tangazo

Thursday, August 23, 2012

Taharuki nchini Kenya baada ya mauaji



                                                   Tana River, Kenya

 Baadhi ya watu wamelazimika kutafuta hifadhi sokoni kwa kuhofia usalama wao.

 Mauaji hayo yalitokea wakati watu wenye silaha kutoka jamii ya Pokomo waliposhambulia kijiji kimoja katika eneo la Reketa huku wakiteketeza makaazi ya watu.

Mmoja wa wale walioathiriwa ameelezea BBC kwamba walishambuliwa usiku, ''hata tumekimbia kutoka kijiji chetu sasa. Walikuja kwa kijiji cha Riketa, watu walikuwa wanalala hata hawana habari wakavamia akina mama, watoto wote wamekufa hapa hapa.''

Alisema shambulizi hilo limewashangaza kwa sababu hata wakati mifugo wao wameingia kwenye mashamba, kuna njia ya kufidia, ''sisi kawaida yetu, hiyo mifugo inashikwa kisha unalipishwa. Sio kukatakata mifugo au kumaliza wachungaji.''

Naibu kamanda wa polisi mjini Mombasa, Joseph Kitur amesema uchunguzi wa awali umebainisha kuwa shambulio hilo lilifanywa na watu kutoka jamii ya Pokomo.

Jamii za Pokomo na Orma zimekuwa zikizozania malisho na maji tangu mwezi uliopita lakini shambulizi hili ndilo mbaya zaidi kutokea kati yao.

Mwaka wa 2001, karibu watu 130 walifariki wakati mzozo kati ya jamii hizo mbili ulipozuka.

Jamii ya Pokomo ni wakulima na huwa inategemea sana mto wa Tana kwa shughuli zao.
Jamii ya Orma ni wafugaji.

Mauaji hayo yameleta kumbukumbu za ghasia za baada ya uchaguzi za mwaka wa 2007, ambapo watu 1,200 walifariki katika mapigano.

No comments:

Translate