani Mbeya limemfukuza kazi askari wake Enock Daffa (22) kwa tuhuma za kufanya  mapenzi na mtuhumiwa wa kike mwenye umri wa miaka 25 katika Kituo cha Polisi cha Mji mdogo wa Tunduma, Wilaya ya Momba, mkoani hapa. 


Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Athuman Diwani, askari huyo alitenda kosa hilo Novemba 21,2012 na kwamba mtuhumiwa aliyefanya naye mapenzi alikuwa akikabiliwa na kosa la wizi.
 
Kamanda Athumani alisema kuwa mbali ya kufukuzwa kazi askari huyo tayari amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Mbozi ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.

Aidha alisema kuwa hali kama hiyo haitaweza kuvumiliwa na Jeshi la Polisi na kwamba atakayebainika kufanya tukio kama hilo adhabu yake itakuwa ni kufukuzwa kazi.
 
Kamanda huyo alitoa wito kwa askari polisi kufanya kazi kwa kufuata sheria na kanuni za Jeshi la Polisi kama mwongozo unavyowaagiza ili kulinda maadili ya Jeshi la Polisi ambacho ndicho chombo kinachotumika na wananchi katika kuzisimamia sheria.
 
Akizungumzia tukio hilo, baba mzazi wa askari huyo alisema kuwa kitendo alichofaya mtoto wake si cha kiungwana ambacho pia kimetia fedheha familia yake pia kwa jeshi la Polisi ambalo limepewa dhamana ya kutunza usalama wa raia na mali zake.

chanzo na mpekuzi blogspot

WANANCHI WA WILAYA YA GEITA WATAKA MAFISADI WANYONGWE HADI KUFA.


WANANCHI wa Wilaya ya Geita mkoani Geita wamesema ili kurudisha ari ya viongozi kutumikia umma, wale viongozi watakaokumbwa na kashfa za rushwa ama ufisadi wapewe adhabu kali ikiwa ni pamoja na kunyongwa hadi kufa.

Wakitoa maoni yao kwa ajili ya uundwaji wa Katiba Mpya, baadhi ya wakazi hao kwa nyakati tofauti walisema kwamba tatizo la rushwa na ufisadi limekuwa ni jambo la kawaida kiasi cha kuathiri maendeleo ya nchi na hivyo kuitaka Katiba Mpya kubainisha adhabu ya wala rushwa kuwa ni kunyongwa hadi kufa.

Akitoa maoni yake Elisha Ngeleja alieleza kwamba ili kukomesha rushwa nchini, ipo haja ya Katiba ijayo kubainisha kuwa adhabu ya wala rushwa wote watoaji na wapokeaji pale wanapopatikana na hatia, iwe ni kunyongwa.

“Hatua zinazochukuliwa sasa hazijasaidia tatizo linazidi kukua kila siku, rushwa inaongezeka, ili kukomesha katiba inapaswa kutamka bayana kwamba kila anayepatikana na hatia ya kula rushwa anyongwe hadi kufa,” alieleza.

Sylvester Mwanole yeye alipendekeza katiba ijayo inapaswa kubainisha wazi kuwa wanaohujumu mali za umma wafungwe kifungo cha maisha pale wanapopatikana kuwa na hatia.

Alisema tatizo la kuhujumu mali za umma linazidi kuongezeka kila uchao hii ni kutokana na kutokuwa na adhabu kali kwa wanaohujumu na hivyo kubainisha wafungwe kifungo cha maisha.

Naye Mary Mrungu akitoa maoni yake alipendekeza katika Katiba Mpya ufisadi ubainishwe kama kosa kubwa sawa na kosa la kuuwa na adhabu yake iwe kali kwani itasaidia kuwafaanya viongozi waliopewa dhama ya kuongoza nchi kuogopa.

POLISI WAJERUHI KWA MABOMU DAR,RUFIJI.



POLISI wamewajeruhi watu watatu kwa mabomu, mmoja kati yao akiwa katika hali mbaya katika matukio mawili tofauti ya kusambaratisha mikusanyiko iliyotokea Tegeta, Dar es Salaam na Rufiji mkoani Pwani.

Aliyejeruhiwa vibaya ametambuliwa kuwa mkazi wa Tegeta, John Paul ambaye baada ya tukio hilo alipelekwa katika Hospitali ya Mwananyamala na baadaye Muhimbili.
Tukio la Tegeta lilitokea wakati polisi walipokuwa wakiwatawanya wananchi waliokuwa wakipinga operesheni ya kuwaondoa katika hifadhi ya barabara katika eneo hilo saa nne asubuhi baada ya wafanyakazi wa Kampuni ya Udalali ya Mwankinga wakiwa na polisi waliyolikamata gari la mkazi mmoja wa eneo hilo.
Hali hiyo ilizua ubishi na baadaye vurugu baada ya wakazi hao kutaka gari hilo lisichukuliwe na polisi.

Vurugu hizo ziliwafanya polisi kutumia nguvu kuwatawanya wakazi hao, kazi ambayo hata hivyo, haikuwa rahisi kwani nao walikuwa wakijibu kwa kuwarushia mawe na fimbo, hali iliyodumu kwa saa kadhaa na kufanya eneo hilo kugeuka uwanja wa mapambano kusababisha maduka kufungwa na mali kuharibiwa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Chales Kenyela alithibitisha kutokea kwa vurugu hizo na kueleza kuwa, kijana huyo alijeruhiwa shavuni na kitu ambacho bado hakijafahamika na kupelekwa katika Hospitali ya Mwananyamala kwa matibabu.
Kamanda Kenyela alisema kuwa, polisi bado wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo na taarifa zaidi zitatolewa baadaye. Alisema awali, wafanyakazi wa kampuni hiyo wakiwa na polisi, walifika eneo hilo na kuanza operesheni ya kuondoa magari.

“Walipokamata gari la mmoja wa wakazi wa eneo hilo wananchi hao walipinga na kuanza kuwafanyia vurugu polisi ambao walijibu mapigo kwa kupiga mabomu ya machozi na kuwatawanya. Kijana huyo alionekana baadaye akiwa amejeruhiwa na kupelekwa Mwananyamala,” alisema. Katibu wa Afya katika Hospitali ya Mwananyamala, Edwin Bisakala alithibitisha kupokewa kwa majeruhi huyo na kudai kuwa uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa alijeruhiwa kwa bomu.

Bisakala alisema hali ya majeruhi huyo ilikuwa mbaya na uongozi wa hospitali ulilazimika kumpeleka Muhimbili kwa uchunguzi na matibabu zaidi.
Mmoja wa mashuhuda wa vurugu hizo ambaye hakutaka kutaja jina lake alisimulia jinsi eneo hilo lilivyokuwa: “Polisi wanarusha mabomu na wananchi wanawarushia mawe, ilikuwa tafrani kubwa hapa.”

Alisema hali hiyo iliwafanya polisi wajibu kwa kupiga risasi hewani na kufyatua mabomu ya machozi hali iliyozua taharuki na baada ya watu kutawanyika, kijana huyo alionekana akiwa ameanguka chini, huku damu zikimvuja.

Ofisa Habari wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Aminiel Eligaeshi alithibitisha kufikishwa kwa kijana huyo katika hospitali hiyo akimtaja kwa jina la John Massawe. Alisema alikuwa amejeruhiwa vibaya kichwani.

Mabomu 22 Rufiji
Wilayani Rufiji, polisi walitumia mabomu 22 ya machozi kuwatawanya wananchi wa Kijiji cha Mgomba Kati waliozingira jengo la kufua umeme wakipinga hatua ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kuondoa mashine mbili za kufua umeme bila wao kuwa na taarifa na kuzipeleka wilayani Liwale, Mkoa wa Lindi.

Mwandishi wa habari aliyekuwapo eneo la tukio saa nne asubuhi alishuhudia umati mkubwa wa watu wakiwa katika eneo hilo wakipinga kuondolewa kwa mashine hizo.
Wananchi hao walisema licha ya kuwa na umeme unaotumia gesi ya Songosongo, jenereta hizo huwasaidia wakati umeme huo wa gesi unapokosekana huku wakisema hawakushirikishwa katika uhamishwaji huo.

Askari wawili walifika katika eneo la tukio na kuwaamuru wananchi hao kuondoka katika eneo hilo bila mafanikio. Baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya, polisi hao walikimbia huku wananchi wakiwa na mawe wakiwafukuza. Askari mmoja aliyekuwa na bomu la machozi alidandia pikipiki na kukimbia na kumuacha mwenzake ambaye alishambuliwa vibaya kwa mawe.

Askari huyo aliyeachwa aliepuka kipigo baada ya kukimbilia katika nyumba moja ya msamaria mwema na kujificha.

Baadaye polisi wenye silaha waliwasili eneo la tukio na kuanza kufyatua mabomu mfululizo kuwasambaratisha wananchi hao waliokuwa wamelizunguka jengo hilo wakitaka gari ambalo linasadikiwa kuwa lilikodiwa kwa ajili kunyanyua mashine hizo liondoke.
 
Mganga Mkuu wa Kituo cha Afya Ikwiriri, Dk Idi Malinda alisema raia wawili na polisi mmoja aliyetambulika kwa jina la Ali walifikishwa hapo kwa matibabu baada ya vurugu hizo.
 
Aliwataja raia waliofikishwa hapo kuwa ni Seif Baja ambaye alijeruhiwa mkono wa kushoto, Hemedi Juma aliyeumia kichwani na askari Ali ambaye aliumia sehemu mbalimbali za mwili. Wakati hayo yakitokea katika eneo la tukio, wananchi wengine katikati ya Mji wa Ikwiriri walifunga Barabara Kuu ya Kibiti kwenda Lindi kwa zaidi ya saa moja na kusababisha usumbufu mkubwa kwa abiria waliokuwa wanatumia njia hiyo.
 
Hali ilitulia ilipofika saa 8:46 mchana baada ya polisi kuongeza nguvu kukabiliana na wananchi hao. Meneja wa Tanesco Tawi la Ikwiriri, Ladslaus Kalisa alisema mashine hizo mbili zilikuwa zikipelekwa Liwale kwa kuwa Ikwiriri ilipoanza kutumia umeme wa gesi, mashine hizo hazifanyi kazi.

Mkuu wa Wilaya ya Rufiji, Nurdin Babu alilaani tukio hilo akisema Serikali iliamua kuzipeleka mashine hizo Liwale kwa nia njema ya kuwasaidia wananchi wenzao ambao wanakabiliwa na shida ya umeme.Babu aliwataka wananchi wa Ikwiriri kufuata taratibu za kisheria kudai kile wanachoamini akisema Wilaya ya Rufiji kuonekana kila mara kuwa chanzo cha matatizo siyo sifa njema.

Alisema mashine hizo haziendi kuuzwa kama ambavyo wananchi hao wanadai bali zinakwenda Liwale kuwasaidia watanzania kama wa Ikwiriri ambao kwa sasa wanauhakika wa Umeme wa gesi.

Chanzo cha habari Mwananchi.

MMILIKI WA GARI AMBALO LILIPOTEZA MAISHA YA SHARO MILLIONEA AFUFUNGUKA.

MMILIKI wa gari ambalo lilikuwa likiendeshwa na msanii maarufu nchini, Hussein Ramadhan ‘Sharo Milionea’ na kupata nalo ajali iliyosababisha kifo chake huko Muheza, Tanga, Mohammed Ismaili maarufu kwa jina la Mudi Suma, ameibuka na kueleza uhusiano wake na marehemu, huku akisema amekubali hasara.

Akizungumza kwa simu kutoka Muheza jana Suma alisema hana mpango wa kudai fidia au kupeleka malalamiko yoyote kwa ndugu wa marehemu kwa kuwa; “Kilichotokea ni kazi ya Mungu.” “Siwezi kudai hata kidogo hivyo ni vitu vya kupita tu. Marehemu alikuwa ni zaidi ya ndugu yangu, gari ni kitu kidogo sana katika uhusiano tuliokuwa nao,” alisema Suma na kuongeza kwamba hata Marehemu Sharo Milionea naye alikuwa amemwachia mali zake kadhaa ikiwamo gari.

“Siyo gari tu alilokuwa ameniachia. Kuna mikataba yake ya kazi, Bajaji yake na funguo za chumbani kwake. Nasubiri kukabidhi vitu hivyo baada ya kukaa na ndugu zake. Vitu viko kwenye mikono salama,” alisema.

Kuhusu gari lake lililopata ajali, Suma alisema lilikuwa na bima ndogo, lakini anapanga kwenda TRA atakaporejea Dar es Salaam kufuatilia baadhi ya mambo.
“Kabla ya kuondoka bima ile kubwa ilikuwa imekwisha kwa hiyo nikaamua kuikatia bima ndogo. Nitakapofika kesho (leo) Dar es Salaam, nategemea kwenda ofisi za bima kuzungumza nao,” alisema Suma.

Alipoulizwa kama kuna mtu mwingine atakayeathirika kutokana na gari hilo kuharibika katika ajali mbali na yeye, alijibu: “Hakuna tofauti na mimi mwenyewe na familia yangu.”

Kabla ya ajali
Suma alieleza kuwa kabla ya kuanza safiri yake, Sharo Milionea alifika nyumbani kwake mchana na kumweleza kuwa afya yake haikuwa nzuri.

“Kabla ya kuondoka aliniambia kuwa hajielewi elewi na kifua kilikuwa kinambana. Nikamshauri asiondoke peke yake, atafute mtu wa kuondoka naye ambaye atamsaidia kuendesha gari njiani,” alisema Suma na kuongeza:

“Tulianza kuwapigia simu jamaa zetu wanne wa kusafiri naye lakini kila tuliyemwambia hakuwa tayari. Ilikuwa ni changamoto mpaka ilipofika saa 10:45 hivi jioni, akaamua kuondoka peke yake. Wakati anatoa gari getini kwangu, nikamwambia, basi jaribu kuwa mwangalifu sana, maana alikuwa kweli anasumbuliwa na kifua. Tukakubaliana kwamba atakaporudi aende hospitali kucheki afya yake.”

Kuhusu uhusiano wake na marehemu, Suma alisema: “Mimi ni mfanyabiashara na yeye alikuwa msanii, lakini ilitokea tukawa marafiki sana mpaka ikafikia wakati nikaona kuwa ni ndugu yangu. Nilimwamini nikamtambua kama sehemu ya familia.”

Alisema marehemu alikuwa akitumia gari hilo kila alipolihitaji na safari ya kwenda nalo Tanga kwa wazazi wake ilikuwa ni ya tatu.“Siyo mara ya kwanza kuitumia gari lile, nilikuwa nimemwamini sana. Safari ya kwanza alichukua na kusafiri nalo mwenyewe, halafu safari ya pili ikafuata na hii ilikuwa safari ya tatu,” alisema Suma.

Eneo la ajali wakimbia makazi
Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Songa Kibaoni mahala ambako Sharo Milionea alipatia ajali, wamezikimbia nyumba zao baada ya Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Subira Mgalu kutoa siku moja kwa waliopora mali za marehemu huyo kuzisalimisha mara moja.

Mgalu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Muheza alisema jana kwamba usiku wa kuamkia jana, baadhi ya nyumba kijijini hapo zilikuwa tupu baada ya wakazi wake kuzikimbia.

“Baadhi ya nyumba katika Kijiji cha Songa Kibaoni usiku wa kuamkia leo (jana) zilikuwa tupu, wenyewe wamezikimbia baada ya kusikia amri yangu ya kutaka waliopora vitu vya marehemu Sharo Milionea wavisalimishe,” alisema Mgalu.Alisema kukimbia kwao ni ishara kwamba walihusika katika uporaji wa fedha na vitu vya marehemu mara baada ya ajali.

“Tumewaachia ngazi ya ukoo waendeshe mchakato wa kupiga kura za kuwafichua wahusika wa tukio la uporaji wa msanii huyo halafu majina yao watuletee sisi ili tutumie utaalamu wetu kuwanasa waliohusika,” alisema Mgalu.

Mkuu huyo wa Wilaya alisema mbali ya mchakato huo, amri yake ya kufanya msako wa nyumba kwa nyumba iko palepale.

Alisema anataka kuonyesha mfano wa makali ya Serikali kwa waliohusika na uporaji huo ili kuwa fundisho kwa wengine wanaoishi kandokando ya barabara wenye tabia ya kupora mali za wanaopata ajali.

Thursday, November 29, 2012

Rasimu ya katiba Misri licha ya zogo



Purukushani katika medani ya Tahrir wakati wa maandamano dhidi ya rais Mursi


Kiongozi wa baraza linaloandika katiba mpya ya Misri amesema kuwa pindi tu stakabadhi hiyo itakapokamilika ikiwa katika hali rasimu, huenda wananchi wakahitajika kushiriki katika kura ya maamuzi baadaye Alhamisi.

Ikiwa itaidhinishwa na Rais wa Misri Mohamed Mursi, katiba inaelekeza wananchi washiriki katika kura ya maamuzi.

Katika mahojiano na gazeti la Times, Bwana Musri alipa kuwa atayaachilia mbali mamalka mapya aliyojikabidhi katiba mpya itakapoanza kutumika.

Taarifa hii inakuja huku mahakama ya kikatiba ikiashiria kuwa itaamua Jumapili ikiwa itavunja baraza hilo

Idara ya mahakama ya Misri iko katika mvutano na Rais wa nchi hiyo Mohammed Mursi na wafuasi wake wa kiisilamu baada ya bwana Mursi wiki jana kupitisha sheria inayompa mamlaka kupindukia.

Hofu kuhusu rasimu ya katiba

Hatua hiyo ya rais imezua zogo kote nchini humo.
Huku maandamano yanayopinga hatua ya rais yaliendelea kote nchini , maafisa katika baraza hilo walisema kuwa wanakamilisha rasimu ya katiba licha ya bwana Mursi kuliongezea muda ili kukamilisha rasimu hiyo mwezi Februari.

Kulingana na vyombo vya habari vya serikali, kura ilitarajiwa kupigwa siku ya Alhamisi kuhusiana na mada hiyo.

Waandamanaji walipinga hatua ya rais kujilimbikizia mamlaka
Mwandishi wa BBC nchini Misri, Jon Leyne, anasema kuwa kutolewa kwa katiba katika mazingira haya ya zogo, huenda ikawa tisho kubwa kwa usalama.

Kiongozi wa upinzani na aliyekuwa mwenyekiti wa Jumuiya ya kiarabu,Amr Moussa aliambia waandishi wa habari kuwa ni upuzi mtupu, na mojawapo ya hatua ambazo hazipaswi kuchukuliwa kabisa ikizingatiwa hasira ya watu juu ya baraza la kikatiba.

Baraza la kikatiba lina wanachama wengi wa Muslim Brotherhood na wanasiasa wengine wenye msimamo mkali na ambao wanamuunga rais Mursi.

UN YAWASAIDIA MALI JAAPOKUWA KWA TAHADHARI


Waasi wa Tuareg nchini Mali
Katibu Mkuu wa Umoja wa mataifa, Ban Ki-moon ameunga mkono mapendekezo ya Baraza la usalama la umoja wa Mataifa kuidhinisha vikosi vya usalama vya kulinda amani vya AU vipelekwe Mali kukabiliana na wapiganaji wa kiisalamu Kaskazini ya Mali.

Hata hivyo ilikataa kutoa ufadhili wa Umoja wa Matifa katika shughuli hiyo.
Alionya kuwa kuingiliwa kijeshi katika eneo hilo kutasababisha hatari kubwa za kibinadamu na akataka kuwe na mipango ya kutuliza hali hiyo.

Wanadiplomasia wanasema kuwa vikosi hivyo vitatumia nguvu kupita kiasi ilihali vinatakiwa tu kutoa huduma za kusitisha vita kwa njia ya amani.

Hata hivyo bwana Bana hakutoa msaada wa kifedha na ksuema kuwa mataifa ya Afrika yanahitaji maswali kuhusu jeshi hilo litakavyoendesha kazi zake.

Viongozi wa Afrika wamekuwa wakitaka kuungwa mkono na Umoja wa Mataifa ili kuunda jeshi la pamoja na nchi za Afrika Magharibi litakalosaidia jeshi la Mali kupambana na waasi.

Jeshi la Mali lilipoteza udhibiti wa Kaskazini mwa nchi ambalo linashikiliwa tena.

Kuhusu mapendekezo yake kwa baraza la usalama la umoja huo, bwana Ban alisema ataidhinisha wanachama wa muungano wa Afrika kuunda kikosi cha wanajeshi 3,300 ambao watajulikana kaa AFISMA kuweza kushika doria nchini humo kwa mwaka mmoja.

Alisema wataisaidia jeshi la Mali kurejesha hali ya utulivu kaskazini mwa nchi na kupunguza tisho la makundi ya kigaidi kuvamia eneo hilo

Wednesday, November 28, 2012

MAZISHI YA SHAROMILIONAER




 Mwili wa Marehemu Sharo Milionea ukiswaliwa mapema mchana huu kabla ya kupelekwa kwenye nyumba yake ya milele 
 Rafiki mkubwa wa marehemu Sharo Milionea,Mzee Majuto akiwa ameshikwa mkono wakielekea kwenye mazishi mapema mchana huu,Muheza mkoani Tanga.

MAANDALIZI YA MAZISHI YA MAREHEMU SHAROBARO HUKO HANDENI

                                                           Mama Mzazi wa Marehemu
                                                   
                                  Nape akizungumza na wananchi waliofika katika msiba huo.

                                          Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

Maajabu Ya Dunia, Mtoto Amuua Mama Yake Mzazi Kwa Kumpiga Ngumi...!

 Akina mama waombolezaji wakisawazisha kaburi la marehemu Sinjembele Julius(62) aliyeuawa kwa kupigwa na mwanae Ndele Julius(25)


 Baadhi ya waombolezaji wakishuhudia mazishi ya Sinjembele yaliyofanyika Nyumbani kwake katika kitongoji cha Igawilo kata ya Swaya Mbeya


 Kaburi baada ya kuzikwa marehemu

Mkazi wa  Swaya jijini Mbeya Ndugu Ndele  Julius amemuua mama yake mzazi kwa kumpiga mateke na ngumi kisha kutoroka pasipo julikana Novemba 25 mwaka huu.
Tukio hilo limetokea majira ya saa 10 jioni nyumbani kwa mama huyo mara baada ya kutokea kwa ugomvi kati ya mtoto wake na kijana  mwingine hali iliyopelekea mama huyo kuingilia ndipo alipo kutwa na mauti huo.

Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa Polisi  Mkoani humo Ndugu Diwani Athumani amesema kuwa Chanzo cha tukio hilo ni ugomvi uliokuwepo kati ya mtoto wake na kijana  mwenzake kitendo ambacho kilipelekea mama huyo kuingilia ugomvi huo .

Amesema wakati  mama huyo akijaribu kuamulia ugomvu huo mtoto wake alicha kupigana na mwenzake na kuanza kumshambulia mama yake kwa kumpiga ngumi na mateke mwilini.

Amesema mama huyo alifariki muda mchache kutokana na kupigwa sehemu mbalimbali za mwili wake na kusababishiwa majeraha makuibwa yaliyopeleka kupoteza uhai wake.
Awali akizungumzia tukio hilo Mtoto wa Kwanza wa mama huyo Ndugu Razaro Mbwiga amesema kuwa mdogo wake alikuwa na tabia ya kugombana na mama yake marakwamara .
Hata hivyo teyari mwili huo umekwisha chukuliwa hospitali na kuzikwa ambapo katika maziko hayo Chama cha Muungano wa kijamii (Mujata) umewataka vijana kujiepusha na vitendo viovu kama uvutaji bangi na pombe za kienyeji kwani ndio chanzo cha kutokea kwa vurugu nyingi.

  Na E .Madafa ,Picha kwa hisani ya Joachim Nyambo

BAADHI YA PICHA ZA GARI AMBALO MAREHEMU SHAROBARO LILIPOTEZA MAISHA YAKE.


Gari aina ya Toyota Harrier lenye namba za usajili T 478 BVR alilokuwa akiendesha msanii wa filamu na muziki Hussein Ramadhani Mkieti ‘Sharo Millionea’ kutoka jijini Dar es salaam kuelekea Kijijini kwao Lusanga Wilaya ya Muheza  mkoa wa Tanga. Sharo Millionea alikufa papo hapo na mwili wake kuhifadhiwa Hospitali ya Teule Muheza Tanga.
 Baadhi ya watu wakiliangalia gari aina ya Toyota Harrier lenye namba za usajili 
 T 478 BVR alilokuwa akiendesha msanii wa filamu na muziki Hussein Ramadhani Mkieti ‘Sharo Millionea’ kutoka jijini Dar es salaam kuelekea Kijijini kwao Lusanga Wilaya ya Muheza  mkoa wa Tanga. Sharo Millionea alikufa papo hapo na mwili wake kuhifadhiwa Hospitali ya Teule Muheza Tanga.


Mbunge wa Jimbo la Muheza Hebert Mtangi akiwasili nje ya jengo la Chumba cha Kuhifadhia Maiti cha Hospitali ya Teule Muheza kwa ajili ya kushuhudia mwili wa msaniii Sharo Millionea aliyekufa katika ajali ya gari wakati akitoka Dar es Salaam kwenda Lusanga, Muheza mkoani Tanga, ajali hiyo imetokea katika kijiji cha Kijiji cha Songa Kibaoni .
Wakazi wa wilaya ya Muheza na maeneo mengine wakiwa wamefurika nje ya Chumba cha Maiti cha Hospitali Teule Muheza, kusubiri kushuhudia mwili wa Sharo Millionea, aliyefariki kwa ajali ya gari.

Tuesday, November 27, 2012

MWILI WA ALIEKUWA KIONGOZI WA PALESTINA WAFUKULIA



Hayati Yasser Arafat
Mwili wa kiongozi wa zamani wa Palestina, Yasser Arafat, umefukuliwa kutoka kaburi lake liloko ukingo wa Magharibi mjini Rammala ili kuwawezesha kuufanyia uchunguzi kubaini iwapo aliuwawa kwa sumu.

Bwana Arafat alifariki dunia mwaka 2004 nchini Ufaransa baada ya kuugua kwa kipindi kifupi.

Maradhi yaliyopelekea kifo chake hayakubainika. Uamuzi wa kuufukua mwili wa Yasser Arafat katika kaburi lake lililoko ukingo wa Magharibi unafuatia makala ya televisheni iliyodai kupata mabaki ya madini ya kitonoradi aina ya Polonium kwenye nguo zake.

Wapalestina wengi wanashuku kwamba huenda Israel ilihusika katika kifo cha kiongozi huyo. Israel imekuwa ikikanusha shutuma hizo.

Uchunguzi wa mauaji dhidi ya Bwana Arafat umeanzishwa nchini ufaransa kufuatia ombi lililowasilishwa na mjane wake.

BASI LA KAMPUNI YA DAR EXPRESS LATEKETEA KWA MOTO LEO ASUBUHI.

 
Basi la Dar Express kutoka Arusha kwenda Dar linateketea kwa moto eneo la Segera, mkoani Tanga, abiria wote 65 wamenusurika. Picha zote na Tanga Yetu Blog

GARI AMBALO MAREHEMU ALIPATA NALO AJALI.

                                                        MAREHEMU ENZI ZA UHAI WAKE
        GALI AMBALO MAREHEMU SHAROBARO AMEPATA AJALI NA KUPOTEZA MAISHA
MWILI WAMAREHEMU SHAROBARO

WAFAHAMU MABILIONEAR WATANO NCHINI TANZANIA

 WAFANYABIASHARA watano, Said Bakhressa Gulam Dewji, Rostam Aziz, Reginald Mengi na Ali Mufuruki, wametajwa na Jarida la Ventures Africa linalozungumzia masuala mbalimbali ya uchumi wa Afrika kuwa ndiyo matajiri zaidi nchini.
Anayeongoza katika orodha hiyo ni Bakhressa anayemiliki mali na fedha zenye thamani ya Dola za Marekani 620 milioni sawa na Sh992 bilioni (Dola moja Sh1,600) akifuatiwa na Dewji ambaye utajiri wake ni Dola 560 milioni (Sh896 bilioni). Wengine na kiasi cha mali na fedha wanazomiliki kwenye mabano ni Rostam (Sh672 bilioni- Dola 420 milioni) Mengi (Sh448bilioni- Dola 280 milioni) na Mufuruki (Sh176 bilioni - Dola 110 milioni).

Matajiri hao wamepatikana baada ya kuangalia nafasi zao kifedha, ufanisi wa kampuni zao katika soko la hisa, mfumo wa wanahisa katika soko la hisa na mtiririko mzima wa fedha katika akaunti zao kwenye benki mbalimbali. Jarida hilo linalotoka mara moja kwa mwezi kutoka Afrika Magharibi, limesema matajiri hao wa Tanzania ni kati ya Waafrika wenye utajiri ambao ni mabilionea 4,800 kutoka mataifa 17.Asilimia kubwa ya watu 1,523 ni mamilionea na wamo katika ripoti ya watu matajiri Afrika.Jarida hilo linataja jinsi matajiri hao walivyokuwa wajasiriamali wadogo kabla ya kuibuka na kuwa mabilionea.

REST IN PEACE SHAROMILIONAER



MAREHEMU SHAROBARO ENZI ZA UHAI WAKE


Msanii maarufu wa filamu na Vichekesho nchini almaarufu kama Sharo Millionea amefariki Dunia Kutokana na Ajali ya Gari  alilokuwa akiendesha aina ya Harrier eneo la Muheza Mkoani Tanga.

Kwa mujibu wa mitandao mbalimbali nchini inasema Kamanda wa Polisi mkoani Tanga Constatine Masawe amekiri kutokea kwa msiba wa Sharobaro, baada ya kupata ajali majira ya saa 2 usiku katika kijiji cha Lusanga, Muheza ambapo pia ndio nyumbani kwao.

Mwili wa Marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya mkoa wa Tanga.
Msanii huyo maarufu ambaye amefanya tangazo la mtandao wa simu za Mkononi wa Airtel pamoja na Tangazo la Kinywaji cha Azam Cola akishirikiana na mwenzake King Majuto  ambayo yamekuwa kivutio kwa watoto na wakubwa kutoka na staili ya kuweka mdomo pembeni akionyesha jinsi gani mashabaro walivyo.

MGAGANI HABARI NA MATUKIO: Iko pamoja na Familia ya marehemu sanjari na Watanzania wote  kwa ujumla katika kuomboleza msiba huu mkubwa wa mpendwa wetu Sharo Millionea.
Mungu ailaze roho ya Marehemu Mahali pema peponi Amen.
 

MUAFAKA KATI YA TANZANIA NA MALAWI BADO UNAWEZEKANA.


Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete wakipeana mikono na Rais wa Malawi Joyce Banda

Rais Jakaya Kikwete amerudisha matumaini yaliyokuwa yamepotea baada ya kusema kwamba siyo kweli kwamba mazungumzo kati ya Malawi na Tanzania yameshindikana. Rais alisema mgogoro huo wa mpaka katika Ziwa Nyasa hautapelekwa katika jopo la viongozi wastaafu wanaoshughulikia migogoro ya nchi mbalimbali barani Afrika kwa usuluhishi.

Taarifa za awali zilizokuwa zimechapishwa na kutangazwa katika vyombo vya habari nchini zilisema mgogoro huo ungepelekwa kwa viongozi hao wastaafu baada ya nchi hizo kudaiwa kushindwa kuafikiana katika mazungumzo yaliyomalizika jijini Dar es Salaam wiki mbili zilizopita na kuwakutanisha mawaziri wa mambo ya nchi za nje wa nchi hizo mbili ambao walifuatana na maafisa wa juu wa serikali hizo.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Bernard Membe alikaririwa na vyombo hivyo vya habari akidaiwa kusema kwamba pande zote mbili zilikuwa na matumaini kwamba viongozi hao wastaafu wangesaidia kumaliza tatizo hilo. Hata hivyo, Membe alikuwa amewaeleza waandishi wa habari kuwa, Ziwa Nyasa ni urithi wa nchi tatu za Tanzania, Malawi na Msumbiji na kwamba siyo sahihi kwa upande wowote kati ya nchi hizo kudai unamiliki sehemu kubwa ya ziwa hilo.

Tumetiwa moyo na kauli ya Rais Kikwete kwamba mgogoro huo bado unazungumzika na kwamba nchi hizo mbili bado zinao uwezo wa kumaliza tatizo hilo pasipo kuhitaji wasuluhishi kutoka nje. Hata hivyo, tungependa kutoa angalizo kwa Serikali yetu kwamba mgogoro huo wa mpaka kati yetu na Malawi sasa umeingia katika hatua nyeti na muhimu, hivyo kauli zote zinazohusu mgogoro huo lazima zitolewe kwa tahadhari kubwa ili kuepuka kuupa upande wa pili kisingizio cha kujitoa katika usuluhishi huo.

Kama tulivyoshuhudia mwenendo wa mgogoro huo huko nyuma, baadhi ya kauli za viongozi wetu hakika zilionekana kuchochea kuvunjika kwa mazungumzo hayo kwa sababu upande wa pili ulihisi Tanzania haikuwa na dhamira ya kupata mwafaka wa mgogoro huo.

Tunachotaka kusema hapa ni kuwa, pamoja na ukweli kwamba Serikali ina kila sababu za kupinga hatua ya Malawi kudai kwamba eneo lote la Ziwa Nyasa liko katika himaya yake, Serikali yetu hiyo iache kutumia vyombo vya habari kuelekeza lawama upande wa pili. Kama alivyosema Rais Kikwete, Serikali lazima ithamini vikao vya usuluhishi.

Pamoja na kauli hiyo ya Rais, tungependa kushauri kwamba Serikali itafanya vyema kwa kutambua kuwa, huu sasa ni wakati wa kutumia mbinu za kidiplomasia kuzishawishi nchi marafiki na jumuiya ya kimataifa kwa jumla kwamba mpaka kati ya nchi hizo mbili uko katikati ya ziwa hilo. Tunasema hivyo kwa kuwa, Tanzania iko katika nafasi nzuri ya kuungwa mkono na jumuiya ya kimataifa katika mgogoro huo, kutokana na ukweli kwamba tangu uhuru imekuwa na sera ambazo siyo tu zimeifanya iwe kisima cha amani na kimbilio la wanyonge duniani kote, bali pia imekuwa moja ya nchi chache zinazoendelea ambayo imekoga nyoyo za jumuiya ya kimataifa kama mfano wa kuigwa.

Tunapendekeza pia kuwa, Serikali ibuni mkakati wa kidiplomasia kwa kuwatumia mabalozi wake na wasomi waliobobea kupeleka hoja zake kwa nchi na jumuiya mbalimbali zenye ushawishi, lengo likiwa ni kutaka msimamo wetu uiridhishe dunia kwamba hakika mpaka wetu na Malawi uko katikati ya ziwa hilo.

Sisi tunadhani kwamba Serikali haijachelewa kufanya hivyo. Jambo muhimu ni kwa viongozi wetu kutambua kuwa, katika wakati tuliomo mchakato wa usuluhishi na upatanishi wa migogoro una taratibu zake na kwamba siasa za diplomasia ya kimataifa haziendeshwi kwa fujo, kelele wala ubabe, bali kwa ushawishi na mashauriano miongoni mwa pande zote husika.

Ni matumaini yetu kwamba kupatikana kwa mafuta na gesi katika ziwa hilo hakutazifanya nchi zetu hizi majirani kutangaza uadui. Kauli ya Rais sasa inatupa matumaini mapya kwamba mgogoro huu utamalizika kwa njia ya maridhiano.

Monday, November 26, 2012

Dereva anayeugua saratani kwa kubebeshwa Uranium bila kufahamu


NOVEMBA 6, 2011, siku mbili kabla ya uchaguzi wa Urais nchini Kongo ni siku ambayo Shabani Ally hatoweza kuisahau.
Kama ilivyo ada ya shughuli zake za udereva, Shabani alikwenda nchini Kongo, mjini Lubumbashi kupeleka mzigo. Alipofika huko alitakiwa kupakia mzigo mwingine wa kurudi nao Dar es Salaam.
Walipofika sehemu ya ukaguzi katika eneo la Kisanga, jimbo la Katanga, gari lake lilikamatwa  na baada ya mzigo kuchunguzwa ilibainika kuwa gari limebeba madini yenye mionzi mikali.
Gari hilo, lenye namba za usajili T506BFK, namba ya trela T161ASM na  conteina namba CRXU933671/4 lilikamatwa na kupelekwa katika kituo cha ukaguzi wa madini nje kidogo ya mji wa Lubumbashi.
Shabani  Mkazi wa wilaya ya Temeke, mtaa wa Sandali anasema baada ya wataalamu wa madini kulifanyia uchunguzi gari hilo, walibaini kuwa limebeba madini ya Uranium ambayo yanatajwa kuwa yana mionzi mikali.
Anaitaja kampuni ya Somika ya Kongo kuwa ndiyo iliyoupakia mzigo huo kuuleta Tanzania, ambapo badaye ungesafirishwa na kupelekwa China kwa kutumia meli.
“Nilikuwa nikisaidia kuupanga mzigo ule katika conteina bila kujua ni nini ninachopakia. Kwani karatasi ya maelezo ilionyesha kuwa ninapakia mzigo wa madini ya Ndandash, kumbe hayakuwa madini ya Ndandash pekee bali yalichanganywa na Uranium,” anasema Shabani
 Ilibainika kuwa kampuni ya Somika ilitoa zabuni ya mzigo wa tani 26 na kumbe kati ya tani hizo, 22 zilikuwa ni madini ya uranium na nne tu, ndizo zilikuwa za madini ya Ndandash.
Anasema  magari madogo ya kupakia mizigo ‘focal  lift’ yalikuwa yakiingiza mzigo ndani ya conteina na yeye akisaidia kuipanga hivyo alikuwa akiyashika na kuyakanyaga kabisa madini hayo yenye asili ya mchangamchanga.
Kwa kuwa uchaguzi nchini Kongo ulikuwa katika kilele, Shabani  baada ya kukamatwa alitakiwa kusubiri hadi matokeo yatangazwe ndipo apewe kibali cha kuendelea na safari.
“Ilibidi kampuni ya madini iturudishe hadi katika kampuni ya Somika. Tulipakua mzigo wa madini yote na tukapewa mzigo mwingine ili turudi nao Tanzania,” anasema Shabani
Shabani anasema  akiwa njiani kurudi Tanzania alianza kusikia maumivu makali ya mguu wa kushoto, hata hivyo, aliyapuuzia akijua ni maumivu ya kawaida.
Alipofika Tanzania aliendelea na shughuli zake za udereva na safari hii alipangiwa kwenda Lusaka, Zambia.
“Nikiwa njiani kuelekea Lusaka, kabla hata ya kufika Tunduma nilianza kuumwa. Mguu uliniuma mno na ikabidi niwapigie simu ofisini ili waniletee dereva mwingine,” anasema
 Ilibidi Shabani arudi Dar es Salaam ambapo ofisi yake ilimpa fedha za matibabu na kuanza kufanyiwa uchunguzi.
Anasimulia na kusema  alikutana na Dk Waane katika hospitali ya Burhani, ambaye baada ya kumpima alimshauri ahamie Muhimbili kwa matibabu zaidi kwani tatizo lake linaonekana kuwa kubwa.
“Ilibidi niusikilize ushauri wa Dk Waane,nilikwenda Muhimbili, vipimo vikachukuliwa na majibu yalipotoka yalionyesha kuwa  chembe hai nyeupe za damu zimeongezeka katika kiwango kisicho cha kawaida,” anasema
Cheti cha Shabani kinaonyesha kuwa  chembe hai nyeupe za damu zimeongezeka na kufikia 101 na hata alipokwenda kupima baada ya wiki moja zilionekana kupanda na kufikia 193.
Balaa halikukomea hapo, mapema mwezi Aprili, Shabani alikwenda hospitali baada ya kusikia maumivu makali ya tumbo.
Alipofanyiwa uchunguzi aliambiwa kuwa bandama yake imeongezeka ukubwa kwa kitaalamu  alikuwa amepata maradhi ya ‘splenomegally.’
Mwajiri wake
Mwajiri wa Shabani, aliyefahamika kwa jina la Frank alipopigiwa simu alikataa kuzungumza lolote akidai kuwa amekwishazungumza na shabani na kuyasuluhisha
Shabani, anadai kuwa  Ruvu Transport Limited ilikuwa ikimsaidia kwa fedha za matibabu.
Hata hivyo kwa maelezo ya Shabani, kasi ya huduma hiyo iliendelea kupungua siku hadi siku  na siku moja walimwita na kumtaka asaini barua ya kuacha kazi.
“Waliniita na kuniambia kuwa nitie saini barua ya kuacha kazi na kunipa mshahara wa miezi minne jambo ambalo mimi sikuliafiki. Sikuliafiki kwa sababu  hayo hayakuwa makubaliano yetu,”anasema
Katika mgogoro huo Shabani anasema alikumbana na kauli za kukatisha tamaa kutoka kwa mwajiri wake ambazo zilionyesha kuwa ‘wamemchoka’
“ Wakati mwingine walisema mimi ni mzigo, napenda kubebwa na maneno mengine mengi,’ anasema
Anasema  aliwaeleza kuwa amepata madhara hayo akiwa kazini hivyo anahitaji msaada wao lakini hawakuwa tayari kumsaidia.
Aidha shabani anadai kuwa waajiri wake wamekuwa wakitafuta visingizio kadha wa kadha ili kuipindisha kesi yao.
“Ninachotaka kwao ni huduma za matibabu kwa sababu hata wakinipa mshahara wa miezi minne niliyofanya kazi, sitaweza kufanya kazi sehemu nyingine  kwa sababu tayari ni mgonjwa,” anasema
Shabani  ambaye ana mke na watoto sita anasema amejaribu kutafuta msaada  kutoka kwa mashirika na taasisi  kama Kituo cha Haki za Binadamu(LHRC) na Baraza la Usuluhishi(CMA)
Si hivyo tu, bali pango la nyumba limekwisha na ameshavumiliwa na mwenye nyumba kwa miezi mitatu sasa.
Anasema mwajiri wake alimwambia kuwa  anatakiwa kuchangia shilingi elfu 50  kwa miezi kumi aliyofanya kazi lakini hakukuwa na mchango wowote katika mfuko wake.
“Kilichonishtua ni kuwa nilipokwenda kuangalia mafao yangu NSSF nilikuta hakuna mchango wangu hata mmoja,” anasema
Aidha Shabani analalamika kuwa  hata viongozi wa serikali za mitaa wanaonekana kupewa rushwa ili suala  lake lisitatuliwe.
Alipofanyiwa uchunguzi aliambiwa kuwa bandama yake imeongezeka ukubwa kwa kitaalamu  alikuwa amepata maradhi ya ‘splenomegally.’
Mwajiri wake
Mwajiri wa Shabani, aliyefahamika kwa jina la Frank alipopigiwa simu alikataa kuzungumza lolote akidai kuwa amekwishazungumza na shabani na kuyasuluhisha
Shabani, anadai kuwa  Ruvu Transport Limited ilikuwa ikimsaidia kwa fedha za matibabu.
Hata hivyo kwa maelezo ya Shabani, kasi ya huduma hiyo iliendelea kupungua siku hadi siku  na siku moja walimwita na kumtaka asaini barua ya kuacha kazi.
“Waliniita na kuniambia kuwa nitie saini barua ya kuacha kazi na kunipa mshahara wa miezi minne jambo ambalo mimi sikuliafiki. Sikuliafiki kwa sababu  hayo hayakuwa makubaliano yetu,”anasema
Katika mgogoro huo Shabani anasema alikumbana na kauli za kukatisha tamaa kutoka kwa mwajiri wake ambazo zilionyesha kuwa ‘wamemchoka’
“ Wakati mwingine walisema mimi ni mzigo, napenda kubebwa na maneno mengine mengi,’ anasema
Anasema  aliwaeleza kuwa amepata madhara hayo akiwa kazini hivyo anahitaji msaada wao lakini hawakuwa tayari kumsaidia.
Aidha shabani anadai kuwa waajiri wake wamekuwa wakitafuta visingizio kadha wa kadha ili kuipindisha kesi yao.
“Ninachotaka kwao ni huduma za matibabu kwa sababu hata wakinipa mshahara wa miezi minne niliyofanya kazi, sitaweza kufanya kazi sehemu nyingine  kwa sababu tayari ni mgonjwa,” anasema
Shabani  ambaye ana mke na watoto sita anasema amejaribu kutafuta msaada  kutoka kwa mashirika na taasisi  kama Kituo cha Haki za Binadamu(LHRC) na Baraza la Usuluhishi(CMA)
Si hivyo tu, bali pango la nyumba limekwisha na ameshavumiliwa na mwenye nyumba kwa miezi mitatu sasa.
Anasema mwajiri wake alimwambia kuwa  anatakiwa kuchangia shilingi elfu 50  kwa miezi kumi aliyofanya kazi lakini hakukuwa na mchango wowote katika mfuko wake.
“Kilichonishtua ni kuwa nilipokwenda kuangalia mafao yangu NSSF nilikuta hakuna mchango wangu hata mmoja,” anasema
Aidha Shabani analalamika kuwa  hata viongozi wa serikali za mitaa wanaonekana kupewa rushwa ili suala  lake lisitatuliwe.
Madhara ya kiafya yatokanayo na madini ya Uranium
 Madini ya uranium hutumika kutengeneza silaha za nyuklia ambazo zinapingwa vikali kutokana na uhatari wake.
Mabaki (residual)ya  madini hayo yanayotajwa kuwa na madhara makubwa kiafya katika mwili wa binadamu. Madhara hayo yanaweza kuwa ya kikemikali na kimionzi.
Sumu iliyopo katika madini hayo inaweza kuingia mwilini kwa kuvuta hewa yenye vumbi la uranium au kwa kula vitu vyenye chembe za madini hayo.
Vumbi au chembe hizo huingia katika mzunguko wa damu na kuchujwa katika figo jambo ambalo linasababisha figo kuathirika na kushindwa kufanya kazi.
Watu wanaofanya kazi katika maeneo au machimbo ya uranium, kama kubeba na kukanyaga  wapo hatarini kupata saratani pale wanapovuta hewa yenye vumbi lake au kumeza chembechembe zake.
Madhara ya mionzi kwa wachimbaji na wasagaji wa madini ya uranium nchini Marekani hayakugundulika mapema. Miaka ya 1940 na 50 ndipo wengi wao wlaipogundulika na saratani ya mapafu.
Mwaka 1962 takwimu za mahusiano kati ya uchimbaji wa uranium na saratani na mwaka 1990  serikali ya nchi hiyo iliunda sheria (RECA) kuwalinda na kuwalipa mafao walioathirika na madini hayo. Hadi sasa, zaidi ya asilimia 50 ya migodi ya uranium imetelekezwa.

MWALIMU AMUUA MWANAFUNZI KWA KUMCHOMA KISU



Mwalimu wa Shule ya Msingi Kwamwachalima, iliyopo katika Kijiji cha Kwamwachalima Kata ya Komkonga wilayani Handeni Mkoa wa Tanga, ametoweka baada ya kutuhumiwa kufanya mauaji ya kinyama kwa mwanafunzi wa darasa la tatu na kumjeruhi vibaya mwingine wa kidato cha pili.


Mwalimu huyo, Suhalungi Nangoma (23) anatafutwa na Polisi kwa tuhuma hizo
za kuua na kujeruhi kwa kisu wanafunzi hao ambao ni ndugu, na watoto wa mwalimu mwenzake, Ijumaa Mjaliwa.

Nangoma anatuhumiwa kumuua kwa kumchoma kisu kifuani binti huyo anayesoma darasa la tatu katika shule hiyo, Farihia Mjaliwa (9), kisha kumjeruhi kwa kumcharanga kisu tumboni  kaka wa binti huyo, Mohamed Farhia anayesoma kidato cha pili katika Sekondari Kisaza.


Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Jafari Mohamed alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema polisi wanaendelea kumsaka mtuhumiwa ili afikishwe mahakamani.


Taarifa zilizopatikana kutoka katika eneo la tukio na kuthibitishwa na Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Muhingo Rweyemamu zilieleza kuwa tukio hilo lilitokea saa 9:00 usiku Novemba 23, mwaka huu wakati mtuhumiwa alipowavamia watoto hao chumbani kwao na kuanza kuwashambulia kwa kisu. Baba mzazi wa watoto hao, Mjaliwa anafundisha shule moja ya Kwamwachalima anasema hawakuwahi kugombana.


Mtuhumiwa huyo ametenda kosa hilo huku akikabiliwa kesi ya kumpachika mimba mwanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari ya Kisaza.

Akisimulia mkasa uliowakuta watoto wake mbele ya mkuu wa wilaya, Mjaliwa alisema Mohamed ambaye alinusurika kifo, alichomwa kisu tumboni na kusababisha utumbo kutoka nje na kwamba sasa amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Korogwe, Magunga.

Kwa mujibu wa Mjaliwa, mtuhumiwa baada ya kufanya kitendo hicho alimgeukia mdogo mtu na kisha kumchoma kisu kifuani upande wa kushoto na kukiacha kikining’inia.

“Watoto hao walianza kupiga kelele kutoka na mashambulizi hayo, lakini mtuhumiwa alitimua mbio na kukimbilia kusikojulikana,” alisema Mjaliwa ambaye hakuwepo siku ya tukio.


“Cha kushangaza alikuwa nje kwa dhamana kwa kumpa mimba mwanafunzi,” alisema.
Habari zinadai kuwa siku ya tukio, baadhi ya walimu wa Shule ya Kwamwachalima walifanya kikao kifupi kujadili jinsi ya kumwekea dhamana Nangoma, iwapo angefikishwa mahakamani kwa kesi ya kumpachika mwanafunzi mimba.


Mwenyekiti wa Kamati ya Shule hiyo Ali Hatibu, alisema walimhoji majeruhi huyo kabla hajapoteza fahamu na kumtaja mwalimu huyo kwamba ndiye aliyemchoma kisu.


“Tuliingia chumbani kwa watoto na kukuta kumetapakaa damu nyingi, lakini binti huyu ambaye sasa ni marehemu tulikuta tayari ameshafariki dunia na alikuwa ameshikilia kisu, maana alichomwa kwenye moyo,” alisema Hatibu.


Mwalimu Mkuu wa Shule ya Kwamwachalima, Eva Msenga alisema kwamba siku ya tukio mchana alizungumza na mtuhumiwa baada ya kuona mwenendo wake hauridhishi na kwamba alimjibu kwamba alikuwa amechanganyikiwa kutokana na kesi inayomkabili.


Msenga alisema baadaye jioni alikuwa na watoto hao wakijisomea hadi saa tatu usiku, na kwamba muda huo aliwataka wakalale kwani muda ulikuwa umekwenda.


“Tuliagana na waliondoka kwenda kulala, baadaye usiku ndipo tuliposikia tukio hili na tuliambiwa kwamba mtuhumiwa alibisha hodi na watoto kwa kumfahamu walimfungulia kisha akawafanyia unyama huo wa kutisha,” alisimulia Msenga.

Rweyemamu akizungumza wakati akiwafariji wanafamilia hao alisema Serikali itachukua hatua za kumsaka mtuhumiwa popote alipo ili aweze kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Alisema hatua ya kwanza ambayo ofisi yake imechukua ni kuomba kufungwa kwa akaunti za mtuhumiwa na kwamba hilo linaweza kuwa msaada wa kunaswa kwake.

“Tutafanya kila namna kuhakikisha kwamba mwalimu huyu anakamatwa ili apambane na mkono wa sheria,” alisema mkuu huyo wa wilaya.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Jafari Mohamed alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba polisi wanaendelea kumsaka mtuhumiwa ili afikishwe mahakamani kwa kosa la mauaji.

Friday, November 23, 2012

Mahakama Yaamuru Madiwani Watano Kuilipa Chadema Sh15 Milioni

 
 Na:Na Mussa Juma

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Arusha, imewaamuru madiwani watano waliotimuliwa Chadema kulipa gharama za kesi waliyokuwa wamefungua kupinga kufukuzwa uanachama, vinginevyo watapelekwa magereza.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Charles Magesa alitoa hukumu hiyo jana baada ya Chadema kushinda kesi hiyo.Hakimu Magesa alisema madiwani hao wanapaswa kulipa Sh15 milioni ndani ya miezi miwili, wakishindwa watapelekwa gerezani.

Madiwani hao ni Estomih Mallah (aliyekuwa Naibu Meya ya Manispaa ya Arusha kipindi hicho), John Bayo aliyekuwa Diwani wa Elerai, Reuben Ngowi (Themi), Charles Mpanda (Kaloleni) na Rehema Mohamed aliyekuwa Diwani wa Viti Maalumu.

Pia, katika kesi hiyo ya madai Chadema walikuwa wakiwakilishwa na Wakili Method Kimomogoro, wakati wadaiwa hao walikuwa wakijitetea wenyewe baada ya aliyekuwa wakili wao kujitoa.Akisoma uamuzi huo, Hakimu Magesa alisema baada ya mahakama kupitia hoja za pande zote, imeona wadaiwa hao wanapaswa kulipa zaidi ya Sh15.1 milioni, kila mmoja anatakiwa kulipa zaidi ya Sh3.2 milioni katika kipindi kisichozidi miezi miwili.

Awali, kulikuwa na mvutano kati ya wadaiwa hao jambo lililosababisha kesi hiyo kusikilizwa kwa kipindi kirefu ambapo walitakiwa kueleza mahakama hiyo sababu ya kutokupelekwa gerezani, huku kila mmoja akitamka kiwango cha fedha ambacho angeweza kulipa kwa mwezi.

Kwa upande wake, Ngowi alisema ana uwezo wa kulipa Sh25,000 kwa mwezi, Mpanda Sh20,000, Mallah Sh20,000, Rehema Sh15,000 na Bayo Sh15,000 kwa mwezi bila kuonyesha mchanganuo wa kipato chao, jambo lililopingwa vikali na Wakili Kimomogoro kwamba kiwango hicho ni kidogo.

Hakimu Magesa alisema kisheria mtu akishinda kesi ana uwezo wa kuchagua hukumu ya kulipwa kwa kuchukua mali za mdaiwa au mlalamikiwa kupelekwa kifungoni.

“Kimsingi mtu anaposhinda kesi lazima alipwe gharama aliyotumia na iwapo mahakama itaridhia alipwe kwa kiwango hicho, itachukua muda mrefu kati ya miaka 10 na 16 kumaliza deni hilo, jambo litakalosababisha aliyeshinda kushindwa kuona matunda ya ushindi wake,” alisema Magesa.

Alisema fedha hizo wanapaswa kuzilipa mara mbili,  awamu ya kwanza inatakiwa kila mmoja kulipa zaidi ya Sh1.5 milioni na  wawe wamemaliza kwa miezi miwili na kwamba, iwapo watashindwa mdai anaweza kupeleka mchanganuo wa gharama za kumtunza mfungwa na mahakama kuupitia na baadaye kutoa amri

MAGAZETI YA LEO IJUMAA TAREHE 23/11/2012











Translate