tangazo

Sunday, July 15, 2012

El Bashir na Salva KIir wazungumza

Kando-kando ya mkutano wa viongozi wa nchi za Umoja wa Afrika, AU, marais wa Sudan na Sudan Kusini wamekutana kwa mara ya kwanza, tangu nchi zao kukaribia vita awali mwaka huu.
   Redio ya Sudan imeripoti kuwa Omar al-Bashir na Salva Kiir walizungumza kwa saaa moja mjini Addis Ababa, na baadae walisema wanataraji wataimarisha uhusiano baina ya nchi mbili zao - nchi zinazozozana juu ya mpaka na mafuta.
Viongozi katika mkutano wa AU wamezisihi nchi hizo zitatue ugomvi wao ifikapo tarehe mbili Agosti - muda uliowekwa na Umoja wa Mataifa.

No comments:

Translate