tangazo

Saturday, August 25, 2012

Wachimba migodi waanza kurudi kazini

Kampuni ya migodi iliyokuwa chanzo cha mgomo wa ghasia Afrika Kusini, Lonmin, inasema kuwa wafanyakazi wake zaidi wamerudi kwenye mgodi wa Marikana, karibu na Rustenberg.
Polisi nje ya mgodi wa Marikana wakati wa mgomo

Juma lilopita wachimba migodi 34 waliogoma walipigwa risasi na polisi na kuuwawa, na kama 70 walijeruhiwa.

Serikali ya Afrika Kusini imeteua tume ya
majaji kuchunguza kilichotokea.

Lonmin inasema kuwa katika mgodi wa Eastern Shafts, huko Marikana, 57% ya wachimba migodi wako kazini Jumamosi.
Sehemu nyengine ya machimbo imefungwa kwa sababu ya mapumziko ya mwisho wa juma.

Kampuni inasema hali ni ya amani, na kwamba mazungumzo yanaendelea ili kushawishi wafanyakazi wote warudi kazini.

Lakini uchimbaji wa madini ya dhahabu nyeupe, platinum, ulisimamishwa kwenye mgodi huo zaidi ya majuma mawili yaliyopita kwa sababu ya mgomo, na bado kazi haikuanza.

Mazishi ya baadhi ya wachimba migodi waliokufa yamefanywa na mawaziri walihudhuria na kuahidi kuzisaidia familia za wachimba migodi hao.

Wakuu sasa wamethibitisha kuwa kati ya waliokufa, watano walikuwa wageni kutoka nchi za nje.

No comments:

Translate