tangazo

Wednesday, December 26, 2012

Watoto 140 wazaliwa mkesha Krismasi







Wamama wakiwa na watoto wao baada ya kujifungua.  

ZAIDI ya watoto 140 wamezaliwa katika mkesha wa kuamkia Sikukuu ya Krismasi katika hospitali za wilaya tatu ikiwamo hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam.

Miongoni mwa watoto hao ni kutoka katika hospitali ya Temeke ambayo idadi yao ni 53 ambapo wasichana ni 24 wavulana 29 na kati yao pacha ni mmoja.

Kutoka katika hospitali ya Amana wavulana ni 32 na wasichana 30 ni na mmoja wao ni pacha katika hospitali ya Taifa watoto watatu ambao kati yao wawili ni wavulana na msichana mmoja.

Akizungumza na waandishi wa habari Daktari wa zamu katika hospitali ya Amana, Pendo Kataponda alisema ni kawaida kupokea wajawazito na
kuwahudumia kipindi cha Krismasi kama ilivyo kwa siku za kawaida.

Kutoka hospitali ya Mwanayamala idadi ya watoto waliozaliwa kwenye mkesha huo ni 25 ambapo kati yao wasichana ni 10 na wavulana ni 15.

Kwa upande wao baadhi ya wazazi waliojifungua katika mkesha huo walielezea furaha zao  ambapo walisema wanamshukuru Mungu kwa kuwatunuku zawadi hizo.

Walisema kuwa  hali zao na afya zao watoto wao ni za kuridhisha kitendo ambacho kiliwafanya washindwe kuficha hisia zao za furaha waliyo kuwa nayo.

Mbali na kushukuru walitumia fursa hiyo kupaza sauti zao kuwataka wanawake wenye tabia za kutupa watoto kuacha mara moja kwani wanamuasi Mungu.

Mwasiti Omary mzazi kutoka katika Hospitali ya Temeke alisema kumekuwa na habari nyingi kuhusiana na kutelekezwa kwa watoto ama kutupwa kabisa ni jambo la kulaaniwa.

“Ni bora kama hutaki kuzaa ukatumia kinga au ukaacha kabisa kushiriki tendo la ndoa kuliko kuwatupa watu wasiokuwa na hatia “aliongeza.


No comments:

Translate