TAMASHA la Majahazi, ZIFF linalofanyika kila mwaka limeanza juzi kwa 
staili ya aina yake kwa mashindano ya Ngalawa kutoka Forodhani mpaka 
fukwe za Chukwani visiwani Zanzibar.
Ngalawa hizo zilipewa majina
 ya baadhi ya kampuni zinazodhamini tamasha hilo na Zanlink wanaotoa 
huduma ya mtandao ndiyo waliibuka washindi na kunyakua kiasi cha Sh 
200,000. 
Mshindi wa pili ilikuwa ni kampuni ya Zat iliyopata Sh 
150,000 na Mtoni Marine ilishika nafasi ya tatu na kupata kiasi cha Sh 
100,000.
Akizindua tamasha hilo, Afisa Mtendaji Mkuu wa ZIFF, 
Ikaweba Bunting alisema tamasha la mwaka huu kama yaliyopita 
limemejikita katika kuleta burudani, kuwaunganisha watu wa tamaduni 
mbalimbali, kutoa ajira kwa Watanzania hasa vijana na kuchangia katika 
pato la taifa.
“ZIFF ni kiungo muhimu katika kubadilishana 
utamaduni, kuanzia leo watu kutoka nchi mbalimbali wanakutana, tunaleta 
siku tisa za kubadilishana utamaduni na kujifunza, Watanzania itumieni 
fursa hii kujifunza na pia kuonyesha taswira nzuri ya taifa letu,” 
alisema Bunting na kuongeza;
“Tunaomba muendelee kutuunga mkono kwa kuwa kila mwaka wakati wa tamasha
 tunaajiri vijana wapatao mia nne, haya ni mafanikio makubwa kwetu na 
kwa taifa kwa ujumla,” alisema Bunting.
Tamasha la ZIFF 
litaendelea kwa siku tisa mpaka Julai 15, ambapo mbali na kuonyesha 
filamu pia litakuwa likisindikizwa na burudani za muziki kutoka kwa 
wanamuziki nyota wa ndani na nje ya Tanzania.
Nyota 
watakaolipamba tamasha mwaka huu ni pamoja Jose Chameleone (Uganda), 
Diamond, Linah, Barnaba, Roma, THT, Dossar, Tausi Women Group,Tazneem.
Upande
 wa filamu mwigizaji kutoka Marekani, Mario Van Peebles atakuwa mgeni 
mashuhuri wa mwaka huu na anatarajiwa kuzindua filamu yake, 'We The 
Party' katika ukumbi wa Cinema Century uliopo mlimani City jijini Dar es
 Salaam.
Wasanii wa filamu watakaohudhuria ni pamoja na Irene 
Uwoya, Jackline Wolper, Issa Musa, Jacob Steven, Steve Nyerere na 
wengine wengi.

 
No comments:
Post a Comment