tangazo

Wednesday, August 15, 2012

HUENDA CHANJO YA UGONJWA WA EBOLA ISIPATIKANE KABISA

Virusi vya Ebola
                                                           Virus vya ugonjwa wa Ebola

Wanasayansi wanaoendesha utafiti kuhusu virusi vinavyosababisha ugonga wa Ebola, wameiambia BBC kuwa, chanjo inayoweza kutumiwa kuzuia maambukizi ya virusi hivyo huenda isifumbuliwe.

Wiki chahche zilizopita idara ya ulinzi ya Marekani, Pentagon, ilisitisha ufadhili wake kwa kampuni mbili ambazo zilikuwa zikiendesha utafiti huo.

Mmoja wa wataalamu katika jopo hilo amesema kuna uwezekano mkubwa wa chanjo hiyo itakayotumiwa kuzuia mkurupuko wa ugonjwa wa Ebola haitatumika.

Ugonjwa wa Ebola umetajwa kama moja ya magonjwa hatari na ya kuogofya zaidi ulimwenguni.

Virusi hivyo vinasababisha homa kali ambayo hufanya mtu kuvuja damu katika viungo vya ndani na hata kupitia sehemu zingine kama vile masikio, mapua na hata ngozi.

Wataalamu wanasema virusi hivyo ambavyo hushambulia chembe chembe nyeupe na mishipa ya damu na kusababisha mwasho wa ngozi, macho mekundu, kutapika na mauimivu ya viungo.

Katika miezi ya hivi karibuni watu 16, waliaga dunia Magharibi mwa Uganda, kutokana na ugonjwa huo.

Kufikia sasa hakuna tiba kamili ya ugonjwa huo ambao unaweza kusababisha vifo kwa asilimia 90 ya watu walioambukizwa virusi hivyo.

Mikakati ya kujaribu kufumbua chanjo ya kutibu na kuzuia virusi vya Ebola imefadhiliwa na Idara ya Ulinzi na Taasisi ya Kitaifa ya Afya nchini Marekani NIH.

Idara hizo mbili zimewekeza mamilioni ya dola kwa utafiti huku zikiwa na wasi wasi kuwa virusi hivyo vinaweza kutumiwa kama silaha za kibiolojia.

Kutokana na ufadhili huo, chanjo kadhaa zimefumbuliwa na tayari zimefanyiwa majaribio kwa wanyama na matokeo yake yamekuwa ya kuridhisha.

Kampuni mbili Sarepta na Tekmira tayari zimeanzisha majaribio ya tiba hiyo kwa binadamu.
Lakini kampuni hizo zimefahamaishwa na Idara ya Ulinzi ya Marekani kusitisha utafiti huo mwa muda
kutokana na ukosefu wa fedha.
Uamuzi wa mwisho kuhusu ikiwa ufadhili huo utarejelewa tena utatolewa

No comments:

Translate