tangazo

Thursday, September 20, 2012

SUPERCLASICO DE LAS AMERICAS: Neymar aipa ushindi Brazil, yaipiga Argentina 2-1

Chapisha Toleo la kuchapisha
NEYMAR_v_MESSI
Penati ya Dakika ya 94 ya Neymar imeipa ushindi Brazil wa bao 2-1 leo Alfajiri katika Mechi ya kwanza ya SUPERCLASICO DE LAS AMERICAS iliyochezwa huko Goias, Brazil.
Brazil na Argentina, zikichezesha Wachezaji wale tu wanaocheza Soka lao kwenye Vilabu vilivyopo huko Marekani ya Kusini, zitarudiana hapo Oktoba 3 huko Resistencia, Argentina.
Katika Mechi hii, Argentina ndio waliotangulia kupata bao katika Dakika ya 20 kupitia Juan Manuel Martinez ambae alicheza vizuri pasi za moja mbili na Clemente Rodriguez.
Brazil walisawazisha Dakika 6 baadae baada ya mchezo safi wa Neymar kumfungulia Paulinho aliefunga.
Huku ngoma ikiwa inamalizika kwa sare ya 1-1, Mchezaji wa Argentina aliunawa mpira ndani ya boksi na Neymar kufunga Penati hiyo.
++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
VIKOSI:
ARGENTINA:
Oscar Ustari (Boca Juniors), Marcelo Barovero (River Plate), Esteban Andrada (Lanus), Gino Peruzzi (Velez Sarsfield), Maximiliano Caire (Colon de Santa Fe), Lisandro Lepez (Arsenal), Sebastian Dominguez (Velez Sarsfield), Leandro Desabato (Estudiantes de La Plata), Vergini Santiago (Newell's Old Boys), German Re (Estudiantes de La Plata), Clemente Rodriguez (Boca Juniors), Leonel Vangioni (Newell's Old Boys), Rodrigo Brana (Estudiantes de La Plata), Leandro Somoza (Boca Juniors), Leonardo Ponzio (River Plate), Mino Sanchez Juan (Boca Juniors), Maximiliano Rodriguez (Newell's Old Boys), Julio Buffarini (San Lorenzo), Ricardo Centurion (Racing Club), Cristian Chavez (Boca Juniors), Lucas Viatri (Boca Juniors), Rogelio Funes Mori (River Plate), Lucas Mugni (Colon de Santa Fe).
BRAZIL:
Cassio (Corinthians), Jefferson (Botafogo), Carlinhos (Fluminense), Marcos Rocha (Atletico Mineiro), Fabio Santos (Corinthians), Lucas Marques (Botafogo), Dede (Vasco), Rhodolfo (Sao Paulo), Rever (Atletico Mineiro), Arouca (Santos), Bernard (Atletico Mineiro), Fernando (Gremio), Jadson (Sao Paulo), Lucas (Sao Paulo), Paulinho (Corinthians), Ralf (Corinthians), Thiago Neves (Fluminense), Leandro Damiao (Internacional), Luis Fabiano (Sao Paulo), Neymar (Santos), Wellington Nem (Fluminense).

No comments:

Translate