Rose Ndauka
                                                          Aunt Ezekiel
                                                                Frola Mvungi
                                                              Jacqueline Wolper
SHEHE
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhadi Musa Salum amezifumua swaumu za 
baadhi ya mastaa ambao hufunga bila kufuata taratibu za dini ya Kiislam.
 Akizungumza na Ijumaa katika mahojiano maalum, Shehe huyo alisema funga
 ina taratibu zake hivyo mastaa wanaoingia kwenye ibada hiyo bila 
kuzifuata ni sawa na kushinda na njaa.
 Alisema kitendo cha mastaa 
kufunga kisha baada ya kufungua kuendelea kufanya mambo yaliyo kinyume 
na Uislam ni sawa na kuoga kisha kuingia kwenye tope.
 “Itakuwa ni 
jambo la ajabu kama utakuwa umefunga kisha kuendelea kuvaa vimini, 
kunywa pombe, kuzini au usiku unakwenda klabu. Wanaofanya hivyo ndani ya
 mwezi huu, ni sawa na kusema hawajafunga,” alisema shehe huyo.
 
Aidha, amewashauri mastaa Aunt Ezekiel, Jacqueline Wolper, Rose Ndauka 
na Flora Mvungi ambao katika siku za hivi karibuni walitangaza kusilimu 
kutobadilisha maamuzi yao kwani kufanya hivyo itakuwa ni kumcheza shere 
Mungu.
 “Kwa hawa waliobadili nawasihi wasirudi nyuma na hata 
wakifunga wafuate maandiko yanasemaje, wasipofanya hivyo mwisho wao 
unaweza kuwa motoni,” alisema Shehe Musa.




 
No comments:
Post a Comment